Habari ya leo mpendwa msomaji wa Makala zangu za kila siku sijulikanazo kwa jina la Wazo La Leo.
Ni kawaida kusikia watu wakilalamika ya kuwa wanapenda sana kufanya biashara lakini tatizo hawana mtaji kuwawezesha kuanza biashara. Yawezekana hata wewe usomaye hii makala ni mmojawapo. Hili limewafanya walio wengi washindwe kuona mtaji wa kwanza ambao kila binadamu amezaliwa nao.
Ikumbukwe na kuamini ya kuwa mwenyezi Mungu katika uumbaji wake alihakikisha kila binaadamu aliyemuumba alimkabidhi mtaji wa kuendesha maisha yake pasi shida yoyote. Mtaji ninaoongelea hapa ni AKILI. Akili ni kila kila kitu linapokuja suala la mchakato wa kutatua matatizo (changamoto).
Shida kubwa kwa tulio wengi huwa hatutengi muda wa kufikiri na mbaya kuliko vyote hatuna tabia ya kukaa eneo tulivu ambalo ni muafaka kwa zoezi la kufikiri.
Kuna nyakati akili zetu hutupa mawazo (Ideas) nzuri sana kutekeleza na kufanikisha kile tumekuwa tunakitafuta kwa muda mrefu lakini kwa kujua au kutokujua mawazo haya huja na kuondoka kutokana na tabia yetu mbaya ya kutokua na utamaduni wa kuyaandika mawazo yote yanayotujia na kinachotokea mawazo haya hupotea na kamwe hatuwezi yakumbuka.
Katika Makala yangu ya jana nimeongelea suala la mtu kuwa na noti buku yenye ukubwa wa kuenea mfuko wa shati na leo naendelea kusisitiza ya kuwa hilo ni hitaji muhimu sana kwa kila anayetaka kubadili maisha yake. Hii itakuwezesha kuyapakua mawazo yako kirahisi kwa kuyaandika kwenye hicho kinoti buku.
Ikumbukwe kuwa ili kukuza akili yako/ufahamu, yakupasa kuifanyisha mazoezi mbalimbali kama ilivyo miili yetu tunapoifanyisha mazoezi na kujikuta tu wakakamavu na maradhi mbalimbali kutuachilia.
Nimalizie kwa kuanisha aina ya mazoezi ambayo akili haina budi kushughulishwa ili iweze kukua na kukusaidia kuendesha maisha yako kirahisi.
1. Kujisomea vitabu sahihi kutoka kwa watu mashuhuri
2. Kusikiliza video/audio zilizosheheni hotuba au mafunzo kutoka kwa watu waliofanikiwa
3. Kuhudhuria mafunzo sahihi, maana siku hizi vituko haviishi. Mafunzo mengine huharibu akili badala ya kujenga.
4. Kutengeneza mazingira ya kuwa unakutana na watu waliofanikiwa ili kupata wasaa wa kuwauliza na kupokea ushauri wao inapobidi.
5. Kushikamana na watu chanya na kuachana watu hasi kabisa.
6. Kuanza kuweka katika matendo mambo yote mazuri unayojifunza na kubwa zaidi ni kuendelea maana wengine ni moto wa mabua. Unakuta mtu amehamasika kwa siku tatu na baadae anarudia tabia zake zilezile alizozizoea (comfort zone). Hii ni sawa na kuchimba shimo na kulifukia au kujenga nyumba ya miti hewani. Yaani hakuna kinachofanyika. Kikubwa ukijifunza kitu kifanyie kazi mpaka kimekuwa sehemu ya maisha yako na hapo ndipo utaanza kuona mabadiliko.
7. Orodha inaendelea, lakini uhakika nilionao, akili yako itapevuka/itakua vizuri na kugeuka kuwa mtaji wako nambari moja katika maisha yako.
Ni kawaida kusikia watu wakilalamika ya kuwa wanapenda sana kufanya biashara lakini tatizo hawana mtaji kuwawezesha kuanza biashara. Yawezekana hata wewe usomaye hii makala ni mmojawapo. Hili limewafanya walio wengi washindwe kuona mtaji wa kwanza ambao kila binadamu amezaliwa nao.
Ikumbukwe na kuamini ya kuwa mwenyezi Mungu katika uumbaji wake alihakikisha kila binaadamu aliyemuumba alimkabidhi mtaji wa kuendesha maisha yake pasi shida yoyote. Mtaji ninaoongelea hapa ni AKILI. Akili ni kila kila kitu linapokuja suala la mchakato wa kutatua matatizo (changamoto).
Shida kubwa kwa tulio wengi huwa hatutengi muda wa kufikiri na mbaya kuliko vyote hatuna tabia ya kukaa eneo tulivu ambalo ni muafaka kwa zoezi la kufikiri.
Kuna nyakati akili zetu hutupa mawazo (Ideas) nzuri sana kutekeleza na kufanikisha kile tumekuwa tunakitafuta kwa muda mrefu lakini kwa kujua au kutokujua mawazo haya huja na kuondoka kutokana na tabia yetu mbaya ya kutokua na utamaduni wa kuyaandika mawazo yote yanayotujia na kinachotokea mawazo haya hupotea na kamwe hatuwezi yakumbuka.
Katika Makala yangu ya jana nimeongelea suala la mtu kuwa na noti buku yenye ukubwa wa kuenea mfuko wa shati na leo naendelea kusisitiza ya kuwa hilo ni hitaji muhimu sana kwa kila anayetaka kubadili maisha yake. Hii itakuwezesha kuyapakua mawazo yako kirahisi kwa kuyaandika kwenye hicho kinoti buku.
Ikumbukwe kuwa ili kukuza akili yako/ufahamu, yakupasa kuifanyisha mazoezi mbalimbali kama ilivyo miili yetu tunapoifanyisha mazoezi na kujikuta tu wakakamavu na maradhi mbalimbali kutuachilia.
Nimalizie kwa kuanisha aina ya mazoezi ambayo akili haina budi kushughulishwa ili iweze kukua na kukusaidia kuendesha maisha yako kirahisi.
1. Kujisomea vitabu sahihi kutoka kwa watu mashuhuri
2. Kusikiliza video/audio zilizosheheni hotuba au mafunzo kutoka kwa watu waliofanikiwa
3. Kuhudhuria mafunzo sahihi, maana siku hizi vituko haviishi. Mafunzo mengine huharibu akili badala ya kujenga.
4. Kutengeneza mazingira ya kuwa unakutana na watu waliofanikiwa ili kupata wasaa wa kuwauliza na kupokea ushauri wao inapobidi.
5. Kushikamana na watu chanya na kuachana watu hasi kabisa.
6. Kuanza kuweka katika matendo mambo yote mazuri unayojifunza na kubwa zaidi ni kuendelea maana wengine ni moto wa mabua. Unakuta mtu amehamasika kwa siku tatu na baadae anarudia tabia zake zilezile alizozizoea (comfort zone). Hii ni sawa na kuchimba shimo na kulifukia au kujenga nyumba ya miti hewani. Yaani hakuna kinachofanyika. Kikubwa ukijifunza kitu kifanyie kazi mpaka kimekuwa sehemu ya maisha yako na hapo ndipo utaanza kuona mabadiliko.
7. Orodha inaendelea, lakini uhakika nilionao, akili yako itapevuka/itakua vizuri na kugeuka kuwa mtaji wako nambari moja katika maisha yako.
Maoni
Chapisha Maoni