Ruka hadi kwenye maudhui makuu

UKWELI KUHUSU MAISHA

Maisha ni neno moja lakini lenye mana nyingi unapoamua kumyambulisha maana yake. Kufikia malengo utakayo kuyafikia nayo ni maisha na hili ni eneo nitakaloliongelea kwa kina siku ya leo.
Kutamani uwe vile na hivi ni rahisi sana lakini kuchukua hatua ya kutenda ndilo eneo ambalo wengi hushindwa na kuishia kuona maisha hayana maana yoyote. Wanadamu wanatakiwa kujua ya kwamba kutenda ni muujiza unaojiridhisha kwa watu wenye uthubutu na hili linatuthibitishia kusahau kabisa kutamani kuwa kama fulani bila kuchukua hatua ya utendaji.
Kwa kawaida huwa nawashauri watu ya kuwa chochote unachotamani kuwa nacho, tayari wengine wanacho. Kwa hiyo njia rahisi ni kukutana na hao ambao tayari wanavyo ili upate kujua yakupasa kunya nini ili nawe uweze kupata. Hii inamaanisha ya kuwa unakuwa tayari kupitia maumivu yatakayokufikisha unapotamani kufika, au ukaishia hatua ambayo hukuitamani kuifikia kwa kutofanya yale uliyoelekezwa kufanya. Yote kwa yote wewe ndiye mwamuzi.
Ni sawa na nadharia ihusishayo habu na rimu ya tairi ya gari – Je unapenda kuwa habu, au rimu? Ili uwe habu inamaanisha uwe mtu wa katikati Zaidi, na kuwa rimu ni kuwa mbali na utendaji au nguvu ya kuzuzungusha. Ninaposisitiza juu ya umuhimu wa nguvu iliyopo katika kuzamia kitu (kuweka macho, akili, nguvu kwenye kitu kimoja tu hata mtu akikuita inakuwa ngumu kumsikiliza kutokana na kuzama katika jambo moja), hii ni namna ya kulitazama suala zima la kuwa habu. Hivyo kung’ang’ana katikati kama habu ndicho kitu muhimu katka maisha yako, ndicho kitakachokutafautisha kati ya kuwa habu au rimu
Endelea kutafakari juu ya utendaji wa habu ili nawe katika maisha ujiweke kwenye nafasi ya habu na kitakachofuata ni maisha yako kuwa bora Zaidi.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Akili Hisia (emotional intelligence).

Lea mtizamo wa kisayansi, akili hisia ni ule uwezo wa mtu kuweza kutawala anachokiona kwenye mazingira aliyomo. Hii inaamanisha kwamba aweze kutawala mazingira kwa kutumia akili ya hisia zake na wale waliomzunguka. Mtu atawezaje kuelewa kwa kutumia hisia, ishara zinazoonekana kwenye mahusiano mbalimbali bila kuambiwa sentensi au hata neno moja? Utawezaje kutawala hisia zako na za watu wengine katika mazingira uliyomo? Kuna hatua sita za kuchukua ili akili hisia zako zikupe mafanikio unayoyatafuta. #1. Hatua ya kwanza ni wewe mwenyewe kujitambua. Kujitambua ni kitu muhimu kabisa linapokuja suala la akili hisia au emotional intelligence (EQ). Hebu tujiulize ni kwanini? Bila akili hisia hatuna namna yeyote ya kujitathmini kwa vile vipaji ama tulivyo navyo, tusivyo navyo au tunavyohitaji kujifunza ili tuweze kufanikiwa katika mambo yetu mbalimbali. Utaishia kuwa kama kipofu, maana hutaona chochote katika mazingira yaliyokuzunguka. Utapata shida kubwa kutumia mikono isiyoonekana. Aki...

Timiza Malengo Yako na Joel Nanauka.

Ninamshukuru Mungu sana kuweza kuwa na waandishi mashuhuri wa kitanzania ambao wanaweza andika vitabu kwa lugha ya Kiswahili na kusaidia watanzania wengi zaidi. Kitabu cha Timiza Malengo ni kitabu cha aina yake na kamwe si cha kukosekana kwenye maktaba yako. Kama kuna kitu familia yako inabidi ikushukuru basi ni hichi kitabu. Mimi ni msomaji sana wa vitabu na niseme tu ukweli kitabu hichi ni hazina tosha na hakikisha unapata nakala yako. Wahenga walisema tusiandikie wino wakati mate yapo. Nilichokifanya ni kukupatia sehemu ya hichi kitabu kutoka ukurasa wa 29 hadi 40 neno kwa neon ujisomee na useme mwenyewe je uko tayari kukikosa hichi kitabu? Tafadhali fuatana name nikinukuu kitabu cha Joel Nanauka kwa idhini yake kama ifuatavyo:- NJIA MBILI ZA KUTAMBUA KUSUDI LA MAISHA YAKO: Siku moja wakati Tiger Woods anahojiwa na mtangazaji akamwabia ‘’It seems like you like golf so much’’ (Inaonekana kuwa unaipenda gofu sana).Tiger Woods akamjibu, ‘’Not only I like golf but I am golf,’’ a...

Siri ya Maisha ni nini?

Siri ya mafanikio inaishi wapi? Wewe unajitambua? Muda wako wa kujiweka huru umefika. Ninakuweka huru kuanzia sasa. Je, uko tayari? Anza na maswali haya: 1) Huwa unalisha tumbo lako kila siku? 2) Huwa unalisha ubongo wako kila siku? 3) Huwa unalisha moyo wako kila siku? Ninakuweka huru kwa kukulipa sarafu yenye pande tatu kwa majina yake ni: #1. Jana yako #2. Kesho yako #3. Sasa yako Mwendo wa jaribio (experiment) Kwanza. Leo ni leo. Anza kutembea kuelekea kwenye mafanikio yako. Unaijua njia? Anza kutembea kwa miguu yako miwili. Kama huna miguu na uanze kufanya kile unachoweza utoke hapo ulipo hadi sehemu nyingine. Tembea kama vile maisha yako yote yanategemeana na kutembea huko. Kiuhalisia kutembea kwako ndo muujiza wa kujiweka huru. Unashangaa? Ni hivi: Miili yetu inashibishwa sumu kibao kwa hewa tunayopumua na vyakula tunavyokula. Hewa ina Carbon dioxide kutoka kwenye moshi wa magari (pollution) na viwanda. Vyakula vina dawa za mimea(pesticides). Itapendeza k...