Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Muda na Pesa

  1. MTU ANAYECHEZEA MUDA = MTU ANACHEZEA PESA

  1. MTU ANAYECHEZEA PESA = MTU ANACHEZEA HATIMA YAKE KAA MBALI NA MTU HUYU NI SUMU KULIKO KANSA.

Jambo la kwanza nitaongelea kuhusiana na utafiti uliofanyika na kuonesha ya kuwa angalau kila familia kuna mtu mmoja ambaye akikujia na kukusomesha lazima utatoa pesa, sijui niwaite matapeli bado nazidi kutafuta lugha nzuri nataabika lakini nisaidie kuwapatia jina sahihi.

Ninachojaribu kuelezea hapa ni kwamba kuna watu hapa duniani ni wabunifu wa kutunga stori ili kujipatia pesa. Watu wa jinsi hii usiombe kukutana nao maana ukimpa tu nafasi akajieleza lazima utatoa pesa.

Inawezekana kabisa ukajisemea ya kwamba fulani akija kwangu simpi hata senti tano. Kinachoshangaza kwa ubunifu maridhawa walionao utajikuta si tu nunampatia pesa bali pia unamsaidia kumtafutia na kwa wengine wamuongezee.

Sijui kama ninachongea umekutana nacho  maishani au unawafahamu watu wa jinsi hiyo katika jamii zetu kama sio kwenye familia zetu.

Yawezekana kabisa wengine wamo katika kundi hili. Kama umo humu ndani basi mshukuru sana Mungu maana siku ya ukombozi imewadia.

Imegundulika pasi shaka ya aina yoyote ya kuwa watu wote walio wabunifu kutunga stori za kujipatia pesa wamekosa mtu wa kuwasaidia kutwisti ubunifu huo kuelekeza kwenye ubunifu wa kujitengenezea pesa kama njugu.

Ukweli ni kwamba watu wa jinsi hii wana uwezo mzuri sana wa kubuni kitu kikatokea isipokuwa sasa wameelekeza ubunifu wao kwenye sehemu hasi. Ubunifu huo huo ukielekezwa kwenye kutengeneza pesa, kubuni miradi na kadhalika watatajirika sana.

Jambo la pili – Matajiri wote wanapigania wasipoteze muda, wakati masikini wote msimamo wao ni kupigania pesa isipotee.


Ndio maana mtu yuko radhi akae sehemu chafu yenye mainzi aweze  kula chakula cha bei rahisi yaani mfano sahani sh. 500. Hapa anahurumia pesa yake isipotee maana ndicho kilichojengeka kwenye ubongo hata kama uwezo wa kula sahani ya 1,500 anao.

Mtu wa jinsi hii hata akiwa na mafanikio ni ngumu sana kubadilika kwa sababu ya Imani iliyojengeka kwa muda mrefu jinsi ya kuichukulia pesa tangu akiwa mdogo, akitumwa anaambia angalia kitu cha bei  rahisi. Mpaka mtu anazeeka anajikuta amejengeka kiimani ya kwamba ni vyema kuihurumia pesa. Badala ya kutumia pesa kutokana jinsi ilivyo.

Pesa kimsingi ni mtumishi. Ndio maana haitanichukua muda kutoa uamuzi pale jirani anapokuwa na mgonjwa na hana pesa ya taxi. Nitawapatia mtumishi wangu pesa awasaidie maana hiyo ndio kazi yake na pia kitendo hicho kinanihakikishia mimi kuendelea kuwa na pesa Zaidi. Maana kutoa ni bora kuliko kupokea.
Naomba nikupe mfano ili kulielewa hili. Tajiri anaona ni rahisi kwenda Mwanza kwa kutumia ndege maana ataokoa muda mwingi sana maana haitachukua masaa mawili kufika Mwanza na kuweza kuendelea na shughuli zake. Hapo amepigania muda wake usipotee maana anahitaji muda zaidi kuliko pesa. Hivyo akilini mwake siku zote ni kuokoa muda si pesa, Na kama matokeo anaishia kuokoa muda na kutengeneza pesa Zaidi.
Natamani hili ulijue ikibidi hata kwa kukuchapa viboko maana kuna siri kubwa sana hapa.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Akili Hisia (emotional intelligence).

Lea mtizamo wa kisayansi, akili hisia ni ule uwezo wa mtu kuweza kutawala anachokiona kwenye mazingira aliyomo. Hii inaamanisha kwamba aweze kutawala mazingira kwa kutumia akili ya hisia zake na wale waliomzunguka. Mtu atawezaje kuelewa kwa kutumia hisia, ishara zinazoonekana kwenye mahusiano mbalimbali bila kuambiwa sentensi au hata neno moja? Utawezaje kutawala hisia zako na za watu wengine katika mazingira uliyomo? Kuna hatua sita za kuchukua ili akili hisia zako zikupe mafanikio unayoyatafuta. #1. Hatua ya kwanza ni wewe mwenyewe kujitambua. Kujitambua ni kitu muhimu kabisa linapokuja suala la akili hisia au emotional intelligence (EQ). Hebu tujiulize ni kwanini? Bila akili hisia hatuna namna yeyote ya kujitathmini kwa vile vipaji ama tulivyo navyo, tusivyo navyo au tunavyohitaji kujifunza ili tuweze kufanikiwa katika mambo yetu mbalimbali. Utaishia kuwa kama kipofu, maana hutaona chochote katika mazingira yaliyokuzunguka. Utapata shida kubwa kutumia mikono isiyoonekana. Aki...

Timiza Malengo Yako na Joel Nanauka.

Ninamshukuru Mungu sana kuweza kuwa na waandishi mashuhuri wa kitanzania ambao wanaweza andika vitabu kwa lugha ya Kiswahili na kusaidia watanzania wengi zaidi. Kitabu cha Timiza Malengo ni kitabu cha aina yake na kamwe si cha kukosekana kwenye maktaba yako. Kama kuna kitu familia yako inabidi ikushukuru basi ni hichi kitabu. Mimi ni msomaji sana wa vitabu na niseme tu ukweli kitabu hichi ni hazina tosha na hakikisha unapata nakala yako. Wahenga walisema tusiandikie wino wakati mate yapo. Nilichokifanya ni kukupatia sehemu ya hichi kitabu kutoka ukurasa wa 29 hadi 40 neno kwa neon ujisomee na useme mwenyewe je uko tayari kukikosa hichi kitabu? Tafadhali fuatana name nikinukuu kitabu cha Joel Nanauka kwa idhini yake kama ifuatavyo:- NJIA MBILI ZA KUTAMBUA KUSUDI LA MAISHA YAKO: Siku moja wakati Tiger Woods anahojiwa na mtangazaji akamwabia ‘’It seems like you like golf so much’’ (Inaonekana kuwa unaipenda gofu sana).Tiger Woods akamjibu, ‘’Not only I like golf but I am golf,’’ a...

CONSCIOUS NA SUB-CONCIOUS MIND

Wazo La Leo Hongera sana mwanakarakana ya ubongo kwa siku hii nyingine nzuri sana ya leo. Ni nafasi bora na ya kipekee sana kwetu kwenda kuweka juhudi kubwa ili kuweza kupata matokeo bora sana. Leo nimeona vyema nizungumzie maana ya maneno ambayo tumekuwa tukiyasikia mara kwa mara. Conscious na Subconscious. Kwanza unatakiwa uelewe "sub" maana yake nn, hii ni prefix...ikiwa na maana ya "below" something, sio negative or opposite that something. Kwa hiyo maana ya "conscious mind" ni kujitambua na subconscious mind means: internal sense of being ambayo consious mind haiwezi decipher, i mean kukupa maono halisi, wakristo wanaita nafsi, mfano mzuri wa activities za subconscious mind ni ndoto Conscious mind-ni kutumia akili wakati tendo fulani linafanyika. Hii inatokea pale mtu anapokuwa hana uzoefu wakati anafanya jambo/tendo fulani, kutokana na kutokuwa na uzoefu inabidi atumie uzingativu wakati wa kutekeleza jambo/tendo husika. kwa mfano mtu anayej...