Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 16
Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku.
Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli
Leo tunakwenda kujifunza juu ya PESA HAITAFUTWI BALI INATENGENEZEWA NJIA.
Maisha ya utafutaji/usakaji pesa umewaacha wengi katika maumivu na wengine kupoteza maisha.
Dhana ya fedha ni vyema kuijua kwa undani. Fedha kwa lugha nyepesi ni mtumishi. Najua ninaposema mtumishi tayari umeanza kupata picha ya nini hufanywa na mtumishi.
Kwa kawaida mtumishi ni mtu wa kutumwa huko na huku ili kusaidia kufanya mambo yaende inavyotakiwa. Na mtumaji hawezi kumtuma mtu mahali ambapo hakuna uhitaji wa mtu kutumwa.
Hivyo kwangu pesa inatambulika kwa jina la mtumishi. Jirani yangu akiwa mgonjwa na hana namna ya kufika hospitali sijiulizi mara mbili kama mtumishi yupo naitisha uber na mtumishi mara moja anachukua nafasi yake na kuhakikisha mgonjwa amefika hospitali na kumfikisha kwa daktari na hatimaye kupewa dawa na kumrudisha nyumbani. Yote hayo yanawezeshwa na mtumishi pesa.
Uhitaji wa mtumishi fedha ni mkubwa mno na kama huna ndipo maisha hukosa ladha. Ladha ya maisha kwa mwanadamu ni vyema awe na fedha, ukata ni kutishia/kukosa matumaini ya maisha.
Kimsingi fedha hupatikana kupitia njia kuu mbili.
1. Fedha ipatikanayo kwa kutoa jasho (Active Income) – Hapa unahitajika wewe binafsi ujishughulishe ili uweze kuzipata fedha iwe kwa kujiajiri au kuajiriwa. Hapa ni pamoja na waajiriwa na wanao fanya biashara binafsi (kununua na kuuza, ushauri wa kitaalamu, nk). Fedha ya aina hii ina ukomo na ni vyema ukawa na mpango wa kuachana nayo kama si kupunguza kasi ya namna ya kuzipata.
Shida ya aina hii ya upatikanaji wa fedha inakutegemea wewe, na itokeapo umeumwa kwa mwajiria mwisho miezi sita unastafishwa kwa sababu ya ugonjwa ikiwa na maana ya kuwa kamwe utapewa mshahara tena. Hali kama hii usababisha maisha kubadilika nyumbani.
Wewe utakuwa shahidi hata wafanyabiashara wazuri wakifa tu basi na shughuli zao hufa.
Nahitaji upate ufahamu kisawasawa juu ya upatikanaji huu wa fedha. Kwa kweli ni vyema kuanza nao lakini kuishia nao ni hatari kwa mstakabari wa maisha yako. Uwepo wa mtu mtafutaji ndio msingi wa kipato cha aina hii na kutokuwepo kwa muhusika ndio ukomo wa aina hii ya kipato.
2. Fedha mtiririko (Passive Income) – Fedha ipatikanayo kwa njia hii ndio lengo la somo la leo. Fedha za aina hii hazihitaji mtu awepo. Uwepo au usiwepo pesa zazidi kukufuata. Na hapa ndipo nisemapo acha kuzitafuta pesa bali zitengenezee njia nazo zitaanza kukufuata. Uwe unacheza golf au bao au mazoezini au unasafiri nchi mbalimbali pasipo kujishughulisha fedha zaendelea kutiririka. Hizi ndizo fedha natamani kila mmoja wetu awe na mpango nazo maana hazina ukomo.
Fedha za aina hii wengine hufananisha na upatikanaji wa fedha kwa kutumia jasho la wengine yaani pasipo wewe kujishughulisha na fedha kuendelea kuzipata.
Mfano wa shughuli za aina hii ni kama vile kumiliki vitega uchumi mfano majengo na kuwa na wapangaji ambao kila mwezi wanakulipa pango. Hapa wewe ulijitengenezea mfereji wa fedha nazo zinafuata mkondo na kukufikia. Uwe mapuzikoni au safari lazima pango lilipwe.
Mfano mwingine ni umiliki wa hisa kwenye soko la hisa au mfuko wa pamoja ambapo unanunua hisa zako na kila mwisho wa mwaka unagawiwa faida.
Hapa tunaona hakuna tena kujishughulisha bali ni kupokea fedha kwa kwenda mbele.
Hakika raha ya fedha ni kuitengenezea njia.
Acha kwa leo niishie hapa. Usikose kunifuatilia katika Makala zinazofuata.
Karakana ya ubongo tunatengeneza ubongo wako
Kwa wasioijua karakana ya ubongo ni watu waliojikusanya pamoja katika kundi la watsapp kwa lengo la kuondoa takataka kwenye ufahamu na kuanza kujifunza pamoja na kukutana angalau mara moja kwa mwezi ili kuwa chachu ndani na nje ya nchi.
Ili kujiunga yakupasa kuwasiliana nami ili kuweza kukufanyia udahili kama unavigezo vya kuwa mmoja wa wanakarakana ya ubongo.
Na kwa sasa tuna kitabu maarufu kiitwacho ‘KOPE ZAKO BAHARI YAKO’ na kama wewe ni mmoja ya wanaojipenda hiki kitabu si cha kukosa. Tuwasiliane na kuona jinsi ya kukipata.
Seth Simon Mwakitalu
Senior Auditor, Entrepreneurship Consultant, Coach and Lifestyle Trainer.
Tel:- +255 754 441325; +255 788 493836
Email: ssmwakitalu2013@gmail.com
Websites:www.karakanayaubongo.blogspot.com;
Instagram: karakana_ya_ubongo
Facebook: https://www.facebook.com/karakana-YA-Ubongo-109000130642880/?referr=whatsapp
You tube: karakanayaubongo
We empower people:-
1. Achieve life and Career goals through part-time business venture.
2. Acquire life changing business skills.
3. Prepare for retirement.
Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku.
Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli
Leo tunakwenda kujifunza juu ya PESA HAITAFUTWI BALI INATENGENEZEWA NJIA.
Maisha ya utafutaji/usakaji pesa umewaacha wengi katika maumivu na wengine kupoteza maisha.
Dhana ya fedha ni vyema kuijua kwa undani. Fedha kwa lugha nyepesi ni mtumishi. Najua ninaposema mtumishi tayari umeanza kupata picha ya nini hufanywa na mtumishi.
Kwa kawaida mtumishi ni mtu wa kutumwa huko na huku ili kusaidia kufanya mambo yaende inavyotakiwa. Na mtumaji hawezi kumtuma mtu mahali ambapo hakuna uhitaji wa mtu kutumwa.
Hivyo kwangu pesa inatambulika kwa jina la mtumishi. Jirani yangu akiwa mgonjwa na hana namna ya kufika hospitali sijiulizi mara mbili kama mtumishi yupo naitisha uber na mtumishi mara moja anachukua nafasi yake na kuhakikisha mgonjwa amefika hospitali na kumfikisha kwa daktari na hatimaye kupewa dawa na kumrudisha nyumbani. Yote hayo yanawezeshwa na mtumishi pesa.
Uhitaji wa mtumishi fedha ni mkubwa mno na kama huna ndipo maisha hukosa ladha. Ladha ya maisha kwa mwanadamu ni vyema awe na fedha, ukata ni kutishia/kukosa matumaini ya maisha.
Kimsingi fedha hupatikana kupitia njia kuu mbili.
1. Fedha ipatikanayo kwa kutoa jasho (Active Income) – Hapa unahitajika wewe binafsi ujishughulishe ili uweze kuzipata fedha iwe kwa kujiajiri au kuajiriwa. Hapa ni pamoja na waajiriwa na wanao fanya biashara binafsi (kununua na kuuza, ushauri wa kitaalamu, nk). Fedha ya aina hii ina ukomo na ni vyema ukawa na mpango wa kuachana nayo kama si kupunguza kasi ya namna ya kuzipata.
Shida ya aina hii ya upatikanaji wa fedha inakutegemea wewe, na itokeapo umeumwa kwa mwajiria mwisho miezi sita unastafishwa kwa sababu ya ugonjwa ikiwa na maana ya kuwa kamwe utapewa mshahara tena. Hali kama hii usababisha maisha kubadilika nyumbani.
Wewe utakuwa shahidi hata wafanyabiashara wazuri wakifa tu basi na shughuli zao hufa.
Nahitaji upate ufahamu kisawasawa juu ya upatikanaji huu wa fedha. Kwa kweli ni vyema kuanza nao lakini kuishia nao ni hatari kwa mstakabari wa maisha yako. Uwepo wa mtu mtafutaji ndio msingi wa kipato cha aina hii na kutokuwepo kwa muhusika ndio ukomo wa aina hii ya kipato.
2. Fedha mtiririko (Passive Income) – Fedha ipatikanayo kwa njia hii ndio lengo la somo la leo. Fedha za aina hii hazihitaji mtu awepo. Uwepo au usiwepo pesa zazidi kukufuata. Na hapa ndipo nisemapo acha kuzitafuta pesa bali zitengenezee njia nazo zitaanza kukufuata. Uwe unacheza golf au bao au mazoezini au unasafiri nchi mbalimbali pasipo kujishughulisha fedha zaendelea kutiririka. Hizi ndizo fedha natamani kila mmoja wetu awe na mpango nazo maana hazina ukomo.
Fedha za aina hii wengine hufananisha na upatikanaji wa fedha kwa kutumia jasho la wengine yaani pasipo wewe kujishughulisha na fedha kuendelea kuzipata.
Mfano wa shughuli za aina hii ni kama vile kumiliki vitega uchumi mfano majengo na kuwa na wapangaji ambao kila mwezi wanakulipa pango. Hapa wewe ulijitengenezea mfereji wa fedha nazo zinafuata mkondo na kukufikia. Uwe mapuzikoni au safari lazima pango lilipwe.
Mfano mwingine ni umiliki wa hisa kwenye soko la hisa au mfuko wa pamoja ambapo unanunua hisa zako na kila mwisho wa mwaka unagawiwa faida.
Hapa tunaona hakuna tena kujishughulisha bali ni kupokea fedha kwa kwenda mbele.
Hakika raha ya fedha ni kuitengenezea njia.
Acha kwa leo niishie hapa. Usikose kunifuatilia katika Makala zinazofuata.
Karakana ya ubongo tunatengeneza ubongo wako
Kwa wasioijua karakana ya ubongo ni watu waliojikusanya pamoja katika kundi la watsapp kwa lengo la kuondoa takataka kwenye ufahamu na kuanza kujifunza pamoja na kukutana angalau mara moja kwa mwezi ili kuwa chachu ndani na nje ya nchi.
Ili kujiunga yakupasa kuwasiliana nami ili kuweza kukufanyia udahili kama unavigezo vya kuwa mmoja wa wanakarakana ya ubongo.
Na kwa sasa tuna kitabu maarufu kiitwacho ‘KOPE ZAKO BAHARI YAKO’ na kama wewe ni mmoja ya wanaojipenda hiki kitabu si cha kukosa. Tuwasiliane na kuona jinsi ya kukipata.
Seth Simon Mwakitalu
Senior Auditor, Entrepreneurship Consultant, Coach and Lifestyle Trainer.
Tel:- +255 754 441325; +255 788 493836
Email: ssmwakitalu2013@gmail.com
Websites:www.karakanayaubongo.blogspot.com;
Instagram: karakana_ya_ubongo
Facebook: https://www.facebook.com/karakana-YA-Ubongo-109000130642880/?referr=whatsapp
You tube: karakanayaubongo
We empower people:-
1. Achieve life and Career goals through part-time business venture.
2. Acquire life changing business skills.
3. Prepare for retirement.
Maoni
Chapisha Maoni