Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Ukibadilika Kila Kitu Kina badilika

Namnukuu Jim Rohn ‘ Mafanikio ni pale unapokua umebadilika kiasi cha kuwa sumaku ya kuvuta mafanikio na wala usijidanganye kwa kufanya kazi sana kwa bidi ili kupata mafanikio. Mafanikio huvutwa na mtu aliyebadilika kiasi cha kuwa sumaku ya kuvuta mafanikio. Kubadilika ni shughuli pevu kushughulikia. Kazi kubwa ni kubadilika kifikra na hakuna njia nyingine Zaidi ya:-
1. Kujisomea vitabu kila siku na kupata maarifa mapya na unapochukua hatua ya kuyafanyia kazi mawazo mapya ndipo badiliko kamili kwako hutokea. Kwanini nasisitiza vitabu. Unaposoma kitabu kimoja unajifunza mambo ambayo yu mkini aliyekiandika imemchukua miaka 30 kuweza kuwa na hayo aliyoamua kuandika ili watu wengine waweze kujifunza. Hivyo kama utasoma kitabu kimoja kwa mwezi tafsiri yake ni kuwa umeweza kujifunza udhoefu wa mtu wa miaka 30 kwa mwezi mmoja. Sasa niambie utakapokuwa umesoma vitabu hamsini utakuwaje? Badiliko ni lazima na linanzia na fikra kwa kujaza mambo yenye tija na fikra taka kuondoka.
2. Kusikiliza/video/tapes za mafundisho kutoka kwa magwiji wa mafanikio kama kina Jim Rohn, Less Brown nk.
3. Kuhudhuria semina hata ikibidi kulipia pesa. Hua inaniuma sana pale mtu unamwambia semina ni Sh 20,000 na mtu analalamika ati kwa nini isingalikuwa bure. Kuna kanuni rahisi sana unatakiwa kuijua upatacho kwa urahisi hupotea kirahisi. Mwenye ufahamu na anase huo usemi. Angalia watu wa bahati nasibu mara tu wakipata mamilioni wanaishia kuchanganyikiwa na mwisho kufilisika kwakuwa hakuna jasho walilochangia kupata hayo mamilioni.
4. Kutana na watu chanya achana na watu hasi. Badiliko ni lazima.
Orodha yaweza endelezwa kadri uwezavyo, lakini jambo la muhimu ni kuwa mafanikio huvutwa na mtu aliyebadilika kiasi cha kuwa sumaku kuvuta mafanikio (Success is something you attract by a person you become’ Jim Rohn.
Watu wanalamika ati uchumi umebadilika maisha yamekuwa magumu. Ukweli ni kwamba maisha hayajabadilika ila sisi ndio tumebadilika kwa kutokuwa na maarifa ya kutosha kupambana na mazingira ya kiuchumi tuliyo nayo. Acha kupigania kubadili uchumi, shughulikia badiliko lako na mengine lazima yafuate mstari.
Mtu mmoja nilikuwa nikiongea naye nikiwa nimetoka Kempiski Hotel. Akasema hata wewe huwa unaingia hotel hii? Ni kamuuliza kwani kuna watu wanazuiliwa? Jibu akaniambia du hapo ni balaa soda tu ni Shs. 5,000 chakula takribani sahani shs 50,000 unawezaje kulipa pesa nyingi kiasi hicho? Hapo ni ghari sana. Nikamuuliza wapi ni rahisi? Jibu mitaani soda ni shs 700. Jibu nililompa ni kwamba haitakuja tokea huduma au vitu kuwa na bei ghari hata siku moja, ila kuna watu wanashindwa kumudu na wengine wanamudu. Tatizo sio bei bali ni watu. Siku ukibadilika hata macho yanabadilika kwani utaanza kuona viwanja kariakoo, Upanga, Masaki, Ocean view vikiuzwa Tshs. 700,000,000 na ukavinunua lakini ni wewe yule siku za nyuma ulikuwa huoni hivyo viwanja na ukaishia kujenga Kimara Bonyokwa. Badilika ndio jibu sahihi.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Akili Hisia (emotional intelligence).

Lea mtizamo wa kisayansi, akili hisia ni ule uwezo wa mtu kuweza kutawala anachokiona kwenye mazingira aliyomo. Hii inaamanisha kwamba aweze kutawala mazingira kwa kutumia akili ya hisia zake na wale waliomzunguka. Mtu atawezaje kuelewa kwa kutumia hisia, ishara zinazoonekana kwenye mahusiano mbalimbali bila kuambiwa sentensi au hata neno moja? Utawezaje kutawala hisia zako na za watu wengine katika mazingira uliyomo? Kuna hatua sita za kuchukua ili akili hisia zako zikupe mafanikio unayoyatafuta. #1. Hatua ya kwanza ni wewe mwenyewe kujitambua. Kujitambua ni kitu muhimu kabisa linapokuja suala la akili hisia au emotional intelligence (EQ). Hebu tujiulize ni kwanini? Bila akili hisia hatuna namna yeyote ya kujitathmini kwa vile vipaji ama tulivyo navyo, tusivyo navyo au tunavyohitaji kujifunza ili tuweze kufanikiwa katika mambo yetu mbalimbali. Utaishia kuwa kama kipofu, maana hutaona chochote katika mazingira yaliyokuzunguka. Utapata shida kubwa kutumia mikono isiyoonekana. Aki...

Timiza Malengo Yako na Joel Nanauka.

Ninamshukuru Mungu sana kuweza kuwa na waandishi mashuhuri wa kitanzania ambao wanaweza andika vitabu kwa lugha ya Kiswahili na kusaidia watanzania wengi zaidi. Kitabu cha Timiza Malengo ni kitabu cha aina yake na kamwe si cha kukosekana kwenye maktaba yako. Kama kuna kitu familia yako inabidi ikushukuru basi ni hichi kitabu. Mimi ni msomaji sana wa vitabu na niseme tu ukweli kitabu hichi ni hazina tosha na hakikisha unapata nakala yako. Wahenga walisema tusiandikie wino wakati mate yapo. Nilichokifanya ni kukupatia sehemu ya hichi kitabu kutoka ukurasa wa 29 hadi 40 neno kwa neon ujisomee na useme mwenyewe je uko tayari kukikosa hichi kitabu? Tafadhali fuatana name nikinukuu kitabu cha Joel Nanauka kwa idhini yake kama ifuatavyo:- NJIA MBILI ZA KUTAMBUA KUSUDI LA MAISHA YAKO: Siku moja wakati Tiger Woods anahojiwa na mtangazaji akamwabia ‘’It seems like you like golf so much’’ (Inaonekana kuwa unaipenda gofu sana).Tiger Woods akamjibu, ‘’Not only I like golf but I am golf,’’ a...

CONSCIOUS NA SUB-CONCIOUS MIND

Wazo La Leo Hongera sana mwanakarakana ya ubongo kwa siku hii nyingine nzuri sana ya leo. Ni nafasi bora na ya kipekee sana kwetu kwenda kuweka juhudi kubwa ili kuweza kupata matokeo bora sana. Leo nimeona vyema nizungumzie maana ya maneno ambayo tumekuwa tukiyasikia mara kwa mara. Conscious na Subconscious. Kwanza unatakiwa uelewe "sub" maana yake nn, hii ni prefix...ikiwa na maana ya "below" something, sio negative or opposite that something. Kwa hiyo maana ya "conscious mind" ni kujitambua na subconscious mind means: internal sense of being ambayo consious mind haiwezi decipher, i mean kukupa maono halisi, wakristo wanaita nafsi, mfano mzuri wa activities za subconscious mind ni ndoto Conscious mind-ni kutumia akili wakati tendo fulani linafanyika. Hii inatokea pale mtu anapokuwa hana uzoefu wakati anafanya jambo/tendo fulani, kutokana na kutokuwa na uzoefu inabidi atumie uzingativu wakati wa kutekeleza jambo/tendo husika. kwa mfano mtu anayej...