Tunaishi nyakati ambazo Ninaziita ni nyakati za habari (Information age). Taarifa vidoleni.
Ukweli ni kwamba upande mmoja wa shilingi ni jambo Jema sana lakini upande wa pili ni jambo baya sana.
Kwa nini tuseme hayo.
1. Ni nyakati nzuri kwa sababu sasa hutumii nguvu na gharama nyingi kupata taarifa kwani ziko kiganjani.
2. Kipindi hichi ni kibaya kwa sababu taarifa nyingi ni mbaya kusikiliza na hata kuangalia, hivyo sehemu ya pili ya ubongo wako inayoitwa subconscious mind inaathirika sana. Na kumbuka sehemu hii ya akili kwanza huna udhibiti nayo lakini ndiyo eneo unalolitegemea kwa 90%. Kazi ya eneo hili ni kurekodi kila kitu unachosikia na unachoona na pili inaamsha matendo ambayo wewe huna udhibiti nayo. Nitakupa mfano mdogo na kwa kuwa site ni watu wazima tutaelewana.
Chukulia mtu anayependa kuangalia Picha za ngono sana. Kinachozalishwa ni kwamba tabia za mtu huyu zitaanza kujifunua kwa kufanya ngono sana mpaka jamii ikamtambua hivyo lakini mwenyewe akifanya anajutia kwa kuwa nguvu aliyoitengeza kumsukuma kufanya ngono ni kubwa mno na imefikia hatua hawezi kudhibiti. Hii ni hatari.
Mfano wa pili ni pale MTU anapopenda sana kuangalia Picha za kivita watu wakiuana sana. MTU wa jinsi hii katika maisha yake ana uwezekano mkubwa wa kuua na ikasemekana ameua bila kukusidia. Ushauri wangu kwa mfano huu wa pili kwa kukilinda kizazi chetu ni vyema tukawakataza kabisa watoto wetu na kuwaambia madhara. Hebu tuanze mapema kuwasaidia maana ndio wamezaliwa nyakati hizi sio sawa na sisi wahenga.
Kwa hiyo ni LAZIMA TUWE WACHAGUZI SANA WA NINI TUNASIKILIZA NA NINI TUNAANGALIA ILI TULINDE SUBCONTIOUS MINDS ZETU.
TVs NA MAGAZETI VINAONGOZA KUHARIBU subconscious MIND - utafiti unaonyesha 90% ya habari zake si nzuri kabisa zinatuharibu. Binafsi kwa ridhaa yangu siangalii TV na sisomi magazeti kabisa ikitokea labda Niko Restraurant na kuna TV au rafiki kanisisitiza kusoma habari fulani kwenye gazeti fulani, basi nitasoma hapo tu na kuliacha gazeti. Ushauri wangu chagua vipindi bora tu japo ushawishi wa kuangalia usivyochagua pia ni mkubwa. Mungu atusaidie.
Naomba niishie hapa kwa Leo nikikusihi kujilinda na unayoyasikia ili tujenge maisha bora.
Ni mimi mwalimu/coach - Seth Simon Mwakitalu 0788 493836/07140574/0754441325
KARAKANA YA UBONGO
Maoni
Chapisha Maoni