Wazo La Leo
Hongera sana mwanakarakana ya ubongo kwa siku hii nyingine nzuri sana ya leo.
Ni nafasi bora na ya kipekee sana kwetu kwenda kuweka juhudi kubwa ili kuweza kupata matokeo bora sana.
Watu wengi hujidanganya kwa kujituma sana ili wafikie mafanikio pasipo kuelewa mafanikio yana namna yake na usipoielewa hiyo namna yake itakuwa sawa na kujenga nyumba hewani (Building a castle in the air) au kutwanga maji kwenye kinu.
Ukweli wa mafanikio ni upeo (Personal Development). Una upeo kiasi gani? Au una maarifa kiasi gani kwenye Nyanja zote ambazo unataka kuyaona hayo mafanikio.
Mfano Nyanja ya pesa. Una upeo kiasi gani juu ya pesa. Kiwango ulichonacho kinatueleza upeo ulio nao juu ya pesa. Kamwe huweza kuwa na pesa kuzidi upeo wako na huo ndio ukweli.
Hakuna njia ya mkato, ongeza upeo juu ya pesa na pesa zitaongezeka. Usipoongezeka upeo, sahau kuongeza pato.
Kifupi mafanikio hayatafutwi bali yanavutwa. Ni kama sumaku. Upeo wako utavuta kwa uwiano. Upeo mdogo kila kitu kidogo, upeo wa kati, kila kitu kwa wastani na upeo uliokithiri vivyo hivyo. Hii ndio naita changamoto endelevu. Kadri unavyo lenga makubwa huna budi kuongeza uelewa (maarifa) na utashangaa utakapotengeneza kiu ya kujifunza.
Kadri unavyo weka juhudi kujifunza, kutendea kazi unayojifunza na kufundisha wengine, inabaki suala la muda tu kuona mabadiliko yako.
Ushauri wangu wa bure ‘Acha kujichanganya na mambo. Amua unataka ujazwe na nini (uelimike kwa mambo yapi) ili uweze pata matokeo uyakusudiayo. Basi weka mkakati wa kujifunza hayo mambo na kusahau makelele mengi ya dunia na ukijifunza yaiishi.
Kumbuka kujifunza peke yake hakusaidii kama si mtendaji na utendaji unataka nidhamu. Vinginevyo leo unaanza na kesho unaacha. Badiliko hutokea pale mtu anapozingatia faida na sio kujisikia.
Mimi ni mwandishi na najua faida ya uandishi ni kusaidia kundi kubwa la watu. Hivyo nisipojisikia kuandika NAANDIKA. Nikijisikia kuandika NAANDIKA TU. Hivyo kujisikia au kutojisikia hakunifungi mimi kutenda nililoamua kutenda. Ukiwa na huu msimamo, nakupa miezi sita maisha yako yatachukua sura nyingine.
Mtu mmoja aliwahi sema ‘ Ikitokea pesa azote za dunia zikikusanywa na kugawiwa kwa wanadamu wote duniani kwa usawa, haitochukua muda zitarudi kwenye mifuko ile ile na wale walio kuwa hawana watabaki hawana’.
Tatitizo ni nini? Upeo wa kuwa nazo usipoongezeka utabaki ulivyo.
Furaha kamili haitokani na unachopata bali furaha kamili hupatikana kwa jinsi unavyongezeka (Groth/Personal Development).
Naona niishie hapa. Mwenye kuelewa na aelewe. Mabadiliko huanza na wewe.
Ninakushukuru sana kwa kuweza kunifuatilia na nikuombe kuwa huru kunipigia, au kuniandikia. Pamoja tunaweza. WASAMBAZIE NA WENGINE WAJIFUNZE.
Je unataka kuwa mmoja wa watu wapendao kujifunza? Kundi la watsApp lijulikanalo kwa jina la KARAKANA YA UBONGO ni jibu lako.
Kundi lina watu wasiopungua 200 ambao hubadilishana mawazo yenye tija kila siku.
Kujiunga na kundi hili bofya hapa: https://chat.whatsapp.com/AVwbS3re0jECObi2VK5uzm
Seth Simon Mwakitalu
Senior Auditor, Entrepreneurship Consultant, Coach and Lifestyle Trainer.
Tel:- +255 754 441325; +255 714 051174; +255 788 493836
Email: ssmwakitalu2013@gmail.com
Websites:www.karakanayaubongo.blogspot.com;
:www.bereadytolearn.org
We empower people:-
1. Achieve life and Career goals through part-time business venture.
2. Acquire life changing business skills.
3. Prepare for retirement.
Hongera sana mwanakarakana ya ubongo kwa siku hii nyingine nzuri sana ya leo.
Ni nafasi bora na ya kipekee sana kwetu kwenda kuweka juhudi kubwa ili kuweza kupata matokeo bora sana.
Watu wengi hujidanganya kwa kujituma sana ili wafikie mafanikio pasipo kuelewa mafanikio yana namna yake na usipoielewa hiyo namna yake itakuwa sawa na kujenga nyumba hewani (Building a castle in the air) au kutwanga maji kwenye kinu.
Ukweli wa mafanikio ni upeo (Personal Development). Una upeo kiasi gani? Au una maarifa kiasi gani kwenye Nyanja zote ambazo unataka kuyaona hayo mafanikio.
Mfano Nyanja ya pesa. Una upeo kiasi gani juu ya pesa. Kiwango ulichonacho kinatueleza upeo ulio nao juu ya pesa. Kamwe huweza kuwa na pesa kuzidi upeo wako na huo ndio ukweli.
Hakuna njia ya mkato, ongeza upeo juu ya pesa na pesa zitaongezeka. Usipoongezeka upeo, sahau kuongeza pato.
Kifupi mafanikio hayatafutwi bali yanavutwa. Ni kama sumaku. Upeo wako utavuta kwa uwiano. Upeo mdogo kila kitu kidogo, upeo wa kati, kila kitu kwa wastani na upeo uliokithiri vivyo hivyo. Hii ndio naita changamoto endelevu. Kadri unavyo lenga makubwa huna budi kuongeza uelewa (maarifa) na utashangaa utakapotengeneza kiu ya kujifunza.
Kadri unavyo weka juhudi kujifunza, kutendea kazi unayojifunza na kufundisha wengine, inabaki suala la muda tu kuona mabadiliko yako.
Ushauri wangu wa bure ‘Acha kujichanganya na mambo. Amua unataka ujazwe na nini (uelimike kwa mambo yapi) ili uweze pata matokeo uyakusudiayo. Basi weka mkakati wa kujifunza hayo mambo na kusahau makelele mengi ya dunia na ukijifunza yaiishi.
Kumbuka kujifunza peke yake hakusaidii kama si mtendaji na utendaji unataka nidhamu. Vinginevyo leo unaanza na kesho unaacha. Badiliko hutokea pale mtu anapozingatia faida na sio kujisikia.
Mimi ni mwandishi na najua faida ya uandishi ni kusaidia kundi kubwa la watu. Hivyo nisipojisikia kuandika NAANDIKA. Nikijisikia kuandika NAANDIKA TU. Hivyo kujisikia au kutojisikia hakunifungi mimi kutenda nililoamua kutenda. Ukiwa na huu msimamo, nakupa miezi sita maisha yako yatachukua sura nyingine.
Mtu mmoja aliwahi sema ‘ Ikitokea pesa azote za dunia zikikusanywa na kugawiwa kwa wanadamu wote duniani kwa usawa, haitochukua muda zitarudi kwenye mifuko ile ile na wale walio kuwa hawana watabaki hawana’.
Tatitizo ni nini? Upeo wa kuwa nazo usipoongezeka utabaki ulivyo.
Furaha kamili haitokani na unachopata bali furaha kamili hupatikana kwa jinsi unavyongezeka (Groth/Personal Development).
Naona niishie hapa. Mwenye kuelewa na aelewe. Mabadiliko huanza na wewe.
Ninakushukuru sana kwa kuweza kunifuatilia na nikuombe kuwa huru kunipigia, au kuniandikia. Pamoja tunaweza. WASAMBAZIE NA WENGINE WAJIFUNZE.
Je unataka kuwa mmoja wa watu wapendao kujifunza? Kundi la watsApp lijulikanalo kwa jina la KARAKANA YA UBONGO ni jibu lako.
Kundi lina watu wasiopungua 200 ambao hubadilishana mawazo yenye tija kila siku.
Kujiunga na kundi hili bofya hapa: https://chat.whatsapp.com/AVwbS3re0jECObi2VK5uzm
Seth Simon Mwakitalu
Senior Auditor, Entrepreneurship Consultant, Coach and Lifestyle Trainer.
Tel:- +255 754 441325; +255 714 051174; +255 788 493836
Email: ssmwakitalu2013@gmail.com
Websites:www.karakanayaubongo.blogspot.com;
:www.bereadytolearn.org
We empower people:-
1. Achieve life and Career goals through part-time business venture.
2. Acquire life changing business skills.
3. Prepare for retirement.
Maoni
Chapisha Maoni