Naomba kabla sijaanza kuandika chochote nimshukuru sana Mchungaji Timoth Kyara ambaye ni rafiki na kocha wangu kwa jinsi alivyonifundisha na anaendelea kunifundisha juu ya pesa. Na mengi nitakayokushirikisha hapa ni yale nilijifunza kwake na baada ya kuona ni elimu murua ya kuweza kushirikisha wana karakana ya ubongo nikaamua kufanya hivyo. Karibu tuendelee.
Kuna msemo wa kiingereza usemao ‘A fool and his money are soon parted’ pia ‘man is born free, but everywhere he is in chain’ by Jean Jacques Rousseau, French Political Philosopher (1972 – 1978).
Kwa nini iko hivyo? Hivi umewahi kujiuliza inakuwaje baadhi ya watu kwao kupata pesa ni kitu raisi sana lakini kwa wengine ni kinyume kwani hujituma sana na kuishia kupata kiduchu ambapo huingiza kwenye mifuko iliyotoboka, kwa kawaida pesa za watu wa jinsi hii zimeungamanishwa na mabomba ambayo kimsingi pesa ikiingia tu mfukoni husafirishwa mara moja kwenda kusikojulikana na kumuacha mtu akiwa kapuku.
Kama kuna kitu nataka ujifunze leo basi ni ukweli kwamba ‘Hakuna kitu hutokea kwa sababu ya kutokea’. Kuna sababu kwa kila jambo. Kama ilivyo kanuni ya mvutano (Gravitational Force) – Ukirusha chochote juu ni lazima kishuke chini tena kwa spidi ya 9.81m/s2 au kama lilivyo jua huchomoza kutokea mashariki na huzamia magharibi ndivyo hivyo ilivyo kwa pesa kwa kila maisha mwanadamu hutawaliwa na kanuni za dunia. Jifunze juu ya pesa/Sheria za pesa na zitumie zikufaidishe.
Kwanini mahusiano yako na pesa yamefarakana?
Jaribu kurudi nyuma miaka 10, 5, au hata 2; Hebu chunguza marafiki zako wote wa karibu nawe ambao kwa sasa wameachana nawe na wengine wewe uliamua kuachana nao. Kuna kitu kilitokea katika mahusiano yenu kilichosababisha kutokuwa tena marafiki. Kitu cha kusikitisha, mahusiano mengi ambayo yamevunjika na mengine yako njiani kuvunjika ni kutokana na mapungufu ya kutopalilia mahusiano (waulize wenye mahusiano yaliyovunjika ya boy fiend na girl friend vilevile wana ndoa utaelewa kwa undani umuhimu wa kupalilia au kuweka mazingira yenye rutuba kimahusiano).
Sababu zingine ni pamoja na kutengwa, kupishana mitizamo/misimamo, kudharauliana na mengine mengi.
Pesa twaweza ifananisha na kiumbe hai chenye uwezo wa kuhusiana na kiumbe kingine hai. Kuna mahusiano makubwa kati yako na pesa ambazo kimsingi unabaki kuwa mwenye kuzihozi, kwa hiyo pesa iwapo mikononi mwako una mamlaka nayo ya kufanya chochote upendacho. Kuna mithali ya kiingereza inasema ‘a fool and his money are soon parted’ says it all. Wakati pesa yako inapo kazana kukukimbia, ni wakati mzuri wa kufikiri; Labda umemkatisha tamaa na hivyo kumfanya ajongee.
Moja ya njia ya kuvunja uhusiano ni kumdhalilisha mwenzako kila wakati ambapo chaguo pekee linabaki kujongea kutengana kabisa kimahusiano. Hivyo, unapowaza juu ya pesa kila mara inakukimbia yawezekana umekuwa ukiidhalilisha na ndio maana imeona njia pekee ni kukukimbia.
Sasa kama utapenda, ngoja nichambue namna tunavyodhalilisha pesa hata zishindwe kutulia na kuamua kutukimbia.
Udhalalishwaji wa mahusiano na pesa
Neno kudhalilisha kifupi linamaanisha matumizi yasiyo ya kawaida, yaani ‘matumizi ambayo siyo yaliyokusudiwa’. Kwa maneno mengine ili kuelezea vizuri ni sawia na kusema kutumika vibaya, kushindwa kushikilia, matumizi mabovu na kadhalika. Ni rahisi sana kudhalilisha mahusiano na pesa na yaweza kuwa na madhala yenye sura tofauti.
Wakati nikitambua kwa hakika ya kuwa kuna namna mbalimbali ambazo zinaashilia namna tunavyodhalilisha pesa tunapojaribu kuhusiana, hivyo kwa lengo la somo hili la leo, nimechagua mambo matatu ambayo yanabeba mizania ya juu kabisa:
Pesa huwa bwana mkubwa kwako pale inapotokea ‘Waweza fanya chochote’ ilikuhakikisha unazishika (kutumika/kuokoa) kwa kufikia hatua hii tamaa inakuwa imechua nafasi. Tamaa kimsingi ni hali ya kutaka Zaidi yaani kutotosheka…kwa kawaida hali hii ugubikwa na hofu ya kujiona una upungufu.
Hebu jipendelee na chunguza, kisha chagua bank ya chaguo lako na kisha endelea na uchunguzi uone faida watakayokupa kwa kuwekeza pesa kwao bila kufanya kazi huku ikiendelea kupungua thamani. Kama ikitokea umeweka pesa kwenye account isiyo ya akiba kiasi cha Tshs. 10,000 katika benki uliyoichagua wewe mwenyewe, pasi shaka kila mwezi watakukata gharama za kukutunzia pesa. Sasa chambua kupungua kwa thamani na gharama za bank wakatazo kukata kwenye pesa yako; utagundua ya kwamba mwisho wa mwaka utachukua kiwango pungufu kwa thamani na pia kwa kiwango.
Pesa katika sura yake ya sarafu au noti au fedha kwa sura ya kuwa mtumishi kamwe haitakiwi kukusanywa na kuhifadhiwa, Na kama utafanya hivyo, basi hapo utakuwa unadhalilisha mahusiano yako na pesa na muda si mrefu utajikuta umekaa kwenye kundi la kupoteza pesa.
‘Kununua vitu usivyovihitaji (vitu vya anasa) pasipo pesa bali kupita kukopa ili tu kuwaridhisha watu ambao yu mkini hata hawavitaki (marafiki, ndugu, majirani)’ Ufanyapo hili, kumuka litakuchelewesha kufikia uhuru wa kifedha siku za usoni.
Pesa ni nyenzo, mtumwa na silaha yenye nguvu; jifunze kuitumia vyema – si kwa ufujaji au kutokuwa makini – iachilie (spend wisely). Busara ni pale unapojua wapi na kwa jinsi gani ya kutumia pesa iweze kukutumikia kwa ubora wa hali ya juu.
Kesho tutaendea na somo hili la pesa.
Kuna msemo wa kiingereza usemao ‘A fool and his money are soon parted’ pia ‘man is born free, but everywhere he is in chain’ by Jean Jacques Rousseau, French Political Philosopher (1972 – 1978).
Kwa nini iko hivyo? Hivi umewahi kujiuliza inakuwaje baadhi ya watu kwao kupata pesa ni kitu raisi sana lakini kwa wengine ni kinyume kwani hujituma sana na kuishia kupata kiduchu ambapo huingiza kwenye mifuko iliyotoboka, kwa kawaida pesa za watu wa jinsi hii zimeungamanishwa na mabomba ambayo kimsingi pesa ikiingia tu mfukoni husafirishwa mara moja kwenda kusikojulikana na kumuacha mtu akiwa kapuku.
Kama kuna kitu nataka ujifunze leo basi ni ukweli kwamba ‘Hakuna kitu hutokea kwa sababu ya kutokea’. Kuna sababu kwa kila jambo. Kama ilivyo kanuni ya mvutano (Gravitational Force) – Ukirusha chochote juu ni lazima kishuke chini tena kwa spidi ya 9.81m/s2 au kama lilivyo jua huchomoza kutokea mashariki na huzamia magharibi ndivyo hivyo ilivyo kwa pesa kwa kila maisha mwanadamu hutawaliwa na kanuni za dunia. Jifunze juu ya pesa/Sheria za pesa na zitumie zikufaidishe.
Kwanini mahusiano yako na pesa yamefarakana?
Jaribu kurudi nyuma miaka 10, 5, au hata 2; Hebu chunguza marafiki zako wote wa karibu nawe ambao kwa sasa wameachana nawe na wengine wewe uliamua kuachana nao. Kuna kitu kilitokea katika mahusiano yenu kilichosababisha kutokuwa tena marafiki. Kitu cha kusikitisha, mahusiano mengi ambayo yamevunjika na mengine yako njiani kuvunjika ni kutokana na mapungufu ya kutopalilia mahusiano (waulize wenye mahusiano yaliyovunjika ya boy fiend na girl friend vilevile wana ndoa utaelewa kwa undani umuhimu wa kupalilia au kuweka mazingira yenye rutuba kimahusiano).
Sababu zingine ni pamoja na kutengwa, kupishana mitizamo/misimamo, kudharauliana na mengine mengi.
Pesa twaweza ifananisha na kiumbe hai chenye uwezo wa kuhusiana na kiumbe kingine hai. Kuna mahusiano makubwa kati yako na pesa ambazo kimsingi unabaki kuwa mwenye kuzihozi, kwa hiyo pesa iwapo mikononi mwako una mamlaka nayo ya kufanya chochote upendacho. Kuna mithali ya kiingereza inasema ‘a fool and his money are soon parted’ says it all. Wakati pesa yako inapo kazana kukukimbia, ni wakati mzuri wa kufikiri; Labda umemkatisha tamaa na hivyo kumfanya ajongee.
Moja ya njia ya kuvunja uhusiano ni kumdhalilisha mwenzako kila wakati ambapo chaguo pekee linabaki kujongea kutengana kabisa kimahusiano. Hivyo, unapowaza juu ya pesa kila mara inakukimbia yawezekana umekuwa ukiidhalilisha na ndio maana imeona njia pekee ni kukukimbia.
Sasa kama utapenda, ngoja nichambue namna tunavyodhalilisha pesa hata zishindwe kutulia na kuamua kutukimbia.
Udhalalishwaji wa mahusiano na pesa
Neno kudhalilisha kifupi linamaanisha matumizi yasiyo ya kawaida, yaani ‘matumizi ambayo siyo yaliyokusudiwa’. Kwa maneno mengine ili kuelezea vizuri ni sawia na kusema kutumika vibaya, kushindwa kushikilia, matumizi mabovu na kadhalika. Ni rahisi sana kudhalilisha mahusiano na pesa na yaweza kuwa na madhala yenye sura tofauti.
Wakati nikitambua kwa hakika ya kuwa kuna namna mbalimbali ambazo zinaashilia namna tunavyodhalilisha pesa tunapojaribu kuhusiana, hivyo kwa lengo la somo hili la leo, nimechagua mambo matatu ambayo yanabeba mizania ya juu kabisa:
- Kubadili Matumizi – ‘Pesa kwa namna mbalimbali yafananishwa na moto, ni mtumishi mzuri kwa upande mmoja lakini ni bwana mwenye kutisha kwa upande mwingine’. P.T.Barnum mwanafalsafa mashuhuri anasema ‘penda watu, tumia pesa kuwaokoa na kuwahudumia’. Katika mahusiano ya kudhalilisha, mtu anapenda pesa na huwatumia watu kuzipata (kuokoa na kutumikia) pesa. Katika mazingira ya jinsi hii, pesa hukoma kuwa mtumishi, na hugeuka kuwa bwana, bwana mwenye kutisha.
Pesa huwa bwana mkubwa kwako pale inapotokea ‘Waweza fanya chochote’ ilikuhakikisha unazishika (kutumika/kuokoa) kwa kufikia hatua hii tamaa inakuwa imechua nafasi. Tamaa kimsingi ni hali ya kutaka Zaidi yaani kutotosheka…kwa kawaida hali hii ugubikwa na hofu ya kujiona una upungufu.
- Kukusanya na Kuhifadhi – Pesa ni sarafu/noti lakini pia ni mtumishi; sarafu/noti, inatakiwa izunguke (ikibadilisha mikono kwa kupitia huduma na bidhaa) na pia kama mtumishi, pesa yatakiwa itumikishwe. Nani miongoni mwetu angefurahia mfanyakazi wake wa ndani awe anakaa tu siku nzima huku ukiwa umemwajiri achape kazi? Vivyo hivyo bwawa lisilo na maji au mkondo wa maji litaishia kunuka na kuua viumbe vyote hai vilivyokuwa vimewekwa humo.
Hebu jipendelee na chunguza, kisha chagua bank ya chaguo lako na kisha endelea na uchunguzi uone faida watakayokupa kwa kuwekeza pesa kwao bila kufanya kazi huku ikiendelea kupungua thamani. Kama ikitokea umeweka pesa kwenye account isiyo ya akiba kiasi cha Tshs. 10,000 katika benki uliyoichagua wewe mwenyewe, pasi shaka kila mwezi watakukata gharama za kukutunzia pesa. Sasa chambua kupungua kwa thamani na gharama za bank wakatazo kukata kwenye pesa yako; utagundua ya kwamba mwisho wa mwaka utachukua kiwango pungufu kwa thamani na pia kwa kiwango.
Pesa katika sura yake ya sarafu au noti au fedha kwa sura ya kuwa mtumishi kamwe haitakiwi kukusanywa na kuhifadhiwa, Na kama utafanya hivyo, basi hapo utakuwa unadhalilisha mahusiano yako na pesa na muda si mrefu utajikuta umekaa kwenye kundi la kupoteza pesa.
- Ufujaji Pesa
‘Kununua vitu usivyovihitaji (vitu vya anasa) pasipo pesa bali kupita kukopa ili tu kuwaridhisha watu ambao yu mkini hata hawavitaki (marafiki, ndugu, majirani)’ Ufanyapo hili, kumuka litakuchelewesha kufikia uhuru wa kifedha siku za usoni.
Pesa ni nyenzo, mtumwa na silaha yenye nguvu; jifunze kuitumia vyema – si kwa ufujaji au kutokuwa makini – iachilie (spend wisely). Busara ni pale unapojua wapi na kwa jinsi gani ya kutumia pesa iweze kukutumikia kwa ubora wa hali ya juu.
Kesho tutaendea na somo hili la pesa.
Maoni
Chapisha Maoni