Tabia yetu sisi ni matunda ya vile vitu vidogo vidogo tunavyofanya kila siku.
Ufanisi tulio nao siyo chochote zaidi ya tabia zetu. Mafanikio hayaji kwa siku moja bali ni tabia zetu ndo zinatuvusha kutoka eneo moja A kuelekea eneo lingine B.
Katika maisha yetu ya kila siku tunaweza kupata changamoto katika kujenga tabia zetu kwa sababu ya vikwazo na visingizio mbali mbali.
Jinsi ya kuondoa vikwazo na visingizio hivyo ni lazima kuangalia nidhamu zetu, motisha tulizo nazo na pia jinsi tunavyojijengea malengo na tabia zetu.
Unapojiwekea malengo unakuwa unachukua hatua nzito na ya maana katika kupangilia maisha yako.
Kupangilia kwa kuandika malengo na utekelezaji wa malengo ni vitu ni tofauti.
Kujijengea tabia fulani ni hatua muhimu zaidi ya kukusaidia kusonga mbele.
Kwa mfano nina lengo la kusoma vitabu kumi mwaka 2018. Hilo ni lengo zuri.
Mfano wa pili ni kujifunza tabia ya kusoma kurasa kumi au zaidi kila siku. Hiyo ni tabia.
Ukilinganisha malengo na tabia ya hii mifano yetu utagundua kwamba tabia ina nguvu ya kukufikisha mbali zaidi. Kivipi?
Ukijenga tabia ya kusoma kurasa kumi au zaidi kila mwaka unaweza kuzidi lengo lako la vitabu kumi kwa mwaka. Unaona je hilo?
Ukifanyia kazi malengo yako bila kujijengea tabia mahsusi ya kutenda, unaweza kujikuta mwaka umeisha na umesoma vitabu 7 tu. Au hata chini ya hapo maana hakuna tabia uliyoiruhusu ikupe mwongozo maalum.
Lazima kuchukua hatua za kugeuza malengo yako kuwa tabia. Tunaona tofauti ya tabia na malengo kwa mapana zaidi.
- Tunataka kujifunza ujasiriamali. Tunaweza kuamua kujifunza kwa miezi sita (lengo) au tunaweza kuamua kutenga lisaa limoja kila siku kujifunza mambo ya ujasiriamali (Tabia)
- Tunahitaji kusoma vitabu zaidi. Twaweza kujiwekea lengo la kumaliza kitabu kimoja kwa mwezi (Lengo) au
tukasoma kurasa 10 kwa siku (Tabia)
- Foleni inaweza kutuzuia kuona watoto kila asubuhi maana unajikuta umeondoka kabla hawajaamka na ulirudi wameshalala. Tunaweza kuamua kutengeneza muda wa lisaa limoja kila siku kuona watoto(Lengo) au tukachagua piga ua tuwahi kula nao chakula cha jioni. Tunaweza kuacha mazoea ya kufanya kazi ili kukwepa foleni au kupitia mahali happy hour kusubiri foleni ipungue (Tabia)
Lea kuchukua hatua madhubuti tujielewe, tuelewe majukumu yetu, na pia jinsi tabia zilivyo na nguvu ya kubadilisha maisha yetu, tunaweza kujitengenezea miujiza na kufanya maisha yawe matamu sana. Ni kwa kubadilisha mifumo na ratiba zetu pekee ndo tutaweza kuogelea kwenye mafanikio tunayoyahitaji.
Tukijifunza tabia zetu. Tukabadilisha zile mbaya kuwa nzuri ndivyo tutakavyoweza kufikia malengo yetu kwa unafuu zaidi. Usishangae hata mzigo wa maumivu ya kufikia malengo yako yakatimia.
Malengo yako ni muhimu katika juhudi ya kufika unakoelekea. Ila tabia zako zikishazoeleka unakuwa kama ndege isiyohitaji rubani.
Mfano mzuri ni kunawa uso au kupiga maswaki asubuhi. Huhitaji kuambiwa tena kama mtoto mdogo maana imeshakuwa ni tabia yako.
Hapa Karakana ya Ubongo tumeshatoa ratiba ya matukio ya mwaka 2018.(Angalia Kalenda yako kwa maelezo zaidi)
Kuna matukio matatu makubwa ambayo ni:
1) Annual Newsletter ambayo unatoka December 2018
2 Kutoa vitabu viwili vizuri vyenye kuelimisha, mwezi wa Sita na Kumi na Mbili
3. Kuendesha Warsha mbili mwezi wa Sita na Kumi na Mbili
Pia kuna tukio maalumu dogo kwa kutupima lakini kubwa kwa kuipatia Gari yetu Karakana ya Ubongo mwanzo mzuri.
Ni sisi wenyewe tutaamua kama gari yetu ichukue mfumo wa ndala kutoka sehemu A kwenda sehemu B. Pia tunaweza kuigeuza iruke kwa kutembelea mabawa yake huku mwili ukiwa umetulia(static) kwa mfumo wa Helikopta. Au itembee kwa kuruka kwa kutumia mwili huku mabawa yametulia(static).
Ufanisi tulio nao siyo chochote zaidi ya tabia zetu. Mafanikio hayaji kwa siku moja bali ni tabia zetu ndo zinatuvusha kutoka eneo moja A kuelekea eneo lingine B.
Katika maisha yetu ya kila siku tunaweza kupata changamoto katika kujenga tabia zetu kwa sababu ya vikwazo na visingizio mbali mbali.
Jinsi ya kuondoa vikwazo na visingizio hivyo ni lazima kuangalia nidhamu zetu, motisha tulizo nazo na pia jinsi tunavyojijengea malengo na tabia zetu.
Unapojiwekea malengo unakuwa unachukua hatua nzito na ya maana katika kupangilia maisha yako.
Kupangilia kwa kuandika malengo na utekelezaji wa malengo ni vitu ni tofauti.
Kujijengea tabia fulani ni hatua muhimu zaidi ya kukusaidia kusonga mbele.
Kwa mfano nina lengo la kusoma vitabu kumi mwaka 2018. Hilo ni lengo zuri.
Mfano wa pili ni kujifunza tabia ya kusoma kurasa kumi au zaidi kila siku. Hiyo ni tabia.
Ukilinganisha malengo na tabia ya hii mifano yetu utagundua kwamba tabia ina nguvu ya kukufikisha mbali zaidi. Kivipi?
Ukijenga tabia ya kusoma kurasa kumi au zaidi kila mwaka unaweza kuzidi lengo lako la vitabu kumi kwa mwaka. Unaona je hilo?
Ukifanyia kazi malengo yako bila kujijengea tabia mahsusi ya kutenda, unaweza kujikuta mwaka umeisha na umesoma vitabu 7 tu. Au hata chini ya hapo maana hakuna tabia uliyoiruhusu ikupe mwongozo maalum.
Lazima kuchukua hatua za kugeuza malengo yako kuwa tabia. Tunaona tofauti ya tabia na malengo kwa mapana zaidi.
- Tunataka kujifunza ujasiriamali. Tunaweza kuamua kujifunza kwa miezi sita (lengo) au tunaweza kuamua kutenga lisaa limoja kila siku kujifunza mambo ya ujasiriamali (Tabia)
- Tunahitaji kusoma vitabu zaidi. Twaweza kujiwekea lengo la kumaliza kitabu kimoja kwa mwezi (Lengo) au
tukasoma kurasa 10 kwa siku (Tabia)
- Foleni inaweza kutuzuia kuona watoto kila asubuhi maana unajikuta umeondoka kabla hawajaamka na ulirudi wameshalala. Tunaweza kuamua kutengeneza muda wa lisaa limoja kila siku kuona watoto(Lengo) au tukachagua piga ua tuwahi kula nao chakula cha jioni. Tunaweza kuacha mazoea ya kufanya kazi ili kukwepa foleni au kupitia mahali happy hour kusubiri foleni ipungue (Tabia)
Lea kuchukua hatua madhubuti tujielewe, tuelewe majukumu yetu, na pia jinsi tabia zilivyo na nguvu ya kubadilisha maisha yetu, tunaweza kujitengenezea miujiza na kufanya maisha yawe matamu sana. Ni kwa kubadilisha mifumo na ratiba zetu pekee ndo tutaweza kuogelea kwenye mafanikio tunayoyahitaji.
Tukijifunza tabia zetu. Tukabadilisha zile mbaya kuwa nzuri ndivyo tutakavyoweza kufikia malengo yetu kwa unafuu zaidi. Usishangae hata mzigo wa maumivu ya kufikia malengo yako yakatimia.
Malengo yako ni muhimu katika juhudi ya kufika unakoelekea. Ila tabia zako zikishazoeleka unakuwa kama ndege isiyohitaji rubani.
Mfano mzuri ni kunawa uso au kupiga maswaki asubuhi. Huhitaji kuambiwa tena kama mtoto mdogo maana imeshakuwa ni tabia yako.
Hapa Karakana ya Ubongo tumeshatoa ratiba ya matukio ya mwaka 2018.(Angalia Kalenda yako kwa maelezo zaidi)
Kuna matukio matatu makubwa ambayo ni:
1) Annual Newsletter ambayo unatoka December 2018
2 Kutoa vitabu viwili vizuri vyenye kuelimisha, mwezi wa Sita na Kumi na Mbili
3. Kuendesha Warsha mbili mwezi wa Sita na Kumi na Mbili
Pia kuna tukio maalumu dogo kwa kutupima lakini kubwa kwa kuipatia Gari yetu Karakana ya Ubongo mwanzo mzuri.
Ni sisi wenyewe tutaamua kama gari yetu ichukue mfumo wa ndala kutoka sehemu A kwenda sehemu B. Pia tunaweza kuigeuza iruke kwa kutembelea mabawa yake huku mwili ukiwa umetulia(static) kwa mfumo wa Helikopta. Au itembee kwa kuruka kwa kutumia mwili huku mabawa yametulia(static).
Maoni
Chapisha Maoni