Wazo La Leo: Acha Visingizio
Habari za leo mpendwa msomaji wa wazo la leo.
Karibu tena kuweza kufuatana nami katika mtiririko wa Makala mbalimbali nizitoazo kila siku ili kuweza kusaidiana katika safari yetu ya maisha.
Leo ningependa kuongelea kwa sehemu juu ya mada niliyoiita ‘ACHA VISINGIZIO’
Imekuwa jambo la kawaida kwa tulio wengi kuacha kuongea ukweli badala yake twakimbilia kutoa visingizio. Leo tutajadili baadhi ya maeneo ili tuone tunavyojidangaya.
Hebu fikiria mtu asemaye siku moja nitafanya hiki na kile. Sentensi hii japo haijasema ni kisingizio bali ni kisingizio tosha.
Siku moja hiyo iko wapi? Na kwani nini siku hiyo moja. Usidanganyike siku sahihi ni leo. Hebu boresha maisha yako kwa kuchukua hatua. Leo ni siku njema mno kufanya kitu. Acha uzembe na binafsi nachukuia watu wazembe. Inuka katende ulitakalo.
Ni vizuri tukajua jinsi ya kupambana na hofu katika maisha zitupelekazo kutoa visingizio. Ufumbuzi sahihi ni kuhakikisha una kitu cha kufanya mbele yako. Hakikisha si mtu wa kijiweni yaani asiyejua la kufanya zaidi ya kuongelea siasa, masihala na sasa kuna janga la watu kuzama ziwani basi utazani wewe ndiye mbunge maana unavyochambua uzembe uliosababisha na kuonesha masikitiko utadhani u mtu wa maana, lakini ukweli unatwanga maji kwenye kinu. Sijui ukimaliza kutwanga utapata nini. Tafadhali jishughulishe.
Pia nitaongelea suala la nani hupenda kuwa naye mara nyingi. Yaani ni akina nani twaweza sema ndio marafiki zako wakubwa. Hapa pana ukweli kwamba ukichukuwa watu watano walio karibu sana nawe na ukajumlisha vipato vyao kwa mwezi na ukagawa kwa 5 jibu utakalopata ndio kipato chako kwa mwezi na huwezi zidi hapo. Sasa unakazana kusema mambo hayakunyookei sijui nini tatizo maana kuhangaika unahangaika lakini maisha hayaendi.
Sikiliza, chagua kipato utakacho na kisha orodhesha wenye kipato hicho utamanicho, kisha tafta namna utakavyooanza kuhusiana nao. Mahusiano ni kila kitu maishani. Chagua marafiki kwa uangalifu wengine ni shida.
Nikiwa naelekea kumalizia Makala yangu naomba kukushauri - PUNGUZA KAMA HUWEZI KUACHA KUTAZAMA TV ili upate muda wa kusoma vitabu. Hii tabia ya kusema unashindwa kusoma vitabu ati huna muda ni kitendo cha kushangaza. Nani alikuambia kuna mtu anagawa muda. Muda upo kwa kila mtu masaa 24. Mipangilio yako ya kutumia muda ndio ya kuangalia. Unaposema huna muda tafsiri yake hujaona umuhimu wa kufanya kitu tofauti badala yake unasema huna muda. Kauli hiyo si sahihi. Mbona unapenda kuangalia movies na hazikupiti ila kusoma vitabu huna muda. Amka chukua hatua.
Ninakushukuru sana kwa kuweza kunifuatilia na nikuombe kuwa huru kunipigia, au kuniandikia. Pamoja tunaweza.
Seth Simon Mwakitalu
Entrepreneurship Consultant and Lifestyle Trainer.
Tel:- +255 754 441325; +255 714 051174; +255 788 493836
Email: ssmwakitalu2013@gmail.com
Website: www.qls.com
Be Ready To Learn/Karakana Ya Ubongo.
We empower people:-
1. Achieve life and Career goals through part-time business venture.
2. Acquire life changing business skills.
3. Prepare for retirement.
Habari za leo mpendwa msomaji wa wazo la leo.
Karibu tena kuweza kufuatana nami katika mtiririko wa Makala mbalimbali nizitoazo kila siku ili kuweza kusaidiana katika safari yetu ya maisha.
Leo ningependa kuongelea kwa sehemu juu ya mada niliyoiita ‘ACHA VISINGIZIO’
Imekuwa jambo la kawaida kwa tulio wengi kuacha kuongea ukweli badala yake twakimbilia kutoa visingizio. Leo tutajadili baadhi ya maeneo ili tuone tunavyojidangaya.
Hebu fikiria mtu asemaye siku moja nitafanya hiki na kile. Sentensi hii japo haijasema ni kisingizio bali ni kisingizio tosha.
Siku moja hiyo iko wapi? Na kwani nini siku hiyo moja. Usidanganyike siku sahihi ni leo. Hebu boresha maisha yako kwa kuchukua hatua. Leo ni siku njema mno kufanya kitu. Acha uzembe na binafsi nachukuia watu wazembe. Inuka katende ulitakalo.
Ni vizuri tukajua jinsi ya kupambana na hofu katika maisha zitupelekazo kutoa visingizio. Ufumbuzi sahihi ni kuhakikisha una kitu cha kufanya mbele yako. Hakikisha si mtu wa kijiweni yaani asiyejua la kufanya zaidi ya kuongelea siasa, masihala na sasa kuna janga la watu kuzama ziwani basi utazani wewe ndiye mbunge maana unavyochambua uzembe uliosababisha na kuonesha masikitiko utadhani u mtu wa maana, lakini ukweli unatwanga maji kwenye kinu. Sijui ukimaliza kutwanga utapata nini. Tafadhali jishughulishe.
Pia nitaongelea suala la nani hupenda kuwa naye mara nyingi. Yaani ni akina nani twaweza sema ndio marafiki zako wakubwa. Hapa pana ukweli kwamba ukichukuwa watu watano walio karibu sana nawe na ukajumlisha vipato vyao kwa mwezi na ukagawa kwa 5 jibu utakalopata ndio kipato chako kwa mwezi na huwezi zidi hapo. Sasa unakazana kusema mambo hayakunyookei sijui nini tatizo maana kuhangaika unahangaika lakini maisha hayaendi.
Sikiliza, chagua kipato utakacho na kisha orodhesha wenye kipato hicho utamanicho, kisha tafta namna utakavyooanza kuhusiana nao. Mahusiano ni kila kitu maishani. Chagua marafiki kwa uangalifu wengine ni shida.
Nikiwa naelekea kumalizia Makala yangu naomba kukushauri - PUNGUZA KAMA HUWEZI KUACHA KUTAZAMA TV ili upate muda wa kusoma vitabu. Hii tabia ya kusema unashindwa kusoma vitabu ati huna muda ni kitendo cha kushangaza. Nani alikuambia kuna mtu anagawa muda. Muda upo kwa kila mtu masaa 24. Mipangilio yako ya kutumia muda ndio ya kuangalia. Unaposema huna muda tafsiri yake hujaona umuhimu wa kufanya kitu tofauti badala yake unasema huna muda. Kauli hiyo si sahihi. Mbona unapenda kuangalia movies na hazikupiti ila kusoma vitabu huna muda. Amka chukua hatua.
Ninakushukuru sana kwa kuweza kunifuatilia na nikuombe kuwa huru kunipigia, au kuniandikia. Pamoja tunaweza.
Seth Simon Mwakitalu
Entrepreneurship Consultant and Lifestyle Trainer.
Tel:- +255 754 441325; +255 714 051174; +255 788 493836
Email: ssmwakitalu2013@gmail.com
Website: www.qls.com
Be Ready To Learn/Karakana Ya Ubongo.
We empower people:-
1. Achieve life and Career goals through part-time business venture.
2. Acquire life changing business skills.
3. Prepare for retirement.
Maoni
Chapisha Maoni