Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Ukweli kuhusu maisha

Maisha ni neno moja lakini lenye mana nyingi unapoamua kumyambulisha maana yake. Kufikia malengo utakayo kuyafikia nayo ni maisha na hili ni eneo nitakaloliongelea kwa kina siku ya leo.
Kutamani uwe vile na hivi ni rahisi sana lakini kuchukua hatua ya kutenda ndilo eneo ambalo wengi hushindwa na kuishia kuona maisha hayana maana yoyote. Wanadamu wanatakiwa kujua ya kwamba kutenda ni muujiza unaojiridhisha kwa watu wenye uthubutu na hili linatuthibitishia kusahau kabisa kutamani kuwa kama fulani bila kuchukua hatua ya utendaji.
Kwa kawaida huwa nawashauri watu ya kuwa chochote unachotamani kuwa nacho, tayari wengine wanacho. Kwa hiyo njia rahisi ni kukutana na hao ambao tayari wanavyo ili upate kujua yakupasa kunya nini ili nawe uweze kupata. Hii inamaanisha ya kuwa unakuwa tayari kupitia maumivu yatakayokufikisha unapotamani kufika, au ukaishia hatua ambayo hukuitamani kuifikia kwa kutofanya yale uliyoelekezwa kufanya. Yote kwa yote wewe ndiye mwamuzi.
Ni sawa na nadharia ihusishayo habu na rimu ya tairi ya gari – Je unapenda kuwa habu, au rimu? Ili uwe habu inamaanisha uwe mtu wa katikati Zaidi, na kuwa rimu ni kuwa mbali na utendaji au nguvu ya kuzuzungusha. Ninaposisitiza juu ya umuhimu wa nguvu iliyopo katika kuzamia kitu (kuweka macho, akili, nguvu kwenye kitu kimoja tu hata mtu akikuita inakuwa ngumu kumsikiliza kutokana na kuzama katika jambo moja), hii ni namna ya kulitazama suala zima la kuwa habu. Hivyo kung’ang’ana katikati kama habu ndicho kitu muhimu katka maisha yako, ndicho kitakachokutafautisha kati ya kuwa habu au rimu
Endelea kutafakari juu ya utendaji wa habu ili nawe katika maisha ujiweke kwenye nafasi ya habu na kitakachofuata ni maisha yako kuwa bora Zaidi.
Ni mimi mwalimu wako Seth Simon Mwakitalu 0754 441325/0714 051 174/0788 493 836 au barua pepe ssmwakitalu2013@gmail.com
Kwa wale wote wenye kuhitaji kujifunza Zaidi waweza wasiliana nami ili kujumuika na wengine ambao hupata kujifunza kwa pamoja kupitia kundi la watsApp lijulikanalo kwa jina la KARAKANA YA UBONGO.
Kujiunga na kundi hili ni lazima ufanyiwe udahili/interview ili kuona kama unafaa au la. Hatuhitaji utuletee virusi katika kundi. Nakutakia siku njema yenye mafanikio tele. Kwa heri.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Akili Hisia (emotional intelligence).

Lea mtizamo wa kisayansi, akili hisia ni ule uwezo wa mtu kuweza kutawala anachokiona kwenye mazingira aliyomo. Hii inaamanisha kwamba aweze kutawala mazingira kwa kutumia akili ya hisia zake na wale waliomzunguka. Mtu atawezaje kuelewa kwa kutumia hisia, ishara zinazoonekana kwenye mahusiano mbalimbali bila kuambiwa sentensi au hata neno moja? Utawezaje kutawala hisia zako na za watu wengine katika mazingira uliyomo? Kuna hatua sita za kuchukua ili akili hisia zako zikupe mafanikio unayoyatafuta. #1. Hatua ya kwanza ni wewe mwenyewe kujitambua. Kujitambua ni kitu muhimu kabisa linapokuja suala la akili hisia au emotional intelligence (EQ). Hebu tujiulize ni kwanini? Bila akili hisia hatuna namna yeyote ya kujitathmini kwa vile vipaji ama tulivyo navyo, tusivyo navyo au tunavyohitaji kujifunza ili tuweze kufanikiwa katika mambo yetu mbalimbali. Utaishia kuwa kama kipofu, maana hutaona chochote katika mazingira yaliyokuzunguka. Utapata shida kubwa kutumia mikono isiyoonekana. Aki...

Timiza Malengo Yako na Joel Nanauka.

Ninamshukuru Mungu sana kuweza kuwa na waandishi mashuhuri wa kitanzania ambao wanaweza andika vitabu kwa lugha ya Kiswahili na kusaidia watanzania wengi zaidi. Kitabu cha Timiza Malengo ni kitabu cha aina yake na kamwe si cha kukosekana kwenye maktaba yako. Kama kuna kitu familia yako inabidi ikushukuru basi ni hichi kitabu. Mimi ni msomaji sana wa vitabu na niseme tu ukweli kitabu hichi ni hazina tosha na hakikisha unapata nakala yako. Wahenga walisema tusiandikie wino wakati mate yapo. Nilichokifanya ni kukupatia sehemu ya hichi kitabu kutoka ukurasa wa 29 hadi 40 neno kwa neon ujisomee na useme mwenyewe je uko tayari kukikosa hichi kitabu? Tafadhali fuatana name nikinukuu kitabu cha Joel Nanauka kwa idhini yake kama ifuatavyo:- NJIA MBILI ZA KUTAMBUA KUSUDI LA MAISHA YAKO: Siku moja wakati Tiger Woods anahojiwa na mtangazaji akamwabia ‘’It seems like you like golf so much’’ (Inaonekana kuwa unaipenda gofu sana).Tiger Woods akamjibu, ‘’Not only I like golf but I am golf,’’ a...

CONSCIOUS NA SUB-CONCIOUS MIND

Wazo La Leo Hongera sana mwanakarakana ya ubongo kwa siku hii nyingine nzuri sana ya leo. Ni nafasi bora na ya kipekee sana kwetu kwenda kuweka juhudi kubwa ili kuweza kupata matokeo bora sana. Leo nimeona vyema nizungumzie maana ya maneno ambayo tumekuwa tukiyasikia mara kwa mara. Conscious na Subconscious. Kwanza unatakiwa uelewe "sub" maana yake nn, hii ni prefix...ikiwa na maana ya "below" something, sio negative or opposite that something. Kwa hiyo maana ya "conscious mind" ni kujitambua na subconscious mind means: internal sense of being ambayo consious mind haiwezi decipher, i mean kukupa maono halisi, wakristo wanaita nafsi, mfano mzuri wa activities za subconscious mind ni ndoto Conscious mind-ni kutumia akili wakati tendo fulani linafanyika. Hii inatokea pale mtu anapokuwa hana uzoefu wakati anafanya jambo/tendo fulani, kutokana na kutokuwa na uzoefu inabidi atumie uzingativu wakati wa kutekeleza jambo/tendo husika. kwa mfano mtu anayej...