Mara nyingi unapokuwa umepewa maelezo ya eneo ambalo toka uzaliwe hujawahi kufika hakika utahitaji kupata namna itakayokuwezesha kufika huko utakako kwenda.
Ashukuriwe Mungu kwa ubunifu aliompa mwanadamu katika suala la kusaidiana kufika maeneo ya ugenini kwani kuna vitu mbali mbali vimsaidiavyo mwanadamu kuweza kufika aendako.
Nakumbuka mimi binafsi kwa mara yangu ya kwanza kwenda Marekani. Haikuwa jambo rahisi.
Ninaye rafiki aishie Marekani na familia yake kwa muda sasa. Hivyo tuliandikiana na kunipatia namba zake za simu akiwa marekani na za mke wake na simu za nyumbani ili tu kutengeneza mazingira ya kupokelewa kirahisi na nisipate usumbufu nchi za watu na tena nchi yenyewe marekani.
Nilimpatia details za ticket ambazo zilionesha hadi muda wa kuwasili Dallas. Simaanishi daladala maana vijana hamishi kusema mzee kateleza, hayo ni majina ya nchi za wenzetu. Eneo hilo liko TEXAS nchini Marekani.
Nakumbuka aliniuliza swali moja unapokuja uwe unaniambia ndege unayokuja nayo maana kuna eneo najua utabadilisha ndege maana ticketi yako siyo ya moja kwa moja. Nikamwambia nimekuelewa.
Safari ilianza uwanja wa Mwalimu Nyerere kwa kupanda Emirate hadi Dubai na kubadilishiwa ndege. Hapo tulipanda ndege ijulikanayo kwa jina la Air Bus, Si wakati wake kuelezea mambo ya ndege lakini nilijifunza mengi.
Ndege hiyo ilitufikisha New York ambapo napo tulibadilisha ndege na kupanda AA (American Airways) ingekuwa bongo basi ni Air Tanzania, hizi ni kama daladala hapa kwetu maana kila baada ya muda mfupi zinaruka yaani ziko nyingi mno.
Amerikan Airways ni ndege ya ndani na mimi nilimtaarifu mwenyeji wangu ya kuwa ndio tumebadili ndege hapa Dubai naja moja kwa moja tafadhali nipokee.
Naye hakufanya ajizi aliwasili airpot pale Dallas lakini upande wa international airpot sio local airpot.
Hapo ndipo ngoma ya kinyakyusa ilipoanza. Marekani kubadili ndege kwenda upande wa local flight inabidi upande treni kwani kuna utofauti wa umbali kati ya local na international flights.
Rafiki yangu alichanganyikiwa maana hakuniona name sikuwa na simu kwani hata Dubai nilitumia call box. Akili ilichoka hata kujiongeza nikawa nimeshindwa. Nikabaki najisemea Kyala Ndula (Mungu nisaidie).
Rafiki alirudi nyumbani kwake baada ya kukaa sana airpot na kutomuona mgeni wake.
Usiombe kupotea ugenini tena Marekani utajuta kuzaliwa.
Baadaye sana kama baada ya masaa 8 kupita ndipo nikapata wazo la kuuliza huduma ya simu na kuoneshwa.
Nilipompigia alikuja mara moja na tulilia kilio cha furaha maana du. Acha niishie hapa.
UNAKWENDA WAPI?
Compas, Vibao barabarani, Simu, Ramani ya jinsi ya kufika maeneo mbalimbali, Kuuliza watu, Kwenda kituo cha polisi na mengine mengi husaidia mtu kufika aendako.
Sasa mimi leo nitaongelea ubao wenye alama ya kukuelekeza kwenye maisha ya ndoto zako.
Ubao wenye alama ioneshayo eneo fulani liliko kwa kamshale kaoneshako uelekeo husaidia kwa wageni kuelekea waendako.
Mara nyingi mbao za jinsi hii uwekwa njia ya panda. Lakini pia maeneo hayo huwepo pia na vibao vyenye kukuonya labda juu ya spidi au kuwataadharisha waendesha baiskeli na au wanyama baada ya umbali kidogo hivyo unataadharishwa kupunguza mwendo zaidi.
Sasa chukulia unaendesha gari katika mji usio na sheria za barabarani, na ni ruksa kuendesha upande wowote na mbaya zaidi hakuna vibao vya kukupa maelezo wala alama za barabarani isitoshe mji wenyewe una pilikapilika za magari mara upigiwe honi tena ile kali mara utukanwe ati mzembe yaani kila aina ya adha na wakati mwingine mtu huja mpaka kwenye gari yako na kukutolea maneno makali. Madereva wenzangu mnajua ninachoongelea Na kila ukiangalia unaona barabara zina magari mengi kupindukia, mara nao waendesha baiskeli wamo utafikiri msafara wa mamba maana kenge hawaishi kujihudhurisha, bodaboda bila kumsahau mjomba ake bajaji – Je utajisikia salama katika hali ya mazingira hayo?
Je, Una nafasi gani uliyonayo katika hali kama hii kufika eneo uendalo ukiwa na uhakika wa usalama wako?
Hebu fikiria tena ya kuwa unaendesha gari katika mji wa ugenini na ghafla unajikuta umefika kwenye makutano ya barabara nne lakini hakuna vibao vya maelekezo ya wapi sasa uende na kibaya Zaidi huna GPS (Navigation Equipment in your car)… kuchanganyikiwa ndio kitu pekee kitakachokuwa kikiendelea kwenye ubongo wako.
Haitoshi kuendesha kwa usalama/uangalifu, yakupasa pia uendeshe kwa kuelekea muelekeo sahihi. Hii ndiyo sababu haswa ya kwa nini tuna vibao barabarani na pia alama za barabarani.
Sheria za barabarani, alama za barabarani na vipao vyenye maelekezo ya kukuelekeza uendako viko ili kukupa amri (Instruct), kukuongoza, na pia kukuonya kwa watumiaji wote wa barabara - vyote vikiwa na lengo kuu moja ambalo ni ulinzi na usalama. Yote hayo ni kwa ajili ya kuwasaidia watumiaji wote wa barabara kuweza kufikia maeneo waliyokusudia wakiwa salama
Tunapokuwa safarini katika maisha yetu kuelekea kwenye vituo vyetu yaani maisha ya ndoto zetu, kuishi maisha kama ambavyo tungependa kuishi – na haya maisha ambayo tungependa kuyaishi, kwa kupitia njia ambayo muumba (kwa wengine dunia) ina alama zake na kibao murua chenye kuonesha uelekeako kwa kila mwanadamu yaani hata wewe usomaye ujumbe huu ili tuweze jishughulisha kama ulivyo mwongozo na kutuhakikishia usalama wa kuhakikisha tunafika tulikokusudiwa.
Ukishindwa kusoma, pia kuelewa na kujishikamanisha kwa kuwa na maisha ya kufuata alama na mshale ukuongozao kitakachozaliwa ni utachelewa kufika kwenye kituo chako au utaishia kwenye kituo ambacho hukukusudia.
Ninachokijua ya kuwa ndio alama ya barabara ya kutupeleka kila mmoja kwenye kituao chake yaani maisha ya ndoto yako kwa bahati nzuri mwenyezi Mungu mwenye kutupa ndoto na pia ametuwekea vibao vitatu na kila kimoja kina alama yake navyo ni AMANI, FURAHA, NA TATU NI UWEZO WA KUZALISHA/KUGAWA ULIVYOVIPATA KWA KUWA MTII KUFUATA ALAMA. (GIVING BACK TO COMMUNITY WHICH IS AN ULTIMATE GOAL FOR EVERY HUMAN BEING) kwa kifupi nikitumia lugha ya wenzetu ni sawa na kusema vibao hivyo ni PHD – Peace, Happiness, Delivery.
Ashukuriwe Mungu kwa ubunifu aliompa mwanadamu katika suala la kusaidiana kufika maeneo ya ugenini kwani kuna vitu mbali mbali vimsaidiavyo mwanadamu kuweza kufika aendako.
Nakumbuka mimi binafsi kwa mara yangu ya kwanza kwenda Marekani. Haikuwa jambo rahisi.
Ninaye rafiki aishie Marekani na familia yake kwa muda sasa. Hivyo tuliandikiana na kunipatia namba zake za simu akiwa marekani na za mke wake na simu za nyumbani ili tu kutengeneza mazingira ya kupokelewa kirahisi na nisipate usumbufu nchi za watu na tena nchi yenyewe marekani.
Nilimpatia details za ticket ambazo zilionesha hadi muda wa kuwasili Dallas. Simaanishi daladala maana vijana hamishi kusema mzee kateleza, hayo ni majina ya nchi za wenzetu. Eneo hilo liko TEXAS nchini Marekani.
Nakumbuka aliniuliza swali moja unapokuja uwe unaniambia ndege unayokuja nayo maana kuna eneo najua utabadilisha ndege maana ticketi yako siyo ya moja kwa moja. Nikamwambia nimekuelewa.
Safari ilianza uwanja wa Mwalimu Nyerere kwa kupanda Emirate hadi Dubai na kubadilishiwa ndege. Hapo tulipanda ndege ijulikanayo kwa jina la Air Bus, Si wakati wake kuelezea mambo ya ndege lakini nilijifunza mengi.
Ndege hiyo ilitufikisha New York ambapo napo tulibadilisha ndege na kupanda AA (American Airways) ingekuwa bongo basi ni Air Tanzania, hizi ni kama daladala hapa kwetu maana kila baada ya muda mfupi zinaruka yaani ziko nyingi mno.
Amerikan Airways ni ndege ya ndani na mimi nilimtaarifu mwenyeji wangu ya kuwa ndio tumebadili ndege hapa Dubai naja moja kwa moja tafadhali nipokee.
Naye hakufanya ajizi aliwasili airpot pale Dallas lakini upande wa international airpot sio local airpot.
Hapo ndipo ngoma ya kinyakyusa ilipoanza. Marekani kubadili ndege kwenda upande wa local flight inabidi upande treni kwani kuna utofauti wa umbali kati ya local na international flights.
Rafiki yangu alichanganyikiwa maana hakuniona name sikuwa na simu kwani hata Dubai nilitumia call box. Akili ilichoka hata kujiongeza nikawa nimeshindwa. Nikabaki najisemea Kyala Ndula (Mungu nisaidie).
Rafiki alirudi nyumbani kwake baada ya kukaa sana airpot na kutomuona mgeni wake.
Usiombe kupotea ugenini tena Marekani utajuta kuzaliwa.
Baadaye sana kama baada ya masaa 8 kupita ndipo nikapata wazo la kuuliza huduma ya simu na kuoneshwa.
Nilipompigia alikuja mara moja na tulilia kilio cha furaha maana du. Acha niishie hapa.
UNAKWENDA WAPI?
Compas, Vibao barabarani, Simu, Ramani ya jinsi ya kufika maeneo mbalimbali, Kuuliza watu, Kwenda kituo cha polisi na mengine mengi husaidia mtu kufika aendako.
Sasa mimi leo nitaongelea ubao wenye alama ya kukuelekeza kwenye maisha ya ndoto zako.
Ubao wenye alama ioneshayo eneo fulani liliko kwa kamshale kaoneshako uelekeo husaidia kwa wageni kuelekea waendako.
Mara nyingi mbao za jinsi hii uwekwa njia ya panda. Lakini pia maeneo hayo huwepo pia na vibao vyenye kukuonya labda juu ya spidi au kuwataadharisha waendesha baiskeli na au wanyama baada ya umbali kidogo hivyo unataadharishwa kupunguza mwendo zaidi.
Sasa chukulia unaendesha gari katika mji usio na sheria za barabarani, na ni ruksa kuendesha upande wowote na mbaya zaidi hakuna vibao vya kukupa maelezo wala alama za barabarani isitoshe mji wenyewe una pilikapilika za magari mara upigiwe honi tena ile kali mara utukanwe ati mzembe yaani kila aina ya adha na wakati mwingine mtu huja mpaka kwenye gari yako na kukutolea maneno makali. Madereva wenzangu mnajua ninachoongelea Na kila ukiangalia unaona barabara zina magari mengi kupindukia, mara nao waendesha baiskeli wamo utafikiri msafara wa mamba maana kenge hawaishi kujihudhurisha, bodaboda bila kumsahau mjomba ake bajaji – Je utajisikia salama katika hali ya mazingira hayo?
Je, Una nafasi gani uliyonayo katika hali kama hii kufika eneo uendalo ukiwa na uhakika wa usalama wako?
Hebu fikiria tena ya kuwa unaendesha gari katika mji wa ugenini na ghafla unajikuta umefika kwenye makutano ya barabara nne lakini hakuna vibao vya maelekezo ya wapi sasa uende na kibaya Zaidi huna GPS (Navigation Equipment in your car)… kuchanganyikiwa ndio kitu pekee kitakachokuwa kikiendelea kwenye ubongo wako.
Haitoshi kuendesha kwa usalama/uangalifu, yakupasa pia uendeshe kwa kuelekea muelekeo sahihi. Hii ndiyo sababu haswa ya kwa nini tuna vibao barabarani na pia alama za barabarani.
Sheria za barabarani, alama za barabarani na vipao vyenye maelekezo ya kukuelekeza uendako viko ili kukupa amri (Instruct), kukuongoza, na pia kukuonya kwa watumiaji wote wa barabara - vyote vikiwa na lengo kuu moja ambalo ni ulinzi na usalama. Yote hayo ni kwa ajili ya kuwasaidia watumiaji wote wa barabara kuweza kufikia maeneo waliyokusudia wakiwa salama
Tunapokuwa safarini katika maisha yetu kuelekea kwenye vituo vyetu yaani maisha ya ndoto zetu, kuishi maisha kama ambavyo tungependa kuishi – na haya maisha ambayo tungependa kuyaishi, kwa kupitia njia ambayo muumba (kwa wengine dunia) ina alama zake na kibao murua chenye kuonesha uelekeako kwa kila mwanadamu yaani hata wewe usomaye ujumbe huu ili tuweze jishughulisha kama ulivyo mwongozo na kutuhakikishia usalama wa kuhakikisha tunafika tulikokusudiwa.
Ukishindwa kusoma, pia kuelewa na kujishikamanisha kwa kuwa na maisha ya kufuata alama na mshale ukuongozao kitakachozaliwa ni utachelewa kufika kwenye kituo chako au utaishia kwenye kituo ambacho hukukusudia.
Ninachokijua ya kuwa ndio alama ya barabara ya kutupeleka kila mmoja kwenye kituao chake yaani maisha ya ndoto yako kwa bahati nzuri mwenyezi Mungu mwenye kutupa ndoto na pia ametuwekea vibao vitatu na kila kimoja kina alama yake navyo ni AMANI, FURAHA, NA TATU NI UWEZO WA KUZALISHA/KUGAWA ULIVYOVIPATA KWA KUWA MTII KUFUATA ALAMA. (GIVING BACK TO COMMUNITY WHICH IS AN ULTIMATE GOAL FOR EVERY HUMAN BEING) kwa kifupi nikitumia lugha ya wenzetu ni sawa na kusema vibao hivyo ni PHD – Peace, Happiness, Delivery.
Maoni
Chapisha Maoni