Leo nimeonelea vyema tukumbushane ya kuwa hatupo hapa duniani milele. Sote tu wapitaji na sijui kama umewahi kujiuliza hili swali ya kwamba siku moja utatoweka.
Ukilijua hili vizuri hutakuwa na muda wa kupoteza maana kifo hakina taarifa wala kanuni. Hivyo kila siku akupayo Mungu hakikisha unajipangia kufanya vitu kana kwamba kesho hutakuwepo.
Hili litakufanya uwaguse watu wengi Zaidi katika uwepo wako duniani. Utalazimika kuishi maisha yenye maana na kuwa mwangalifu kwa mengi ili uache alama utakapokuwa haupo.
Napenda msemo anaoutumia Joel Nanauka ya kwamba ulikuja duniani binafsi lakini yakupasa kuondoka ukiwa taasisi akimaanisha taasisi si ya mtu mmoja bali ya wengi. Hivyo kuondoka kwako kuache mazungumzo kwa wengi kwa jinsi ulivoyagusa maisha yao na hapo ndipo unakuwa taasisi na sio tena mtu binafsi.
Maisha ni mafupi. Ishi kila siku kwa utimilifu wake (Live full today). Kuwa bora kuliko katika kila jambo ulifanyalo.
Kujua utakufa itakujengea kukumbushwa utakapoondoka watakuongeleaje. Yakupasa kuacha kumbukumbu chanya duniani ya jinsi gani uliwafanya watu wajisikie kwa uwepo wako na jinsi gani binafsi ulijisikia.
Ndio tutaondoka lakini maisha yetu hayana budi kuendelea kuishi. Kuwa mwangalifu wa jinsi unavyoishi.
Hivyo ili kuokoa muda – unahitaji nini? Au unatamani nini? Hicho unachotamani tayari watu wanacho. Inaashiria ya kwamba si muujiza na wewe inawezekana kuwa nacho. Jifunze kupitia kwao na vitabu hata mafunzo mbalimbali yenye kukupelekea kupata kile unachohitaji. Maisha ni mafupi hebu harakisha uache alama.
Na siku zote ukijua unapita tu hapa duniani basi hakikisha hupotezi muda kwa kujishughulisha na kitu kisichokupa furaha moyoni. Ishi maisha yenye maana acha kupoteza muda.
Pia kuwa wewe. Acha kuiga. Jisikilize. Kikubwa uache taswira halisi ya kwako. Kamwe usishindane na mtu. Mashindano halisi ni wewe mwenyewe kwa kuhakikisha kila siku unakuwa bora kuliko jana. Na huo ndio ushindi. Maisha ni mafupi. Kaza mkono katika kazi.
Kuwa tayari kuumia na kujitoa kwa vitu vikufanyavyo kuwa na furaha ukivifanya na kama sivyo achana navyo. Maisha ni mafupi.
Namna pekee ya wewe kufanikiwa ni kuwa na furaha. Acha kuishi maisha ya kuigiza kwa kuwafariji watu kinafiki wakati ndani kabisa ya moyo wako sivyo ulivyo. Maisha ni mafupi.
Kumbuka chochote utakacho kipo ndani yako. Nakumbuka siku moja TD Jakes alisema ‘Walikwenda Kenya siku moja na kukuta watu katika kijiji fulani wanataabika juu ya upatikanaji wa maji. Wengi walipoteza maisha na wengine kuugua sana na kila mtu alilalamika sana. Kilichofanyika kwa haraka ilikuwa kuanza mara moja kupima wapi maji yatapatikana. Cha ajabu palepale walipokuwa wanaishi palikuwa na mwamba wenye maji mengi haijapata tokea. Hivyo utaratibu ukafanyika na watu walishangazwa ya kuwa walikalia maji huku wakifa pasi kujuaâ.
Nini mantiki ya habari hiyo na ujinga waweza kukuangamiza kabisa. Weka juhudi kujitafuta kujua nini kilichomo ndani yako. Hiyo ndio shughuli kuu na huna budi kuifanya kwa kasi. Usije juta na ku…
Ukilijua hili vizuri hutakuwa na muda wa kupoteza maana kifo hakina taarifa wala kanuni. Hivyo kila siku akupayo Mungu hakikisha unajipangia kufanya vitu kana kwamba kesho hutakuwepo.
Hili litakufanya uwaguse watu wengi Zaidi katika uwepo wako duniani. Utalazimika kuishi maisha yenye maana na kuwa mwangalifu kwa mengi ili uache alama utakapokuwa haupo.
Napenda msemo anaoutumia Joel Nanauka ya kwamba ulikuja duniani binafsi lakini yakupasa kuondoka ukiwa taasisi akimaanisha taasisi si ya mtu mmoja bali ya wengi. Hivyo kuondoka kwako kuache mazungumzo kwa wengi kwa jinsi ulivoyagusa maisha yao na hapo ndipo unakuwa taasisi na sio tena mtu binafsi.
Maisha ni mafupi. Ishi kila siku kwa utimilifu wake (Live full today). Kuwa bora kuliko katika kila jambo ulifanyalo.
Kujua utakufa itakujengea kukumbushwa utakapoondoka watakuongeleaje. Yakupasa kuacha kumbukumbu chanya duniani ya jinsi gani uliwafanya watu wajisikie kwa uwepo wako na jinsi gani binafsi ulijisikia.
Ndio tutaondoka lakini maisha yetu hayana budi kuendelea kuishi. Kuwa mwangalifu wa jinsi unavyoishi.
Hivyo ili kuokoa muda – unahitaji nini? Au unatamani nini? Hicho unachotamani tayari watu wanacho. Inaashiria ya kwamba si muujiza na wewe inawezekana kuwa nacho. Jifunze kupitia kwao na vitabu hata mafunzo mbalimbali yenye kukupelekea kupata kile unachohitaji. Maisha ni mafupi hebu harakisha uache alama.
Na siku zote ukijua unapita tu hapa duniani basi hakikisha hupotezi muda kwa kujishughulisha na kitu kisichokupa furaha moyoni. Ishi maisha yenye maana acha kupoteza muda.
Pia kuwa wewe. Acha kuiga. Jisikilize. Kikubwa uache taswira halisi ya kwako. Kamwe usishindane na mtu. Mashindano halisi ni wewe mwenyewe kwa kuhakikisha kila siku unakuwa bora kuliko jana. Na huo ndio ushindi. Maisha ni mafupi. Kaza mkono katika kazi.
Kuwa tayari kuumia na kujitoa kwa vitu vikufanyavyo kuwa na furaha ukivifanya na kama sivyo achana navyo. Maisha ni mafupi.
Namna pekee ya wewe kufanikiwa ni kuwa na furaha. Acha kuishi maisha ya kuigiza kwa kuwafariji watu kinafiki wakati ndani kabisa ya moyo wako sivyo ulivyo. Maisha ni mafupi.
Kumbuka chochote utakacho kipo ndani yako. Nakumbuka siku moja TD Jakes alisema ‘Walikwenda Kenya siku moja na kukuta watu katika kijiji fulani wanataabika juu ya upatikanaji wa maji. Wengi walipoteza maisha na wengine kuugua sana na kila mtu alilalamika sana. Kilichofanyika kwa haraka ilikuwa kuanza mara moja kupima wapi maji yatapatikana. Cha ajabu palepale walipokuwa wanaishi palikuwa na mwamba wenye maji mengi haijapata tokea. Hivyo utaratibu ukafanyika na watu walishangazwa ya kuwa walikalia maji huku wakifa pasi kujuaâ.
Nini mantiki ya habari hiyo na ujinga waweza kukuangamiza kabisa. Weka juhudi kujitafuta kujua nini kilichomo ndani yako. Hiyo ndio shughuli kuu na huna budi kuifanya kwa kasi. Usije juta na ku…
Maoni
Chapisha Maoni