Ninamshukuru sana Mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na nchi kwa kutupa siku nyingine yaani tarehe 1 Disemba, 2017. Tarehe hii ni mwanzo wa mwisho wa mwezi katika mwaka. Ninampa sifa na utukufu Muumba kwa kutulinda hadi kufikia siku ya leo.
Ninazidi kumuomba Mungu azidi kunijalia pumzi nizidi kutenda kusudio la mimi kuwepo hapa duniani. Ni matamanio yangu ya kuwa nikifa niwe nimetoa kila kitu alichokiweka ndani yangu na hivyo kuacha alama kama kumbukumbu ya kuwepo kwangu. Sifa na utukufu namwachia Yeye aliye juu.
Leo tunakwenda kujifunza mikakati sita ya kujijengea kujiamini. Naokuomba fuatana nami katika safari hii nikianza kudadavua moja baada ya nyingine:-
1. Kila siku jijengee tabia ya kujikumbusha yote uliyoyafanya kwa uzuri
a. Mkazo ubaki katika kile ulichofanikisha kukikamilisha haijalishi ni kikubwa au kidogo kiasi gani - Kamwe usifanye kosa la kupuuzia kitendo hichi.
b. Tumia utaratibu ufuatao kukujengea tabia maridhawa kila siku
i. Kupangilia mambo ya kufanya siku inayofuata. Tendo hili ni vyema ukalifanya kabla ya kulala kwani itasaidia ubongo wa ndani (subconscious mind) kunasa na ukiwa umelala mipango yako ikawa inafanyiwa mchakato na ukiamka tu ni suala la kufuatilia vile ulivyopanga kutekeleza. Ushauri wangu mipango mkakati izingatie vipaumbele mfano ahadi ulizoweka za kukutana na watu, miradi unayotazamia kuifanya na kadhalika. Hivyo kila siku usiku au asubuhi ya siku inayofuata jijengee tabia ya kutathimini jana yako au kutwa yako kutokana na mipango mikakati yako.
ii. Kuchukua hatua ya kutenda – Fanya kazi kwa kuzingatia vipaumbele vyako ambavyo vitakusogeza kukamilisha malengo yako sema labda umejipangia malengo ya siku sitini basi kila kinachochangia kukusogeza kwenye hayo malengo kipe kipaumbele.
iii. Kujifunza –Jenga tabia kila siku kutanua uelewa wako kupitia kujisomea, kusikiliza cassete za mafundisho, videos, mwalimu wako wa maisha – mentor (kitu hichi ni kigeni sana kwetu watanzania, kwani unaona mtu anaishi pasi kuwa na mtu anayemwongoza katika maisha. Kimsingi huna budi kumchagua mtu ambaye unatamani kuwa kama yeye ili awe ndiye mwalimu wako. Hili ni muhimu sana, nakuomba usipuuzie na kuhudhuria mafunzo mbalimbali hata ikibidi kulipia fanya hivyo.
iv. Kupumzika (Relaxation) – Ondoa msongo wa mawazo wa kila siku. Tahajudi (Meditate), sikiliza muziki na pata muda na familia huku ukiwa umezima simu kabisa.
v. Fikiri – Pata muda wa kuitafakari siku yako ilivyokuwa. Pitia malengo yako na jaribu kuyatengenezea picha kwenye ubongo kana kwamba sasa unamiliki, pata mawazo mapya (develop new ideas), tumia noti buku yako kuyanukuu.
2. Jifundishe wewe mwenyewe, kama ambavyo ungelimsaidia mtu mwingine kuondokana na changamoto, basi jifanyie vivyo hivyo mwenyewe.
3. Jisomee kutoka kwa watu waliokutangulia wenye kukufanya ujisikie u bora kuliko ulivyokuwa ukijifikiria (Read Inspiring biographies and autobiographies).
a. Maisha yasiyo na changamoto ni udanganyifu na sijui utayapata wapi.
b. Tambua na kubali ya kuwa katika maisha utakutana na kupanda na kushukuka. Hayo ndio maisha halisia na si vinginevyo. Kila mtu hupitia hakuna asiyepitia kupanda na kushuka. Hiyo ndio tfsiri sahihi ya maisha.
c. Kujiamini kwako hukua pale tu unapokabiliana na changamoto za kimaisha na sio kuzipa mgongo. Haimanishi utaweza kuzishinda changamoto zote lakini kikubwa ni mtazamo wako sahihi utakufanya upate ushindi katika changamoto lukuki kuliko
d. Kuwa mtu wa shukrani
4. Jijengee wigo mzuri wa kusaidiana. Ishi vizuri na watu. Wafanyie watu yale yote ungependa wewe kufanyiwa. Jenga mahusiano mazuri na watu na mengine mengi. Kifupi kuwa mtu wa watu. Acha majivuno hata kama umefanikiwa kiasi gani. Jishushe. Kumbuka wahenga walisema aliye juu mngoje chini. Naomba hili lisiwe kwako.
5. Jisukume kuhakikisha malengo yako ya muda mfupi unakamilisha.
a. Hakuna njia rahisi na ya muhimu kujijengea kujiamini kama kuhakikisha unakamilisha yale uliyojisemea utafanya.
b. Unahitaji kupoteza kitu fulani kabla ya kupata ushindi. Huwezi kuwa mkimbiaji mzuri ukiwa na kitambi. Ni lazima upoteze kitambi ndipo ushinde mbio. Huwezi kuwa mtu chanya mpaka upoteze marafiki hasi na kadhalika.
6. Jifanyie kitu kwa ajili yako kila wiki
- Tafuta namna ya kusherehekea yale uliyoyafanikisha katika wiki husika. Unadhani hustahili? Kama ni ‘HAPANA’ anza tena na hatua ya kwanza hapo juu hadi ufikie hatua ya sita. Lakini kama unastahili, tafadhali jifanye kitu cha kujipongeza.
Kumbuka safari ya kujijengea kujiamini inaanzia na ushindi upatikanao katika kila wiki. Jifunze kujipongeza.
Ninazidi kumuomba Mungu azidi kunijalia pumzi nizidi kutenda kusudio la mimi kuwepo hapa duniani. Ni matamanio yangu ya kuwa nikifa niwe nimetoa kila kitu alichokiweka ndani yangu na hivyo kuacha alama kama kumbukumbu ya kuwepo kwangu. Sifa na utukufu namwachia Yeye aliye juu.
Leo tunakwenda kujifunza mikakati sita ya kujijengea kujiamini. Naokuomba fuatana nami katika safari hii nikianza kudadavua moja baada ya nyingine:-
1. Kila siku jijengee tabia ya kujikumbusha yote uliyoyafanya kwa uzuri
a. Mkazo ubaki katika kile ulichofanikisha kukikamilisha haijalishi ni kikubwa au kidogo kiasi gani - Kamwe usifanye kosa la kupuuzia kitendo hichi.
b. Tumia utaratibu ufuatao kukujengea tabia maridhawa kila siku
i. Kupangilia mambo ya kufanya siku inayofuata. Tendo hili ni vyema ukalifanya kabla ya kulala kwani itasaidia ubongo wa ndani (subconscious mind) kunasa na ukiwa umelala mipango yako ikawa inafanyiwa mchakato na ukiamka tu ni suala la kufuatilia vile ulivyopanga kutekeleza. Ushauri wangu mipango mkakati izingatie vipaumbele mfano ahadi ulizoweka za kukutana na watu, miradi unayotazamia kuifanya na kadhalika. Hivyo kila siku usiku au asubuhi ya siku inayofuata jijengee tabia ya kutathimini jana yako au kutwa yako kutokana na mipango mikakati yako.
ii. Kuchukua hatua ya kutenda – Fanya kazi kwa kuzingatia vipaumbele vyako ambavyo vitakusogeza kukamilisha malengo yako sema labda umejipangia malengo ya siku sitini basi kila kinachochangia kukusogeza kwenye hayo malengo kipe kipaumbele.
iii. Kujifunza –Jenga tabia kila siku kutanua uelewa wako kupitia kujisomea, kusikiliza cassete za mafundisho, videos, mwalimu wako wa maisha – mentor (kitu hichi ni kigeni sana kwetu watanzania, kwani unaona mtu anaishi pasi kuwa na mtu anayemwongoza katika maisha. Kimsingi huna budi kumchagua mtu ambaye unatamani kuwa kama yeye ili awe ndiye mwalimu wako. Hili ni muhimu sana, nakuomba usipuuzie na kuhudhuria mafunzo mbalimbali hata ikibidi kulipia fanya hivyo.
iv. Kupumzika (Relaxation) – Ondoa msongo wa mawazo wa kila siku. Tahajudi (Meditate), sikiliza muziki na pata muda na familia huku ukiwa umezima simu kabisa.
v. Fikiri – Pata muda wa kuitafakari siku yako ilivyokuwa. Pitia malengo yako na jaribu kuyatengenezea picha kwenye ubongo kana kwamba sasa unamiliki, pata mawazo mapya (develop new ideas), tumia noti buku yako kuyanukuu.
2. Jifundishe wewe mwenyewe, kama ambavyo ungelimsaidia mtu mwingine kuondokana na changamoto, basi jifanyie vivyo hivyo mwenyewe.
3. Jisomee kutoka kwa watu waliokutangulia wenye kukufanya ujisikie u bora kuliko ulivyokuwa ukijifikiria (Read Inspiring biographies and autobiographies).
a. Maisha yasiyo na changamoto ni udanganyifu na sijui utayapata wapi.
b. Tambua na kubali ya kuwa katika maisha utakutana na kupanda na kushukuka. Hayo ndio maisha halisia na si vinginevyo. Kila mtu hupitia hakuna asiyepitia kupanda na kushuka. Hiyo ndio tfsiri sahihi ya maisha.
c. Kujiamini kwako hukua pale tu unapokabiliana na changamoto za kimaisha na sio kuzipa mgongo. Haimanishi utaweza kuzishinda changamoto zote lakini kikubwa ni mtazamo wako sahihi utakufanya upate ushindi katika changamoto lukuki kuliko
d. Kuwa mtu wa shukrani
4. Jijengee wigo mzuri wa kusaidiana. Ishi vizuri na watu. Wafanyie watu yale yote ungependa wewe kufanyiwa. Jenga mahusiano mazuri na watu na mengine mengi. Kifupi kuwa mtu wa watu. Acha majivuno hata kama umefanikiwa kiasi gani. Jishushe. Kumbuka wahenga walisema aliye juu mngoje chini. Naomba hili lisiwe kwako.
5. Jisukume kuhakikisha malengo yako ya muda mfupi unakamilisha.
a. Hakuna njia rahisi na ya muhimu kujijengea kujiamini kama kuhakikisha unakamilisha yale uliyojisemea utafanya.
b. Unahitaji kupoteza kitu fulani kabla ya kupata ushindi. Huwezi kuwa mkimbiaji mzuri ukiwa na kitambi. Ni lazima upoteze kitambi ndipo ushinde mbio. Huwezi kuwa mtu chanya mpaka upoteze marafiki hasi na kadhalika.
6. Jifanyie kitu kwa ajili yako kila wiki
- Tafuta namna ya kusherehekea yale uliyoyafanikisha katika wiki husika. Unadhani hustahili? Kama ni ‘HAPANA’ anza tena na hatua ya kwanza hapo juu hadi ufikie hatua ya sita. Lakini kama unastahili, tafadhali jifanye kitu cha kujipongeza.
Kumbuka safari ya kujijengea kujiamini inaanzia na ushindi upatikanao katika kila wiki. Jifunze kujipongeza.
Maoni
Chapisha Maoni