Ninamshukuru sana Mungu kuiona siku ya leo. Leo napenda kuzungumzia juu ya nguvu ya hamasa.
Naliongelea hili ili kila mtu aone jinsi anavyoweza kujiwezesha kuwa katika hisia chanya.
Kimsingi napenda kila mmoja ajue ukweli kwamba katika kila hali kuna chaguzi tunafanya.
Kitendo hichi cha kufanya uchaguzi ni takribani cha kila siku au kwa lugha nyingine ndio maisha yetu ya kila siku lazima ufanye chaguzi.
Ili kuweza kupata uelewa vizuri wa kujiwezesha kuwa na hisia chanya naomba nikupitishe katika vipengele vifuatavyo:-
Hofu - wakati wowote tunapokuwa watu wa kushughulikia hali iliyotufanya tupoteze amani au furaha tuliyokuwa nayo matokeo yake tunajawa na hofu ya kupata maumivu zaidi. Maumivu haya kamwe sio halisia bali ni onyo ya kuwa kama mambo hayatobadilika, basi hali iliyo mbele yetu itakuwa mbaya zaidi.
Hili lawezea kukutokea katika maisha. Mfano unapofukuzwa kazi ghafla, huingiwa na hofu ya maisha kuwa chini ya kiwango ulichokuwa ukiishi kwa sababu ya uhakika wa mshahara na marupurupu. Hivyo iwapo aliyeguswa na hili hatoamini ya kuwa maisha yatakuwa mazuri baadae, basi ataanza kuandamwa na mambo yafuatayo:-
Maumivu: Kuanza kupoteza matumaini ya mambo ambayo amekuwa akiyategemea kuwa nayo kama umiliki wa nyumba, kusomesha watoto shule bora, mavazi mazuri, Lishe nzuri nk.
Matumaini ya kuwa na furaha hutoweka na Maumivu kuzaliwa. Hili ni dhahiri tunapoanza kuhisi kuondokewa na mapenzi, furaha au faraja iliyokuwepo kwa kuwa kazini basi uwepo na maumivu moyoni huzaliwa.
Hili huwapata wengi mfano watu wanapofikia hatua ya kuvunja uchumba, mtu anapoishiwa fedha au anapojikuta ananenepeana na kupoteza umbile zuri.
Naliongelea hili ili kila mtu aone jinsi anavyoweza kujiwezesha kuwa katika hisia chanya.
Kimsingi napenda kila mmoja ajue ukweli kwamba katika kila hali kuna chaguzi tunafanya.
Kitendo hichi cha kufanya uchaguzi ni takribani cha kila siku au kwa lugha nyingine ndio maisha yetu ya kila siku lazima ufanye chaguzi.
Ili kuweza kupata uelewa vizuri wa kujiwezesha kuwa na hisia chanya naomba nikupitishe katika vipengele vifuatavyo:-
Hofu - wakati wowote tunapokuwa watu wa kushughulikia hali iliyotufanya tupoteze amani au furaha tuliyokuwa nayo matokeo yake tunajawa na hofu ya kupata maumivu zaidi. Maumivu haya kamwe sio halisia bali ni onyo ya kuwa kama mambo hayatobadilika, basi hali iliyo mbele yetu itakuwa mbaya zaidi.
Hili lawezea kukutokea katika maisha. Mfano unapofukuzwa kazi ghafla, huingiwa na hofu ya maisha kuwa chini ya kiwango ulichokuwa ukiishi kwa sababu ya uhakika wa mshahara na marupurupu. Hivyo iwapo aliyeguswa na hili hatoamini ya kuwa maisha yatakuwa mazuri baadae, basi ataanza kuandamwa na mambo yafuatayo:-
Maumivu: Kuanza kupoteza matumaini ya mambo ambayo amekuwa akiyategemea kuwa nayo kama umiliki wa nyumba, kusomesha watoto shule bora, mavazi mazuri, Lishe nzuri nk.
Matumaini ya kuwa na furaha hutoweka na Maumivu kuzaliwa. Hili ni dhahiri tunapoanza kuhisi kuondokewa na mapenzi, furaha au faraja iliyokuwepo kwa kuwa kazini basi uwepo na maumivu moyoni huzaliwa.
Hili huwapata wengi mfano watu wanapofikia hatua ya kuvunja uchumba, mtu anapoishiwa fedha au anapojikuta ananenepeana na kupoteza umbile zuri.
Hasira - Tunapokuwa tumeumizwa tunaanza kuwa na machungu na watu ambao wamekuwa wakichangia tujisikie kupendwa, kuwa na furaha na Faraja katika maisha.
Kuchanganyikiwa - kule kujua ya kuwa ungelikuwa na maisha mazuri kunakufikirisha ya kuwa hutoweza kurudia hali ya matumaini uliyokuwa nayo mwanzo na kuona sasa maisha yamepoteza radha au umaana. Matokeo yake tunaanza kuchukua hatua za kujinasua: kujisomea vitabu tunavyotegemea vitatusaidia, wengine huamua kurudi shule, kuhudhuria semina mbalimbali. Tunapokuwa tukiendelea kujifunza, tunaanza kujiamini, tunapata Tumaini, na hamasa tena na kuanza kupata matarajio ya kufanikiwa katika maisha yetu. Lakini tunapoanza tena kuingia kwenye misukosuko ya kimaisha kwa mambo yetu kutokwenda vizuri huishia kukata tamaa na kuanza kujikutaa katika hali ya...
Kupoteza mategemeo - unapokata tamaa kuendelea kufanyia kazi malengo yako, matokeo yake ni kupoteza kabisa mategemeo uliyokuwa umeyajenga. Hapa ndio mwanzo wa mtiririko wa Maumivu. Hatimaye kupoteza mategemeo kunazaa...
Kujisikia vibaya moyoni: Hii ni hatari ambayo husababisha mtu kuwaza kujizuru. Unatambua ya kuwa unahitaji kubadilika, lakini unajikuta huhitaji tena kujaribu. Kila Mara unaishiwa nguvu kujaribu tena, unabaki kujisikia vibaya moyoni. Ni mpaka pale utakapopata ujasiri tena wa kujaribu tena, vinginevyo utajisikia...
Kutojitosheleza - Umepoteza tumaini. Unaanza kujiona huna thamani tena. Hujiamini tena ya kuwa una uwezo wa kubadili maisha yako tena. Unajihisi kupungukiwa fedha, afya, kazi/fani, hali ya kiroho, mahusiano na maisha kwa ujumla na wanaokuzunguka unaona kana kwamba wamekutenga.
Hapa ndipo linakuja suala la kutafuta msaada kutoka kwa mtu anayeweza kukusaidia kuanza kujiamini tena, Vinginevyo usipopata mtu wa jinsi hiyo utaelekea hatua ya...
Hapa ndipo linakuja suala la kutafuta msaada kutoka kwa mtu anayeweza kukusaidia kuanza kujiamini tena, Vinginevyo usipopata mtu wa jinsi hiyo utaelekea hatua ya...
Mkandamizo wa mawazo: Katika hatua hii utakuwa umeelemewa na Maumivu moyoni. Hapa wengi huishia kuwa mateja wa dawa za kulevya na maisha kuwa ya hovyo kupindukia.
Msaada waweza patikana kwa majirani na pia kumgeukia Mungu.
Nimalizie kwa kusema kuwa iwapo wewe na mimi tunayapenda maisha ni LAZIMA TUAMINI HAJALISHI TUNA HALI MBAYA KIASI GANI MAISHA YATABADILIKA NA KUWA BORA ZAIDI YA AWALI. NI KWELI WAWEZA KOSA CHAKULA KWA MIEZI KADHAA. KUMBUKA JAMBO MOJA TU YA KUWA SHIDA ULIYONAYO NI YA KITAMBO KAMWE HAIWEZI DUMU MILELE.
Ni mimi mwalimu wako/coach Seth Simon Mwakitalu 0754 441325/0788493836/0714051174.
Msaada waweza patikana kwa majirani na pia kumgeukia Mungu.
Nimalizie kwa kusema kuwa iwapo wewe na mimi tunayapenda maisha ni LAZIMA TUAMINI HAJALISHI TUNA HALI MBAYA KIASI GANI MAISHA YATABADILIKA NA KUWA BORA ZAIDI YA AWALI. NI KWELI WAWEZA KOSA CHAKULA KWA MIEZI KADHAA. KUMBUKA JAMBO MOJA TU YA KUWA SHIDA ULIYONAYO NI YA KITAMBO KAMWE HAIWEZI DUMU MILELE.
Ni mimi mwalimu wako/coach Seth Simon Mwakitalu 0754 441325/0788493836/0714051174.
Maoni
Chapisha Maoni