Karibu mfuatiliaji wa Makala sijulikanazo kama wazo la leo. Leo nimeonelea vyema niongelee juu ya nafasi yako katika uzalishaji, iwe umeajiliwa au unajishughulisha na shughuli binafsi – huna budi kujiweka katika nafasi itakayokufanya uwe mtu wa thamani katika uzalishaji na kwa uhakika utashangaa uzalishaji wako ukipanda kwa kasi maana utasaidika iwapo utafuata ushauri ambao ninakwenda kuuachilia kwako.
Kimsingi hakuna mwanadamu anayehitaji kuishi maisha yasiyokuwa na maana. Wengi wetu tunaishi pasipo kuwa na mwalimu/mentor/coach katika maisha. Naomba nikutangazie kuishi kwa namna hiyo kutakucheleweshea mafanikio yako. Ushauri wangu kwako chukua hatua haraka za kumtafuta mtu atakaye kuwa anakuongoza katika maisha. Amini usiamini ukichukua hatua utajionea mwenyewe maisha yako yanavyoanza kuboreka. Sijui naongea na mtu wa jinsi gani, lakini kwangu umri ni namba tu, vinginevyo hauna maana yoyote kimaisha kwani waweza badilisha maisha yako katika kipindi chochote.
Jambo ninalotaka kusisitiza ni kuwa uwe na sifa za kufundishika, acha kiburi kinachokuangamiza.
Sasa wengi mtaniuliza:- Mwalimu ni nani? Jibu ni yule mtu unayemkubali katika ujumla wa maisha yake kiasi kwamba unatamani uwe kama yeye. Ninachosisitiza hapa ni kwamba mwalimu/coach/mentor ni hitaji la muhimu sana kwa kila mwanadamu. Sina lugha ya kukueleza ukanielewa lakini huo ndio ushauri wangu kwako. Hata mimi unionavyo kufikia hatua hii niliyonayo ya kuweza kuwa mwalimu/mentor/coach kiasi cha kukubalika na watu wapatao 24 kwa sasa ni kwa kuwa ninaye mwalimu/coach/mentor wangu anayejulikana kwa jina la DR. AMANI MAKIRITA. Mungu amzidishe kila la heri katika maisha yake na familia. Amenitoa mbali na sioni pesa ya kumlipa nikatimiliza alichonifanyia katika maisha yangu. Kama ansoma Makala haya naomba apokee shukrani zangu za dhati.
Ngoja nikupe ufahamu kidogo uweze kujua umuhimu wa mwalimu katika maisha. Hadi niandikapo ujumbe huu ana watu wapatao 254 na mimi ni miongoni mwa hiyo idadi. Najua umeanza kuwaza ya kwamba anatumudu vipi? Ashukuriwe Mungu aliyetuletea teknologia ya wattsAp, wakati wengine wanaambukizana virusi vya selfie wengine hiyohiyo watssAp inatubadilishia maisha. Mwalimu wangu mpendwa katika kila siku iendayo kwa Mungu anatugawia maarifa adimu ambayo hata darasani huwezi kupata na ndio elimu ya msingi ili kuweza kuishi ukifurahia maisha. Elimu hii inaitwa elimu isiyo rasmi, yaani hakuna shule au chuo kinafundisha. Hii ndiyo inakufanya uwe tofauti na Bill Gate, Dangote, Mengi, Bakhresa, Manji, nisaidie kuendeleza orodha. Watu hawa karibia 97% hawana degree wala udaktari. Lakini ndio madaktari wa maisha. Wakati wewe unajivunia elimu na mbwembwe kibao ati umesoma sana huwezi uza karanga au maandazi, wenzako wenye elimu isiyo rasmi wanakusanya pesa kama mchanga. Unabaki kusema nimelogwa mimi, sina bahati, kweli wa mbili havai moja na misemo kadha wa kadha ukijihalilishia hali uliyonayo.
Naomba unielewe vizuri. Siidharau elimu hata kidogo. Mimi mwenyewe nimesoma kwa kiwango change name najiita msomi. Lakini nikuambie kitu kimoja – Msomi akibahatika kupata elimu isiyo rasmi na kuondokana na kiburi cha kujiona bora kwa ajili ya vyeti vyake vya darasani na ufaulu uliotukuka na kuishia hapo hapo pasi kuisakanya elimu isiyo rasmi - basi iko shida. Kimsingi ELIMU YA DARASANI + ELIMU ISIYO RASMI = MAISHA YENYE MAANA. Mwenye ufahamu na atambue hayo mahesabu. Mwanafunzi wangu Mariamu Manjole sidhani kama atakumbukwa kufundishwa name hiyo hesabu darasani kwani hata mimi nimeifahamu baadae sana.
Sasa naomba rudisha mawazo yako juu ya elimu isiyo rasmi juu ya kuwa na mwalimu/coach/mentor na matumizi ya WatsApp – Utajiuliza mbona watu 254 ni wengi inakuwaje mwalimu Dr. AMANI MAKIRITA KUWAMUDU? Jibu - Kinachofanyika ni kwamba sote katuingiza katika kundi moja la wattsAp lijulikanalo kwa jina la KISIMA CHA MAARIFA. Huko anatulisha hadi kutuzalisha sie akina Mwakitalu yaani katuibua kusikojulikana. Ninajivunia kuwa na Dr. AMANI MAKIRITA katika maisha yangu. Sijutii kukutana naye kimaisha. Narudia tena Mungu amzidishie mwalimu wangu.
Najua una maswali mengi juu ya hili kwa kuwa utaratibu wa kuwa na mwalimu /coach/mentor kwetu tulio wengi ni utamaduni wa kigeni lakini kwa wenzetu wa ulimwengu wa kwanza ni jambo la kawaida na ndio maana hali ya uchumi wao kwa walio wengi imeboreka sana ukilinganisha na sisi tusio na huo utamaduni. Mungu atusaidie maana twafa. Mwenye sikio na asikie maneno haya niyanenayo.
Naomba niishie hapa na endelea kunifuatilia kila siku nikikuletea Makala iitwayo wazo la leo.
Ni mimi mwalimu/coach/mentor wako ninayependa kuona unabadilika huko huko uliko nami ukinilipa mshahara wangu ambao ni shukrani utakazo kuwa ukizitoa kwa Mwenyezi Mungu ukisema hujutii kukutana nami kwenye mitandao ya kijamii maana wengi naamini hatufahamini japo mu wanafunzi wangu.
Kimsingi hakuna mwanadamu anayehitaji kuishi maisha yasiyokuwa na maana. Wengi wetu tunaishi pasipo kuwa na mwalimu/mentor/coach katika maisha. Naomba nikutangazie kuishi kwa namna hiyo kutakucheleweshea mafanikio yako. Ushauri wangu kwako chukua hatua haraka za kumtafuta mtu atakaye kuwa anakuongoza katika maisha. Amini usiamini ukichukua hatua utajionea mwenyewe maisha yako yanavyoanza kuboreka. Sijui naongea na mtu wa jinsi gani, lakini kwangu umri ni namba tu, vinginevyo hauna maana yoyote kimaisha kwani waweza badilisha maisha yako katika kipindi chochote.
Jambo ninalotaka kusisitiza ni kuwa uwe na sifa za kufundishika, acha kiburi kinachokuangamiza.
Sasa wengi mtaniuliza:- Mwalimu ni nani? Jibu ni yule mtu unayemkubali katika ujumla wa maisha yake kiasi kwamba unatamani uwe kama yeye. Ninachosisitiza hapa ni kwamba mwalimu/coach/mentor ni hitaji la muhimu sana kwa kila mwanadamu. Sina lugha ya kukueleza ukanielewa lakini huo ndio ushauri wangu kwako. Hata mimi unionavyo kufikia hatua hii niliyonayo ya kuweza kuwa mwalimu/mentor/coach kiasi cha kukubalika na watu wapatao 24 kwa sasa ni kwa kuwa ninaye mwalimu/coach/mentor wangu anayejulikana kwa jina la DR. AMANI MAKIRITA. Mungu amzidishe kila la heri katika maisha yake na familia. Amenitoa mbali na sioni pesa ya kumlipa nikatimiliza alichonifanyia katika maisha yangu. Kama ansoma Makala haya naomba apokee shukrani zangu za dhati.
Ngoja nikupe ufahamu kidogo uweze kujua umuhimu wa mwalimu katika maisha. Hadi niandikapo ujumbe huu ana watu wapatao 254 na mimi ni miongoni mwa hiyo idadi. Najua umeanza kuwaza ya kwamba anatumudu vipi? Ashukuriwe Mungu aliyetuletea teknologia ya wattsAp, wakati wengine wanaambukizana virusi vya selfie wengine hiyohiyo watssAp inatubadilishia maisha. Mwalimu wangu mpendwa katika kila siku iendayo kwa Mungu anatugawia maarifa adimu ambayo hata darasani huwezi kupata na ndio elimu ya msingi ili kuweza kuishi ukifurahia maisha. Elimu hii inaitwa elimu isiyo rasmi, yaani hakuna shule au chuo kinafundisha. Hii ndiyo inakufanya uwe tofauti na Bill Gate, Dangote, Mengi, Bakhresa, Manji, nisaidie kuendeleza orodha. Watu hawa karibia 97% hawana degree wala udaktari. Lakini ndio madaktari wa maisha. Wakati wewe unajivunia elimu na mbwembwe kibao ati umesoma sana huwezi uza karanga au maandazi, wenzako wenye elimu isiyo rasmi wanakusanya pesa kama mchanga. Unabaki kusema nimelogwa mimi, sina bahati, kweli wa mbili havai moja na misemo kadha wa kadha ukijihalilishia hali uliyonayo.
Naomba unielewe vizuri. Siidharau elimu hata kidogo. Mimi mwenyewe nimesoma kwa kiwango change name najiita msomi. Lakini nikuambie kitu kimoja – Msomi akibahatika kupata elimu isiyo rasmi na kuondokana na kiburi cha kujiona bora kwa ajili ya vyeti vyake vya darasani na ufaulu uliotukuka na kuishia hapo hapo pasi kuisakanya elimu isiyo rasmi - basi iko shida. Kimsingi ELIMU YA DARASANI + ELIMU ISIYO RASMI = MAISHA YENYE MAANA. Mwenye ufahamu na atambue hayo mahesabu. Mwanafunzi wangu Mariamu Manjole sidhani kama atakumbukwa kufundishwa name hiyo hesabu darasani kwani hata mimi nimeifahamu baadae sana.
Sasa naomba rudisha mawazo yako juu ya elimu isiyo rasmi juu ya kuwa na mwalimu/coach/mentor na matumizi ya WatsApp – Utajiuliza mbona watu 254 ni wengi inakuwaje mwalimu Dr. AMANI MAKIRITA KUWAMUDU? Jibu - Kinachofanyika ni kwamba sote katuingiza katika kundi moja la wattsAp lijulikanalo kwa jina la KISIMA CHA MAARIFA. Huko anatulisha hadi kutuzalisha sie akina Mwakitalu yaani katuibua kusikojulikana. Ninajivunia kuwa na Dr. AMANI MAKIRITA katika maisha yangu. Sijutii kukutana naye kimaisha. Narudia tena Mungu amzidishie mwalimu wangu.
Najua una maswali mengi juu ya hili kwa kuwa utaratibu wa kuwa na mwalimu /coach/mentor kwetu tulio wengi ni utamaduni wa kigeni lakini kwa wenzetu wa ulimwengu wa kwanza ni jambo la kawaida na ndio maana hali ya uchumi wao kwa walio wengi imeboreka sana ukilinganisha na sisi tusio na huo utamaduni. Mungu atusaidie maana twafa. Mwenye sikio na asikie maneno haya niyanenayo.
Naomba niishie hapa na endelea kunifuatilia kila siku nikikuletea Makala iitwayo wazo la leo.
Ni mimi mwalimu/coach/mentor wako ninayependa kuona unabadilika huko huko uliko nami ukinilipa mshahara wangu ambao ni shukrani utakazo kuwa ukizitoa kwa Mwenyezi Mungu ukisema hujutii kukutana nami kwenye mitandao ya kijamii maana wengi naamini hatufahamini japo mu wanafunzi wangu.
Maoni
Chapisha Maoni