Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Maswala muhimu ya kujiuliza

Ninamshukuru Mungu kuiona siku nyingine tena. Leo nataka niongelee maswali muhimu maishani yampasayo kila mtu kujiuliza.
Ikumbukwe kwamba tunakaribia kuanza Mwaka mpya kwani tumebakiwa na mwezi mmoja tu. Hivyo nimeonelea vyema niongelee maswali manne muhimu mwanadamu anayejitambua hana budi kujiuliza katika maisha haya tuliyo nayo:-
1. Ni nini
2. Lini
3. Kwa nini
4. Kwa namna gani
Kimsingi kila mmoja wetu hana mudi kujua kusudio la yeye kuruhusiwa kuwepo hapa duniani. Kumbuka hatukuja kupumua tu tukapita. Liko kusudio maalum ambalo Mungu ameweka ndani yako ambalo anataka ulitimize.
Mimi na wewe yawezekana kabisa hatujawahi kukutana ana kwa ana ila uhakika nilio nao ni kwamba wewe ni mtu wa thamani sana kwani una uwezo mkubwa ajabu wa kuweza badilisha kabisa maisha yako na ukabaki kuwa simulizi. Hivyo kujua kwa hakika kusudio lako la kuwepo hapa duniani ni jambo kuu na la maana kwa kila mmoja wetu.
Kujua ni nini unahitaji si mwisho na kiuhakika hupoteza maana hadi pale utakapojua muda au siku maalumu ya hicho unachokitaka kuwa nacho. Hivyo ni vyema kabisa ukajua ni nini unahitaji na lini ukipate hii hukusaidia wewe kuulazimisha ubongo ufanye kazi kwa kasi kukamilisha hayo mawili. Haya ni maswali mazuri yanayotambulisha nini na lini.
Sasa baada ya kujua nini na lini unataka, ni muhimu kuelezea kwa undani ni kwa nini hicho unachohitaji ni muhimu. Hapa ni mithili ya gundi kushikamanisha nini, lini a kwa nini. Unapoelezea sababu za kuhitaji unacho hitaji, kiwango chako cha hamasa huwa juu maana unagusa hisia zako. Tendo hili mara moja huzalisha nguvu ya utekelezaji kwa umakini. Ninachomaanisha hapa ni kwamba kuwa na sababu kimsingi hukufanya ufanye kazi kwa kujituma.
Mwisho, ni kwa namna gani unaweza fanikisha ni swali lingine litakalokufanya sasa upange mikakati ambayo ni muhimu sana kukamilisha mduara wa nini, lini, kwa nini na kwa jinsi gani/namna gani.
Rafiki, anza sasa kuamsha ubongo wako kwa kujiuliza maswali haya muhimu ili uweze zalisha hamasa na juhudi kubwa ya utendaji na hivyo uzalishaji wako utaongezeka maradufu na thamani yako katika jamii itapanda.
Nikutakie siku njema na yenye Baraka tele.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Akili Hisia (emotional intelligence).

Lea mtizamo wa kisayansi, akili hisia ni ule uwezo wa mtu kuweza kutawala anachokiona kwenye mazingira aliyomo. Hii inaamanisha kwamba aweze kutawala mazingira kwa kutumia akili ya hisia zake na wale waliomzunguka. Mtu atawezaje kuelewa kwa kutumia hisia, ishara zinazoonekana kwenye mahusiano mbalimbali bila kuambiwa sentensi au hata neno moja? Utawezaje kutawala hisia zako na za watu wengine katika mazingira uliyomo? Kuna hatua sita za kuchukua ili akili hisia zako zikupe mafanikio unayoyatafuta. #1. Hatua ya kwanza ni wewe mwenyewe kujitambua. Kujitambua ni kitu muhimu kabisa linapokuja suala la akili hisia au emotional intelligence (EQ). Hebu tujiulize ni kwanini? Bila akili hisia hatuna namna yeyote ya kujitathmini kwa vile vipaji ama tulivyo navyo, tusivyo navyo au tunavyohitaji kujifunza ili tuweze kufanikiwa katika mambo yetu mbalimbali. Utaishia kuwa kama kipofu, maana hutaona chochote katika mazingira yaliyokuzunguka. Utapata shida kubwa kutumia mikono isiyoonekana. Aki...

Timiza Malengo Yako na Joel Nanauka.

Ninamshukuru Mungu sana kuweza kuwa na waandishi mashuhuri wa kitanzania ambao wanaweza andika vitabu kwa lugha ya Kiswahili na kusaidia watanzania wengi zaidi. Kitabu cha Timiza Malengo ni kitabu cha aina yake na kamwe si cha kukosekana kwenye maktaba yako. Kama kuna kitu familia yako inabidi ikushukuru basi ni hichi kitabu. Mimi ni msomaji sana wa vitabu na niseme tu ukweli kitabu hichi ni hazina tosha na hakikisha unapata nakala yako. Wahenga walisema tusiandikie wino wakati mate yapo. Nilichokifanya ni kukupatia sehemu ya hichi kitabu kutoka ukurasa wa 29 hadi 40 neno kwa neon ujisomee na useme mwenyewe je uko tayari kukikosa hichi kitabu? Tafadhali fuatana name nikinukuu kitabu cha Joel Nanauka kwa idhini yake kama ifuatavyo:- NJIA MBILI ZA KUTAMBUA KUSUDI LA MAISHA YAKO: Siku moja wakati Tiger Woods anahojiwa na mtangazaji akamwabia ‘’It seems like you like golf so much’’ (Inaonekana kuwa unaipenda gofu sana).Tiger Woods akamjibu, ‘’Not only I like golf but I am golf,’’ a...

CONSCIOUS NA SUB-CONCIOUS MIND

Wazo La Leo Hongera sana mwanakarakana ya ubongo kwa siku hii nyingine nzuri sana ya leo. Ni nafasi bora na ya kipekee sana kwetu kwenda kuweka juhudi kubwa ili kuweza kupata matokeo bora sana. Leo nimeona vyema nizungumzie maana ya maneno ambayo tumekuwa tukiyasikia mara kwa mara. Conscious na Subconscious. Kwanza unatakiwa uelewe "sub" maana yake nn, hii ni prefix...ikiwa na maana ya "below" something, sio negative or opposite that something. Kwa hiyo maana ya "conscious mind" ni kujitambua na subconscious mind means: internal sense of being ambayo consious mind haiwezi decipher, i mean kukupa maono halisi, wakristo wanaita nafsi, mfano mzuri wa activities za subconscious mind ni ndoto Conscious mind-ni kutumia akili wakati tendo fulani linafanyika. Hii inatokea pale mtu anapokuwa hana uzoefu wakati anafanya jambo/tendo fulani, kutokana na kutokuwa na uzoefu inabidi atumie uzingativu wakati wa kutekeleza jambo/tendo husika. kwa mfano mtu anayej...