Wengi wetu huyatazama mafanikio kana kwamba ni kitu kisichowezekana kukifikia. Tunajifananisha na watu ambao jamii inawatambua ya kuwa wamefanikiwa na kamwe tunashindwa kujipima kujua kipi tufanye kuwafikia. Tunaishia kudhamiria vitu vichache kuliko uwezo tulio nao ambao wengi hawajui kwamba wana huo uwezo ambao kimsingi ni mkubwa mno kiliko tujuavyo. Lakini ukweli ni kwamba mafanikio ni rahisi sana. Na si uchawi.
Ili kuweza kufanikiwa katika maisha, unahitaji vitu vikuu viwili: kufanya kitu unachokipenda bila kujali unapata hela au hupati bali furaha yako ni kuendelea kufanya na ajabu itakayo fuata ni pesa kuanza kukufuata na jambo la pili ni unyenyekevu (Kuwa tayari kumwona mtu yeyote ni bora kuliko wewe). Sasa hebu tuongelee maeneo haya mawili ya kihisia.
Jinsi gani ufanikiwe katika maisha: Fanya unachopenda
Yawezekana kabisa unajishughulisha na kitu ambacho hukipendi ila unajilazimisha kufanya. Sijui umeajiriwa, au una fanya biashara ambayo huipendi ila unajisemea moyoni nikiacha nitakula nini. Hilo ni tatizo kubwa. Kuna uhusiano mkubwa kati ya kupenda ufanyacho na mafanikio. Vitu hivi viwili ni vigumu kutenganisha. Na unapojishughulisha na kitu usichokipenda na kukifurahia ukweli ni kwamba hutofika popote.
Unapofanya jambo ulipendalo na kulifurahia, unakuwa na msukumo mkubwa uliojaa hamasa. Kifupi unajiendesha kutokana na kusudio lako la kuwepo hapa duniani. Lengo lako la wewe kuwepo duniani huwa ni kubwa kuliko wewe na ukilikosa hilo kusudio lako la kuwepo hapa duniani utashindwa kabisa kuwahudumia wengine.
Jinsi Gani Ufanikiwe Katika Maisha: Kuwa Mnyenyekevu
Kufanya jambo ulipendalo pasipokuwa mnyenyekevu ni hatari – Katika hali ya kufurahia ufanyacho, mtu aweza kabisa kuanzia akilini kujipa haki ya kufanya vitu ambavyo viko mbali sana na utu na hapo utakuwa hulitumikii kusudi lako halisi la kuwepo hapa duniani. Unyenyekevu maana yake ni kukubali uwe chombo chenye kukupa nguvu kiroho, na kubaki ukiweka akili, nguvu macho vyote vikielekea kwenye kusudio lako la maisha.
Unyenyekevu ni kujihudhurisha kikamilifu (Kwa kadri uwezavyo). Kwa lugha ya KIYAHUDI unyenyekevu ni kujipa nafasi ya ziro unapojilinganisha na wengine. Naomba nieleweke vizuri hapa, kuwa ziro haimaanishi ujichukie. Kinachoongelewa hapa ni ile hali ya umimi/kujisikia matawi ya juu (EGO) kutokana na mafanikio yako ndiyo inayoongelewa ya kwamba ikubali kuchukua siti ya nyuma na kuwa tayari sasa kupokea nguvu kutoka juu.
Kwa kumalizia kufanya upendacho siku zote utakuwa ukisukumwa kusonga mbele na wakati unyenyekevu utakufanya ulitumikie kusudio lako katika maisha. Hivyo umeweza kuona kwa nini funguo hizi mbili zilivyo muhimu kuelekea mafanio.
Natamani Dr. Kimambo, ambaye yumo katika hili kundi kama angeweza kuliongelea suala hili (Purpose Driven Life). Najua ametingwa na majukumu lakini ni maombi yangu siku moja aweze kuliongelea. Ni jambo la muhimu sana wana karakana ya ubongo kulielewa.
Nategemea maswali mengi ili tupate uelewa kamili na kuanza kuishi inavyotakiwa.
Ili kuweza kufanikiwa katika maisha, unahitaji vitu vikuu viwili: kufanya kitu unachokipenda bila kujali unapata hela au hupati bali furaha yako ni kuendelea kufanya na ajabu itakayo fuata ni pesa kuanza kukufuata na jambo la pili ni unyenyekevu (Kuwa tayari kumwona mtu yeyote ni bora kuliko wewe). Sasa hebu tuongelee maeneo haya mawili ya kihisia.
Jinsi gani ufanikiwe katika maisha: Fanya unachopenda
Yawezekana kabisa unajishughulisha na kitu ambacho hukipendi ila unajilazimisha kufanya. Sijui umeajiriwa, au una fanya biashara ambayo huipendi ila unajisemea moyoni nikiacha nitakula nini. Hilo ni tatizo kubwa. Kuna uhusiano mkubwa kati ya kupenda ufanyacho na mafanikio. Vitu hivi viwili ni vigumu kutenganisha. Na unapojishughulisha na kitu usichokipenda na kukifurahia ukweli ni kwamba hutofika popote.
Unapofanya jambo ulipendalo na kulifurahia, unakuwa na msukumo mkubwa uliojaa hamasa. Kifupi unajiendesha kutokana na kusudio lako la kuwepo hapa duniani. Lengo lako la wewe kuwepo duniani huwa ni kubwa kuliko wewe na ukilikosa hilo kusudio lako la kuwepo hapa duniani utashindwa kabisa kuwahudumia wengine.
Jinsi Gani Ufanikiwe Katika Maisha: Kuwa Mnyenyekevu
Kufanya jambo ulipendalo pasipokuwa mnyenyekevu ni hatari – Katika hali ya kufurahia ufanyacho, mtu aweza kabisa kuanzia akilini kujipa haki ya kufanya vitu ambavyo viko mbali sana na utu na hapo utakuwa hulitumikii kusudi lako halisi la kuwepo hapa duniani. Unyenyekevu maana yake ni kukubali uwe chombo chenye kukupa nguvu kiroho, na kubaki ukiweka akili, nguvu macho vyote vikielekea kwenye kusudio lako la maisha.
Unyenyekevu ni kujihudhurisha kikamilifu (Kwa kadri uwezavyo). Kwa lugha ya KIYAHUDI unyenyekevu ni kujipa nafasi ya ziro unapojilinganisha na wengine. Naomba nieleweke vizuri hapa, kuwa ziro haimaanishi ujichukie. Kinachoongelewa hapa ni ile hali ya umimi/kujisikia matawi ya juu (EGO) kutokana na mafanikio yako ndiyo inayoongelewa ya kwamba ikubali kuchukua siti ya nyuma na kuwa tayari sasa kupokea nguvu kutoka juu.
Kwa kumalizia kufanya upendacho siku zote utakuwa ukisukumwa kusonga mbele na wakati unyenyekevu utakufanya ulitumikie kusudio lako katika maisha. Hivyo umeweza kuona kwa nini funguo hizi mbili zilivyo muhimu kuelekea mafanio.
Natamani Dr. Kimambo, ambaye yumo katika hili kundi kama angeweza kuliongelea suala hili (Purpose Driven Life). Najua ametingwa na majukumu lakini ni maombi yangu siku moja aweze kuliongelea. Ni jambo la muhimu sana wana karakana ya ubongo kulielewa.
Nategemea maswali mengi ili tupate uelewa kamili na kuanza kuishi inavyotakiwa.
Maoni
Chapisha Maoni