Wazo La Leo
Hongera sana mwanakarakana ya ubongo kwa siku hii nyingine nzuri sana ya leo.
Ni nafasi bora na ya kipekee sana kwetu kwenda kuweka juhudi kubwa ili kuweza kupata matokeo bora sana.
Jana niliiishia kwa kusema:-
Utaratibu/njia zitakazo kusaidia kupakua mawazo ni hizi zifuatazo:-
1. Nunua kinoti buku chenye ukubwa wa kuingia kwenye mfuko wa shati na kwa akina dada/mama iwe na uwezo wa kukaa kwenye pochi. Yaani popote ulipo ni lazima uwe na noti buku na peni.
2. Moja ya njia rahisi sana ya kupakua mawazo inaitwa kwa lugha ya wenzetu ‘PRIME HOUR’ ambayo nikitafsiri Kiswahili ni ‘SAA MOJA MUHIMU’. Hii inamaanisha nini. Katika ratiba yako ya kutwa nzima ambayo wewe unaijua vizuri ina mchanganyiko wa shughuli. Sasa kanuni hii inasema katika hizo shughuli chagua baadhi ya shughuli utakazo zifanya kwa kutumia kanuni hii ya PRIME HOUR.
Mfano ratiba yangu ya leo iko hivi:
• Kumshukuru Mungu kuniamsha salama
• Kutahajudi
• Kusoma biblia
• Kunywa maji ya vuguvugu yaliyochanganywa na limau
• Kuandaa Makala ya wazo la leo
• Kuoga na kuvaa
• Kupata kifungua kinywa
• Kuelekea Kanisani
• Kupata Lunch
• Kikao na mkurugenzi wa kampuni X
• Kusoma Kitabu
• Kumtembelea rafiki yangu
• Kupata matunda (Dinner)
• Kukaa nusu saa nikiwa peke yangu ili kutafakari siku ilivyo isha na kupanga mambo ya kesho (TO DO LIST).
• Kusikiliza video za mentor wangu Less Brown
• Kuoga na kulala
Sasa kwa lengo la kupakua mawazo nachagua KUANDAA MAKALA YA LEO, KUSIKILIZA IBADA, KIKAO NA MKURUGENZI NA KUSOMA KITABU.
Hapo nimechagua shughuli nne na kila moja nitaifanya kwa saa moja isipokuwa kanisani ni masaa matatu. Hivyo kwa leo nitakuwa na PRIME HOUR zangu 6.
Kivipi? Nitakapokua nikiandaa Makala yangu ya leo, nitazima simu, kama kuna paka nitamtoa nje, nitakaa mahali ambapo hakuna mtu wa kuniingilia. Hivyo mawazo yangu yote, yatabaki kwenye kuandaa Makala tu. Sitokuwa na kitu kingine cha kuingilia nifanyapo shughuli yangu.
Nimalizapo kuandaa Makala nitachukua noti buku na peni na mawazo yataanza kutoka name nitayaandika. Nitafanya vivyo hivyo kwa shughuli zangu zote za leo. Maana yake masaa 6 yangu ya leo ni PRIME HOUR. SIJUI WEWE LEO UNA PRIME HOURS NGAPI?
Sasa leo hebu tuendelee na njia zingine za kupakua mawazo:-
1. Mapumziko:- Ukiwa umepumzika na kutojishughulisha na chochote, mfano umelala iwe ni usiku au mchana. Yawezekana kabisa katikati ya mapumziko/usingizi ukakurupuka na ukawa na mawazo kibao. Unashauriwa hata ukilala hii noti buku (Brain Damping Note Book) ya kupakuwa mawazo iwe pembeni ya kitanda chako ili ukiamka tu uweze kuchukua na kuandika.
2. KUTAHAJUDI (MEDITATION) – Moja kati ya njia muhimu sana na ambayo kila mwana karakana ya ubongo hana budi kuijua ni KUTAHAJUDI (MEDITATION).
Hii njia ni ya muhimu sana kwa kuwa inafaida lukuki. Panapo majaliwa kesho tutashirikishana somo hili la kutahajudi na namna ya kutahajudi. Mara nyingi ukimaliza kutahajudi mawazo hutirirka nawe kuweza kuyapakua.
Naona niishie hapo kutiririka. Mwenye kuelewa na aelewe. Mabadiliko huanza na wewe.
Ninakushukuru sana kwa kuweza kunifuatilia na nikuombe kuwa huru kunipigia, au kuniandikia. Pamoja tunaweza
Seth Simon Mwakitalu
Senior Auditor, Entrepreneurship Consultant, Coach and Lifestyle Trainer.
Tel:- +255 754 441325; +255 714 051174; +255 788 493836
Email: ssmwakitalu2013@gmail.com
Websites:www.karakanayaubongo.blogspot.com;
:www.bereadytolearn.org
We empower people:-
1. Achieve life and Career goals through part-time business venture.
2. Acquire life changing business skills.
3. Prepare for retirement.
Hongera sana mwanakarakana ya ubongo kwa siku hii nyingine nzuri sana ya leo.
Ni nafasi bora na ya kipekee sana kwetu kwenda kuweka juhudi kubwa ili kuweza kupata matokeo bora sana.
Jana niliiishia kwa kusema:-
Utaratibu/njia zitakazo kusaidia kupakua mawazo ni hizi zifuatazo:-
1. Nunua kinoti buku chenye ukubwa wa kuingia kwenye mfuko wa shati na kwa akina dada/mama iwe na uwezo wa kukaa kwenye pochi. Yaani popote ulipo ni lazima uwe na noti buku na peni.
2. Moja ya njia rahisi sana ya kupakua mawazo inaitwa kwa lugha ya wenzetu ‘PRIME HOUR’ ambayo nikitafsiri Kiswahili ni ‘SAA MOJA MUHIMU’. Hii inamaanisha nini. Katika ratiba yako ya kutwa nzima ambayo wewe unaijua vizuri ina mchanganyiko wa shughuli. Sasa kanuni hii inasema katika hizo shughuli chagua baadhi ya shughuli utakazo zifanya kwa kutumia kanuni hii ya PRIME HOUR.
Mfano ratiba yangu ya leo iko hivi:
• Kumshukuru Mungu kuniamsha salama
• Kutahajudi
• Kusoma biblia
• Kunywa maji ya vuguvugu yaliyochanganywa na limau
• Kuandaa Makala ya wazo la leo
• Kuoga na kuvaa
• Kupata kifungua kinywa
• Kuelekea Kanisani
• Kupata Lunch
• Kikao na mkurugenzi wa kampuni X
• Kusoma Kitabu
• Kumtembelea rafiki yangu
• Kupata matunda (Dinner)
• Kukaa nusu saa nikiwa peke yangu ili kutafakari siku ilivyo isha na kupanga mambo ya kesho (TO DO LIST).
• Kusikiliza video za mentor wangu Less Brown
• Kuoga na kulala
Sasa kwa lengo la kupakua mawazo nachagua KUANDAA MAKALA YA LEO, KUSIKILIZA IBADA, KIKAO NA MKURUGENZI NA KUSOMA KITABU.
Hapo nimechagua shughuli nne na kila moja nitaifanya kwa saa moja isipokuwa kanisani ni masaa matatu. Hivyo kwa leo nitakuwa na PRIME HOUR zangu 6.
Kivipi? Nitakapokua nikiandaa Makala yangu ya leo, nitazima simu, kama kuna paka nitamtoa nje, nitakaa mahali ambapo hakuna mtu wa kuniingilia. Hivyo mawazo yangu yote, yatabaki kwenye kuandaa Makala tu. Sitokuwa na kitu kingine cha kuingilia nifanyapo shughuli yangu.
Nimalizapo kuandaa Makala nitachukua noti buku na peni na mawazo yataanza kutoka name nitayaandika. Nitafanya vivyo hivyo kwa shughuli zangu zote za leo. Maana yake masaa 6 yangu ya leo ni PRIME HOUR. SIJUI WEWE LEO UNA PRIME HOURS NGAPI?
Sasa leo hebu tuendelee na njia zingine za kupakua mawazo:-
1. Mapumziko:- Ukiwa umepumzika na kutojishughulisha na chochote, mfano umelala iwe ni usiku au mchana. Yawezekana kabisa katikati ya mapumziko/usingizi ukakurupuka na ukawa na mawazo kibao. Unashauriwa hata ukilala hii noti buku (Brain Damping Note Book) ya kupakuwa mawazo iwe pembeni ya kitanda chako ili ukiamka tu uweze kuchukua na kuandika.
2. KUTAHAJUDI (MEDITATION) – Moja kati ya njia muhimu sana na ambayo kila mwana karakana ya ubongo hana budi kuijua ni KUTAHAJUDI (MEDITATION).
Hii njia ni ya muhimu sana kwa kuwa inafaida lukuki. Panapo majaliwa kesho tutashirikishana somo hili la kutahajudi na namna ya kutahajudi. Mara nyingi ukimaliza kutahajudi mawazo hutirirka nawe kuweza kuyapakua.
Naona niishie hapo kutiririka. Mwenye kuelewa na aelewe. Mabadiliko huanza na wewe.
Ninakushukuru sana kwa kuweza kunifuatilia na nikuombe kuwa huru kunipigia, au kuniandikia. Pamoja tunaweza
Seth Simon Mwakitalu
Senior Auditor, Entrepreneurship Consultant, Coach and Lifestyle Trainer.
Tel:- +255 754 441325; +255 714 051174; +255 788 493836
Email: ssmwakitalu2013@gmail.com
Websites:www.karakanayaubongo.blogspot.com;
:www.bereadytolearn.org
We empower people:-
1. Achieve life and Career goals through part-time business venture.
2. Acquire life changing business skills.
3. Prepare for retirement.
Maoni
Chapisha Maoni