Wazo La Leo
Habari ya leo rafiki na msomaji wa mtiririko wa Makala za kila siku zijulikanazo kama wazo la leo.
Leo nataka niongelee kidogo juu ya upinzani uliopo kati ya ubongo na moyo.
Ninapoanza kuelezea naomba nikuulize kitu kitogo: Je unajua kwa uhakika wewe una kitu kisicho cha kawaida ndani yako kiwezacho kubadili kabisa maisha yako na mengine yakawa stori?
Kama hujui naomba nikuambie ya kwamba maisha unayoishi sasa mfanano wake ni tone ndani ya bahari. Huna haja ya kuwa tone kwani wewe ni bahari.
Sababu moja kubwa inayokufanya ushindwe kuishi kwa viwango vya juu ambapo ni haki yako ni ukinzani uliopo kati ya moyo na ubongo.
Unaweza kuona jambo linafanywa na mtu na ukajisemea moyoni ya kuwa nami naweza kufanya lile afanyalo yule (MOYO). Ghafla unaanza kujiongelesha hivi nitawezaje (UBONGO)? Yaani unaanza angalia uwezakano wa wewe kufanya na ukiendelea kutafakari unajiambia siwezi. Sasa ubongo umesema huwezi lakini na unakuuliza utawezaje. Sasa usipojua kinachoendelea ndani yako utabaki hapo hapo hata miaka ishirini ukitafakari ivi mimi kivipi naweza kuwa kama Bakhresa, Mengi, Mohamed Dewji au Aliko Dangote.
Ukweli ni kwamba chochote unachokiona mwanadamu mwingine anakifanya nawe unauwezo na kuzidi, tatizo hujui jinsi ya kushikamana, moyo unakwamishwa na ubongo ukijaribu kutafari ni kwa jinsi gani waweza na matokeo yake hata kuthubutu unashindwa.
Kimsingi ukitaka kuamsha uwezo ullio nao kuna siri unatakiwa uijue nayo ni hii:-
· Kaa chini ukiwa na notibuku yako. Kisha anza kuandika kila kitu unachohitaji ambacho moyo wako umekuwa ukitamania. Angalizo: Nimekuambia orodhesha sasa wewe unaanza kujiuliza hivi si nitaonekana kichaa mtu akisoma ati nimeandika V8 kweli mimi naweza miliki V8 (UBONGO). Hapo utakwama na inawezekana hata zoezi la kuorodhesha mambo yote utamanio ukaacha. Siri ni moja itendayo kazi hutakiwi hata siku moja kujiuliza utafanyaje kupata ulivyoviorodhesha kwa sababu namna gani si kazi yako, bali kazi yako ni kuusikiliza moyo unataka nini.
Kama hujawahi fanya hili zoezi, naomba leo nikusihii nunua kakauntabuku kenye kava ngumu maana utakuwa na kicho kikaunta buku kwa maisha yako yote. Utakachoshangazwa ni tiki za kukamilishwa kwa yale uliyoorodhesha kila baada ya kipindi.
Sasa nakuambia iwapo pesa si tatizo je ungependa kuwa/kumiliki nini? Orodhesha idadi angalu 100 ya uyatakayo iwapo pesa ingalikuwa si tatizo. Hivi ndivyo watu wawezavyo kuorodhesha ndoto za maisha yao.
· Orodha hiyo ipitie kila siku asubuhi na jioni na unapoipitia tafadhali ipitie kwa hisia. Mfano ukifika kwenye V8 unaweza ukapozi huku ukifikiria utakavyokuwa ukiiendesha alafu unaisikia mpaka harufu ya upya wa gari ukiwa umo ndani. Fanya hivyo asubuhi na jioni kila siku. Utashangaa kwa jinsi utakavyoanza kupata kimoja baada ya kingine. Kifupi ni kwamba kivipi utaweza hiyo inakuja yenyewe wewe usitoe nafasi ya kuzuiliwa kuandika matamanio yako ati itawekana vipi. Nikuambiacho ni kwamba INAWEZEKANA KUWA ZAIDI YA DANGOTE NA WENGINE UNAOWAFAHAMU.Njia hii ni moja ya njia chache za kumstua jemedari wewe UNAYEKOROMA. Kama utapata shida njoo inbox au panga tukutane tupanuane mawazo.
Nimalizie kwa kusema, namnukuu Less Brown (My mentor) – Kuzaliwa kwako kulisababisha vifo vya ndugu zako wapatao 399,999,999 . Kifipi? Mchakato wa wewe kuzaliwa ulikuwa hivi: baba yako aliachia mbengu zipatazo 400,000,000 na zikaanza mbio kukimbilia yai kwa mama yako na mbegu yako ilikuwa na kasi Bombadia itasubiri na kuwai kushikamana na yai la mama yako kitendo hicho kikasababisha ndugu zako 399,999,999 wauwawe wewe jemedari uzaliwe. Fikia kwa kina – Mungu hakuwa mjinga kukuruhusu wewe uje. Aliona makubwa na ya kutisha utakayoyafanya duniani. Wewe ni faida si hasara naomba nikuhakikishie hilo.
Shida makelele yamekuwa mengi hadi unashindwa kujitambua. Naomba nikupe ushauri wa bure:-
· TV ni mcheleweshaji wa kufika utakako punguza muda wa kuiangalia upate muda wa kufanya mengine ya maana na kama utaweza kama mimi achana nayo kabisa.
· Tafuta marafiki wa maana
· Amusha kiu ya kujifunza. Haigharimu chochote kwa mshumaa unaowaka kuuwasha uliozimia. Utaanza kuamka taaratibu kupitia mafunzo mbalimbali.
· Kusoma vitabu fananisha na kula chakula. Ukisema huna muda wa kusoma je muda wa kula unatoka wapi?
· Ondoka kijiweni, maongezi ya ushabiki, siasa, mpira kuongelea watu HAVITAKUSAIDIA.
Ninakushukuru sana kwa kuweza kunifuatilia na nikuombe kuwa huru kunipigia, au kuniandikia. Pamoja tunaweza.
Seth Simon Mwakitalu
Entrepreneurship Consultant and Lifestyle Trainer.
Tel:- +255 754 441325; +255 714 051174; +255 788 493836
Email: ssmwakitalu2013@gmail.com
Website: www.qls.com
Be Ready To Learn/Karakana Ya Ubongo.
We empower people:-
1. Achieve life and Career goals through part-time business venture.
2. Acquire life changing business skills.
3. Prepare for retirement.
Habari ya leo rafiki na msomaji wa mtiririko wa Makala za kila siku zijulikanazo kama wazo la leo.
Leo nataka niongelee kidogo juu ya upinzani uliopo kati ya ubongo na moyo.
Ninapoanza kuelezea naomba nikuulize kitu kitogo: Je unajua kwa uhakika wewe una kitu kisicho cha kawaida ndani yako kiwezacho kubadili kabisa maisha yako na mengine yakawa stori?
Kama hujui naomba nikuambie ya kwamba maisha unayoishi sasa mfanano wake ni tone ndani ya bahari. Huna haja ya kuwa tone kwani wewe ni bahari.
Sababu moja kubwa inayokufanya ushindwe kuishi kwa viwango vya juu ambapo ni haki yako ni ukinzani uliopo kati ya moyo na ubongo.
Unaweza kuona jambo linafanywa na mtu na ukajisemea moyoni ya kuwa nami naweza kufanya lile afanyalo yule (MOYO). Ghafla unaanza kujiongelesha hivi nitawezaje (UBONGO)? Yaani unaanza angalia uwezakano wa wewe kufanya na ukiendelea kutafakari unajiambia siwezi. Sasa ubongo umesema huwezi lakini na unakuuliza utawezaje. Sasa usipojua kinachoendelea ndani yako utabaki hapo hapo hata miaka ishirini ukitafakari ivi mimi kivipi naweza kuwa kama Bakhresa, Mengi, Mohamed Dewji au Aliko Dangote.
Ukweli ni kwamba chochote unachokiona mwanadamu mwingine anakifanya nawe unauwezo na kuzidi, tatizo hujui jinsi ya kushikamana, moyo unakwamishwa na ubongo ukijaribu kutafari ni kwa jinsi gani waweza na matokeo yake hata kuthubutu unashindwa.
Kimsingi ukitaka kuamsha uwezo ullio nao kuna siri unatakiwa uijue nayo ni hii:-
· Kaa chini ukiwa na notibuku yako. Kisha anza kuandika kila kitu unachohitaji ambacho moyo wako umekuwa ukitamania. Angalizo: Nimekuambia orodhesha sasa wewe unaanza kujiuliza hivi si nitaonekana kichaa mtu akisoma ati nimeandika V8 kweli mimi naweza miliki V8 (UBONGO). Hapo utakwama na inawezekana hata zoezi la kuorodhesha mambo yote utamanio ukaacha. Siri ni moja itendayo kazi hutakiwi hata siku moja kujiuliza utafanyaje kupata ulivyoviorodhesha kwa sababu namna gani si kazi yako, bali kazi yako ni kuusikiliza moyo unataka nini.
Kama hujawahi fanya hili zoezi, naomba leo nikusihii nunua kakauntabuku kenye kava ngumu maana utakuwa na kicho kikaunta buku kwa maisha yako yote. Utakachoshangazwa ni tiki za kukamilishwa kwa yale uliyoorodhesha kila baada ya kipindi.
Sasa nakuambia iwapo pesa si tatizo je ungependa kuwa/kumiliki nini? Orodhesha idadi angalu 100 ya uyatakayo iwapo pesa ingalikuwa si tatizo. Hivi ndivyo watu wawezavyo kuorodhesha ndoto za maisha yao.
· Orodha hiyo ipitie kila siku asubuhi na jioni na unapoipitia tafadhali ipitie kwa hisia. Mfano ukifika kwenye V8 unaweza ukapozi huku ukifikiria utakavyokuwa ukiiendesha alafu unaisikia mpaka harufu ya upya wa gari ukiwa umo ndani. Fanya hivyo asubuhi na jioni kila siku. Utashangaa kwa jinsi utakavyoanza kupata kimoja baada ya kingine. Kifupi ni kwamba kivipi utaweza hiyo inakuja yenyewe wewe usitoe nafasi ya kuzuiliwa kuandika matamanio yako ati itawekana vipi. Nikuambiacho ni kwamba INAWEZEKANA KUWA ZAIDI YA DANGOTE NA WENGINE UNAOWAFAHAMU.Njia hii ni moja ya njia chache za kumstua jemedari wewe UNAYEKOROMA. Kama utapata shida njoo inbox au panga tukutane tupanuane mawazo.
Nimalizie kwa kusema, namnukuu Less Brown (My mentor) – Kuzaliwa kwako kulisababisha vifo vya ndugu zako wapatao 399,999,999 . Kifipi? Mchakato wa wewe kuzaliwa ulikuwa hivi: baba yako aliachia mbengu zipatazo 400,000,000 na zikaanza mbio kukimbilia yai kwa mama yako na mbegu yako ilikuwa na kasi Bombadia itasubiri na kuwai kushikamana na yai la mama yako kitendo hicho kikasababisha ndugu zako 399,999,999 wauwawe wewe jemedari uzaliwe. Fikia kwa kina – Mungu hakuwa mjinga kukuruhusu wewe uje. Aliona makubwa na ya kutisha utakayoyafanya duniani. Wewe ni faida si hasara naomba nikuhakikishie hilo.
Shida makelele yamekuwa mengi hadi unashindwa kujitambua. Naomba nikupe ushauri wa bure:-
· TV ni mcheleweshaji wa kufika utakako punguza muda wa kuiangalia upate muda wa kufanya mengine ya maana na kama utaweza kama mimi achana nayo kabisa.
· Tafuta marafiki wa maana
· Amusha kiu ya kujifunza. Haigharimu chochote kwa mshumaa unaowaka kuuwasha uliozimia. Utaanza kuamka taaratibu kupitia mafunzo mbalimbali.
· Kusoma vitabu fananisha na kula chakula. Ukisema huna muda wa kusoma je muda wa kula unatoka wapi?
· Ondoka kijiweni, maongezi ya ushabiki, siasa, mpira kuongelea watu HAVITAKUSAIDIA.
Ninakushukuru sana kwa kuweza kunifuatilia na nikuombe kuwa huru kunipigia, au kuniandikia. Pamoja tunaweza.
Seth Simon Mwakitalu
Entrepreneurship Consultant and Lifestyle Trainer.
Tel:- +255 754 441325; +255 714 051174; +255 788 493836
Email: ssmwakitalu2013@gmail.com
Website: www.qls.com
Be Ready To Learn/Karakana Ya Ubongo.
We empower people:-
1. Achieve life and Career goals through part-time business venture.
2. Acquire life changing business skills.
3. Prepare for retirement.
Maoni
Chapisha Maoni