Wazo La Leo:
Hongera sana mwanakarakana ya ubongo kwa siku hii nyingine nzuri sana ya leo.
Ni nafasi bora na ya kipekee sana kwetu kwenda kuweka juhudi kubwa ili kuweza kupata matokeo bora sana.
Moja ya jambo linalofanya wengi wachelewe kufikia mafanikio ni suala zima la ufanisi.
Leo nitagusia maeneo machache yatakayokusaidia kuongeza ufanisi wa kila utendacho.
1. Jua kupangilia vipaumbele vyako. Waweza kuwa na mambo kumi ya kufanya leo. Unachotakiwa kufanya ni kuanza na kile kilicho muhimu yaani ukifanyapo kinakusogeza kwa sehemu kuelekea lengo lako, kisha kinachofuata kwa umuhimu hadi unafikia cha mwisho. Hivyo utafuata mpangilio uliojiwekea hadi siku yako inakwisha. Ukijizoeza kufanya hivi kila siku, utaona mabadiliko katika maisha yako ya utendaji.
2. Jiambie mara kwa mara ya kwamba kwako msamiati wa kushindwa haupo. Ni kupambana mpaka kieleweke. Maisha si rahisi kivile. Dunia huzawadia majemedari na si walegevu/wachovu/wakata tamaa. Ni majemedari tu ndio hufanikisha maisha. Acha kabisa kuongelea kushindwa au kusema vyuma vimekaza. Hakuna kipindi kizuri kupata pesa kama tulicho nacho iwapo utaishughulisha akili. INAWEZEKANA SONGA MBELE.
3. Jipe nidhamu wewe mwenyewe. Maisha ya mtu asiye na nidhamu atasubiri sana. Nini maana ya nidhamu. Didhamu ni kufanya kile ulichojiambia utafanya bila kuangalia unajisikiaje, wewe ni kufanya tu. Kwa kawaida mwanadamu ni mvivu. Hiyo ni asili ya kila mmoja wetu. Sasa namna nzuri ya kushughulikia uvivu ni kupangilia mambo yako siku moja kabla na ukiamka unafuata mipango yako na kutekeleza. Achana na kuingiliwa, mara ebu fungua watsapp nimekutumia kitu. Muda wa kusoma watsapp kama zina umuhimu panga na sio kila wakati upo kwenye watsapp. Kufanya hivyo kutakusaidia sana kukuongezea ufanisi.
4. Fanya mazoezi kila siku ya kujitathmini. Ikifika jioni mara baada ya shughuli. Jitenge peke yako pasipo makelele ya aina yoyote na anza kutathmini siku yako ilivyoisha na jiulize unatakiwa uboreshe nini. Fanyia mazoezi kila siku na utaona unavyo badilika kiutendaji.
5. Jifunze kusema HAPANA. Maisha ya kufurahisha watu yamepitwa na wakati na pia haioneshi ukomavu. Jifunze kusema hapana na achana kufanya mambo ili uonekane mwema. Tabia ya kupenda kufurahisha watu haitakuacha salama.
6. Okoa muda kwa kukasimisha shughuli zako. Anza kupitia shughuli ulizopanga iwapo ni lazima uzifanye wewe mwenyewe au waweza mtuma mtu afanye hata kwa ujira kidogo. Mfano nataka kwenda kulipia bima ya gari langu Posta nami niko Mbezi mwisho. Swali la kujiuliza ni kweli hakuna kabisa mtu wa kumpa shughuli hii mpaka mimi mwenyewe niende? Mara nyingi tunajishughulisha na vitu ambavyo tunaweza kukasimisha na kuokoa muda kufanya mambo yenye tija. Anza leo kujiuliza na ukiona iko namna ya kukasimisha basi usifanye.
7. Unazungukwa na nini nyumbani kwako, ofisini kwako, gerejini kwako nk. Jenga tabia ya kuchambua vitu unavyohitaji na sio kujaza vitu vingi visivyohitajika. Gawa au tupa kama havifai kugawa na baki na eneo lenye kuvutia na hewa sawi inayokuhamasisha kufanya zaidi.
8. Kuwa bora wewe mwenyewe. Moja ya jambo litakalokusaidia ni aina ya watu wanaokuzunguka. Chagua watu wenye kukuongezea kitu. Achanana kupendelea kila wakati kuzungukwa na watu wanaokutegemea wewe. Kila mara kukusifia yaani hawakufanyi ufikirike bali wewe ndiye mfalme wao. UNAJICHELEWESHA. Zunguka na watu unaopenda maisha yao na yumkini siku moja ufikie hatua waliyo nayo.
Naona niishie hapo kutiririka nitaendelea kesho na Makala hii. Mwenye kuelewa na aelewe. Mabadiliko huanza na wewe.
Ninakushukuru sana kwa kuweza kunifuatilia na nikuombe kuwa huru kunipigia, au kuniandikia. Pamoja tunaweza
Seth Simon Mwakitalu
Senior Auditor, Entrepreneurship Consultant, Coach and Lifestyle Trainer.
Tel:- +255 754 441325; +255 714 051174; +255 788 493836
Email: ssmwakitalu2013@gmail.com
Websites:www.karakanayaubongo.blogspot.com;
:www.bereadytolearn.org
We empower people:-
1. Achieve life and Career goals through part-time business venture.
2. Acquire life changing business skills.
3. Prepare for retirement.
Hongera sana mwanakarakana ya ubongo kwa siku hii nyingine nzuri sana ya leo.
Ni nafasi bora na ya kipekee sana kwetu kwenda kuweka juhudi kubwa ili kuweza kupata matokeo bora sana.
Moja ya jambo linalofanya wengi wachelewe kufikia mafanikio ni suala zima la ufanisi.
Leo nitagusia maeneo machache yatakayokusaidia kuongeza ufanisi wa kila utendacho.
1. Jua kupangilia vipaumbele vyako. Waweza kuwa na mambo kumi ya kufanya leo. Unachotakiwa kufanya ni kuanza na kile kilicho muhimu yaani ukifanyapo kinakusogeza kwa sehemu kuelekea lengo lako, kisha kinachofuata kwa umuhimu hadi unafikia cha mwisho. Hivyo utafuata mpangilio uliojiwekea hadi siku yako inakwisha. Ukijizoeza kufanya hivi kila siku, utaona mabadiliko katika maisha yako ya utendaji.
2. Jiambie mara kwa mara ya kwamba kwako msamiati wa kushindwa haupo. Ni kupambana mpaka kieleweke. Maisha si rahisi kivile. Dunia huzawadia majemedari na si walegevu/wachovu/wakata tamaa. Ni majemedari tu ndio hufanikisha maisha. Acha kabisa kuongelea kushindwa au kusema vyuma vimekaza. Hakuna kipindi kizuri kupata pesa kama tulicho nacho iwapo utaishughulisha akili. INAWEZEKANA SONGA MBELE.
3. Jipe nidhamu wewe mwenyewe. Maisha ya mtu asiye na nidhamu atasubiri sana. Nini maana ya nidhamu. Didhamu ni kufanya kile ulichojiambia utafanya bila kuangalia unajisikiaje, wewe ni kufanya tu. Kwa kawaida mwanadamu ni mvivu. Hiyo ni asili ya kila mmoja wetu. Sasa namna nzuri ya kushughulikia uvivu ni kupangilia mambo yako siku moja kabla na ukiamka unafuata mipango yako na kutekeleza. Achana na kuingiliwa, mara ebu fungua watsapp nimekutumia kitu. Muda wa kusoma watsapp kama zina umuhimu panga na sio kila wakati upo kwenye watsapp. Kufanya hivyo kutakusaidia sana kukuongezea ufanisi.
4. Fanya mazoezi kila siku ya kujitathmini. Ikifika jioni mara baada ya shughuli. Jitenge peke yako pasipo makelele ya aina yoyote na anza kutathmini siku yako ilivyoisha na jiulize unatakiwa uboreshe nini. Fanyia mazoezi kila siku na utaona unavyo badilika kiutendaji.
5. Jifunze kusema HAPANA. Maisha ya kufurahisha watu yamepitwa na wakati na pia haioneshi ukomavu. Jifunze kusema hapana na achana kufanya mambo ili uonekane mwema. Tabia ya kupenda kufurahisha watu haitakuacha salama.
6. Okoa muda kwa kukasimisha shughuli zako. Anza kupitia shughuli ulizopanga iwapo ni lazima uzifanye wewe mwenyewe au waweza mtuma mtu afanye hata kwa ujira kidogo. Mfano nataka kwenda kulipia bima ya gari langu Posta nami niko Mbezi mwisho. Swali la kujiuliza ni kweli hakuna kabisa mtu wa kumpa shughuli hii mpaka mimi mwenyewe niende? Mara nyingi tunajishughulisha na vitu ambavyo tunaweza kukasimisha na kuokoa muda kufanya mambo yenye tija. Anza leo kujiuliza na ukiona iko namna ya kukasimisha basi usifanye.
7. Unazungukwa na nini nyumbani kwako, ofisini kwako, gerejini kwako nk. Jenga tabia ya kuchambua vitu unavyohitaji na sio kujaza vitu vingi visivyohitajika. Gawa au tupa kama havifai kugawa na baki na eneo lenye kuvutia na hewa sawi inayokuhamasisha kufanya zaidi.
8. Kuwa bora wewe mwenyewe. Moja ya jambo litakalokusaidia ni aina ya watu wanaokuzunguka. Chagua watu wenye kukuongezea kitu. Achanana kupendelea kila wakati kuzungukwa na watu wanaokutegemea wewe. Kila mara kukusifia yaani hawakufanyi ufikirike bali wewe ndiye mfalme wao. UNAJICHELEWESHA. Zunguka na watu unaopenda maisha yao na yumkini siku moja ufikie hatua waliyo nayo.
Naona niishie hapo kutiririka nitaendelea kesho na Makala hii. Mwenye kuelewa na aelewe. Mabadiliko huanza na wewe.
Ninakushukuru sana kwa kuweza kunifuatilia na nikuombe kuwa huru kunipigia, au kuniandikia. Pamoja tunaweza
Seth Simon Mwakitalu
Senior Auditor, Entrepreneurship Consultant, Coach and Lifestyle Trainer.
Tel:- +255 754 441325; +255 714 051174; +255 788 493836
Email: ssmwakitalu2013@gmail.com
Websites:www.karakanayaubongo.blogspot.com;
:www.bereadytolearn.org
We empower people:-
1. Achieve life and Career goals through part-time business venture.
2. Acquire life changing business skills.
3. Prepare for retirement.
Maoni
Chapisha Maoni