Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Fanya Vitu Vingi Kwa muda mchache (Get more done in less time)

Maisha yanahitaji kujipanga. Acha kuishi kihasara.
Wengi wetu hujishughulisha sana na vitu vingi visivyo na tija na kutusababishia uchovu na kwa kuwa havina matokeo makubwa shida nyingine huzaliwa  uhitaji wa pesa, msongo wa mawazo, mahusiano kuharibika, hujihisi hufai na kwa wenye Imani ndogo huishia kusema ukoo wetu una nuksi au nyota yangu imeibiwa.
Leo napenda kwanza ujue ukweli huu Kanuni ya Pareto inasema asilimia 20 ya vitu tufanyavyo vina uwezo wa kutupa matokeo ya asilimia 80 na kwa upande mwingine asilimia 80 ya mambo tufanyayo hutuletea matokeo ya asilimia 20.
Wengi wetu huishia kujishughulisha na vitu ambavyo ni asilimia 80 na tunapata matokeo asilimia 20. Mungu atusaidie tupange kufanya vitu vichache vyenye matokeo makubwa na tufurahie maisha.

Tabia hii ya kufanya mambo mengi yasiyo na tija na kutufanya kila siku tuko hoi imesababisha ndoa nyingi ziyumbe maana wengi wameishia kulala mzungu wa nne na wengine wamegawana vyumba. Hii ni hatari. TUBADILIKE>
Hapa ndipo huja suala la umuhimu wa kuimaliza siku kabla hujaianza.
Hakikisha huendi kitandani mpaka umepanga mambo ya kufanya siku inayofuata. Kitendo hichi kina faida kubwa sana ambayo wengi hawaifahamu.
Kimsingi unapopanga mambo ya kufanya siku inayofuata kwa lugha nyingine unahusisha ubongo wa ndani (subconscious mind).
Hivyo unapoenda kulala ubongo wako wa ndani (Subconsious Mind) huanza kufanyia kazi yale yote uliyoyapanga usiku maana yenyewe ipo kazini masaa 24. Utashangazwa jinsi mambo yako mengi yatakavyokuwa yamerahisishwa na kuifanya siku yako iwe na matokeo makubwa.
Jambo lingine la kuzingatia wakati wa kupanga รข€“ tengeneza utaratibu pia wa kujizawadia. Mfano wewe unafanya kazi ya mauzo na umepanga kuwapigia simu wateja watano kuwataarifu juu ya mali mpya zilizowasili.
Ukianza tu kupiga simu ya kwanza na mara umalizapo jizawadie sema kwa kunywa kahawa au chai mara moja tu yaani mnyonyo mmoja na sio kumaliza kikombe (One sip only). Na ukipiga tena simu ya pili unakunywa tena mara moja tu, vivyo hivyo mpaka unamaliza.
Hamasa itakuwa ikiongezeka ya kupiga simu nyingine ili upate kunywa tena. Maisha yanakuwa na radha nzuri na wakati huo huo unaendelea kuzalisha.
Mifano ipo mingi tuseme unasema nikimaliza repoti hii kabla ya saa tatu nitatoka nje kupunga upepo dakika tano. Hivyo ubongo wako utahakikisha unashughulika ndani ya muda uliopanga ili upate tano bora.
Kupanga kwa kujiwekea ukomo wa kumaliza shughuli Fulani una maana kubwa sana na siku zote usipende kuweka ukomo mrefu. Jitahidi kujibana ili kukamilisha unamaliza ndani ya wakati na hivyo utakuwa ukifanya mambo mengi kwa siku kuliko ulivyokuwa ukiishi pasi utaratibu wa kujipangia.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Akili Hisia (emotional intelligence).

Lea mtizamo wa kisayansi, akili hisia ni ule uwezo wa mtu kuweza kutawala anachokiona kwenye mazingira aliyomo. Hii inaamanisha kwamba aweze kutawala mazingira kwa kutumia akili ya hisia zake na wale waliomzunguka. Mtu atawezaje kuelewa kwa kutumia hisia, ishara zinazoonekana kwenye mahusiano mbalimbali bila kuambiwa sentensi au hata neno moja? Utawezaje kutawala hisia zako na za watu wengine katika mazingira uliyomo? Kuna hatua sita za kuchukua ili akili hisia zako zikupe mafanikio unayoyatafuta. #1. Hatua ya kwanza ni wewe mwenyewe kujitambua. Kujitambua ni kitu muhimu kabisa linapokuja suala la akili hisia au emotional intelligence (EQ). Hebu tujiulize ni kwanini? Bila akili hisia hatuna namna yeyote ya kujitathmini kwa vile vipaji ama tulivyo navyo, tusivyo navyo au tunavyohitaji kujifunza ili tuweze kufanikiwa katika mambo yetu mbalimbali. Utaishia kuwa kama kipofu, maana hutaona chochote katika mazingira yaliyokuzunguka. Utapata shida kubwa kutumia mikono isiyoonekana. Aki...

Timiza Malengo Yako na Joel Nanauka.

Ninamshukuru Mungu sana kuweza kuwa na waandishi mashuhuri wa kitanzania ambao wanaweza andika vitabu kwa lugha ya Kiswahili na kusaidia watanzania wengi zaidi. Kitabu cha Timiza Malengo ni kitabu cha aina yake na kamwe si cha kukosekana kwenye maktaba yako. Kama kuna kitu familia yako inabidi ikushukuru basi ni hichi kitabu. Mimi ni msomaji sana wa vitabu na niseme tu ukweli kitabu hichi ni hazina tosha na hakikisha unapata nakala yako. Wahenga walisema tusiandikie wino wakati mate yapo. Nilichokifanya ni kukupatia sehemu ya hichi kitabu kutoka ukurasa wa 29 hadi 40 neno kwa neon ujisomee na useme mwenyewe je uko tayari kukikosa hichi kitabu? Tafadhali fuatana name nikinukuu kitabu cha Joel Nanauka kwa idhini yake kama ifuatavyo:- NJIA MBILI ZA KUTAMBUA KUSUDI LA MAISHA YAKO: Siku moja wakati Tiger Woods anahojiwa na mtangazaji akamwabia ‘’It seems like you like golf so much’’ (Inaonekana kuwa unaipenda gofu sana).Tiger Woods akamjibu, ‘’Not only I like golf but I am golf,’’ a...

Siri ya Maisha ni nini?

Siri ya mafanikio inaishi wapi? Wewe unajitambua? Muda wako wa kujiweka huru umefika. Ninakuweka huru kuanzia sasa. Je, uko tayari? Anza na maswali haya: 1) Huwa unalisha tumbo lako kila siku? 2) Huwa unalisha ubongo wako kila siku? 3) Huwa unalisha moyo wako kila siku? Ninakuweka huru kwa kukulipa sarafu yenye pande tatu kwa majina yake ni: #1. Jana yako #2. Kesho yako #3. Sasa yako Mwendo wa jaribio (experiment) Kwanza. Leo ni leo. Anza kutembea kuelekea kwenye mafanikio yako. Unaijua njia? Anza kutembea kwa miguu yako miwili. Kama huna miguu na uanze kufanya kile unachoweza utoke hapo ulipo hadi sehemu nyingine. Tembea kama vile maisha yako yote yanategemeana na kutembea huko. Kiuhalisia kutembea kwako ndo muujiza wa kujiweka huru. Unashangaa? Ni hivi: Miili yetu inashibishwa sumu kibao kwa hewa tunayopumua na vyakula tunavyokula. Hewa ina Carbon dioxide kutoka kwenye moshi wa magari (pollution) na viwanda. Vyakula vina dawa za mimea(pesticides). Itapendeza k...