Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 17
Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku.
Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli
Leo tunakwenda kujifunza juu ya UKOSEFU WA UFAHAMU JUU YA UWEKEZAJI.
Ninaandika hii Makala nikiwa na shukrani nyingi kwa mwenyezi Mungu kwani kwa miaka 59 (Leo niandikapo Makala ni tarehe 02.03.2020) iliyopita hii siri sikuijua kabisa na nimekuja kuijua nikiwa nimebakiza miezi michache nifikie miaka 60.
Ninashukuru kwa sababu nayaona maisha yangu yakiwa na pande mbili, moja ni onyo juu ya yapi usiyafanye au kuyafuata maana mimi nimeshuhudia madhara hasi ambayo nimeyaishi kwa kuyafanya hayo ambayo leo nasimama kwa ujasiri nikiwaonya wote wanaosoma hii makala wasiyafanye/wasiyafuate.
Lakini upande wa pili wa maisha yangu nimebeba mambo mazuri ya wewe kuyafuata au kuyafanya maana nimeona namna yalivyofanyika baraka si tu kwangu bali kwa familia nzima. Haya nitazidi kusisitiza kuyafuata.
Hivyo kwa ujumla wake pande hizi mbili leo zinanipa mamlaka ya kuandika na kuandika ili kila asomaye afaidike.
Sasa linapokuja suala la ufahamu juu ya uwekezaji – sina budi kulielezea kwa kukazia maarifa maana mimi nimekuwa nikiishi na pia nimesoma vidato vyote pamoja na chuo lakini hakuna mtu aliyethubutu kunifundisha nikafundishika na kuchukua hatua achali mbali maisha yangu ya kazi kama mwalimu wa fizikia na hisabati pamoja na kuwa meneja wa uhasibu na mwishowe mkaguzi mwandamizi bado suala la ufahamu juu ya uwekezaji lilikuwa mithili ya umbali ulivyo kati ya Tanzania na Marekani.
Kutokujua au kutokuwa na ufahamu juu ya uwekezaji si suala la kufurahia hata kidogo kwani limechelewesha wengi kufikia mafanikiona kubaki kwenye dimbwi la umasikini.
Shida ninayoipata ni pale makanisani elimu hii pia imekuwa adimu. Kutofundishwa kwa elimu hii si kwamba wachungaji na wasaidizi hawapendi kufundisha bali tatizo walio wengi kama si wote hawajui. Hivyo hili linafanya hali kuwa mbaya zaidi na wale wanaofahamu wamejikuta wakijitenga kwa kutofundisha. Mungu atusaidie.
‘Kazi yao wapumbavu huwachosha kila mmoja, Maana hajui hata njia ya kuuendea mji.’ Mhubiri 10:15
Watu wengi hawajui jinsi ya kuipata elimu hii ya uwekezaji ambayo ni ya muhimu kwa mstakabali wa maisha yetu.
Hakuna atakaye kupangia kesho yako iwapo hutaipangilia mwenyewe.
Ukosefu wa ufahamu juu ya uwekezaji umewaacha wengi katika dimbwi la umasikini, kuishiwa (ukata), na ugumu wa maisha.
Mtu yeyote atakaye mafanikio analazimika kufanya juhudi ya makusudi kuhakikisha ufamu wake unaelewa na kuchukua hatua kuhakikisha mambo yanatokea na si hadithi tena.
Wengi wetu tumekuwa vizuizi kwa walio wengi kwa kuwakatisha tamaa juu ya uwekezaji na kama matokeo wengi wameishia kuwa na mawazo hasi juu ya uwekezaji na kujikuta wanaendelea katika umasikini. Njia pekee ni kuhakikisha tunaondokana kabisa na mawazo hasi (mgando).
Tutaendelea kujifunza aina 5 za ufahamu uliotiwa sumu juu ya uwekezaji.
Acha kwa leo niishie hapa. Usikose kunifuatilia katika Makala zinazofuata.
Karakana ya ubongo tunatengeneza ubongo wako
Kwa wasioijua karakana ya ubongo ni watu waliojikusanya pamoja katika kundi la watsapp kwa lengo la kuondoa takataka kwenye ufahamu na kuanza kujifunza pamoja na kukutana angalau mara moja kwa mwezi ili kuwa chachu ndani na nje ya nchi.
Ili kujiunga yakupasa kuwasiliana nami ili kuweza kukufanyia udahili kama unavigezo vya kuwa mmoja wa wanakarakana ya ubongo.
Na kwa sasa tuna kitabu maarufu kiitwacho ‘KOPE ZAKO BAHARI YAKO’ na kama wewe ni mmoja ya wanaojipenda hiki kitabu si cha kukosa. Tuwasiliane na kuona jinsi ya kukipata.
Seth Simon Mwakitalu
Senior Auditor, Entrepreneurship Consultant, Coach and Lifestyle Trainer.
Tel:- +255 754 441325; +255 788 493836
Email: ssmwakitalu2013@gmail.com
Websites:www.karakanayaubongo.blogspot.com;
Instagram: karakana_ya_ubongo
Facebook: https://www.facebook.com/karakana-YA-Ubongo-109000130642880/?referr=whatsapp
You tube: karakanayaubongo
We empower people:-
1. Achieve life and Career goals through part-time business venture.
2. Acquire life changing business skills.
3. Prepare for retirement.
Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku.
Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli
Leo tunakwenda kujifunza juu ya UKOSEFU WA UFAHAMU JUU YA UWEKEZAJI.
Ninaandika hii Makala nikiwa na shukrani nyingi kwa mwenyezi Mungu kwani kwa miaka 59 (Leo niandikapo Makala ni tarehe 02.03.2020) iliyopita hii siri sikuijua kabisa na nimekuja kuijua nikiwa nimebakiza miezi michache nifikie miaka 60.
Ninashukuru kwa sababu nayaona maisha yangu yakiwa na pande mbili, moja ni onyo juu ya yapi usiyafanye au kuyafuata maana mimi nimeshuhudia madhara hasi ambayo nimeyaishi kwa kuyafanya hayo ambayo leo nasimama kwa ujasiri nikiwaonya wote wanaosoma hii makala wasiyafanye/wasiyafuate.
Lakini upande wa pili wa maisha yangu nimebeba mambo mazuri ya wewe kuyafuata au kuyafanya maana nimeona namna yalivyofanyika baraka si tu kwangu bali kwa familia nzima. Haya nitazidi kusisitiza kuyafuata.
Hivyo kwa ujumla wake pande hizi mbili leo zinanipa mamlaka ya kuandika na kuandika ili kila asomaye afaidike.
Sasa linapokuja suala la ufahamu juu ya uwekezaji – sina budi kulielezea kwa kukazia maarifa maana mimi nimekuwa nikiishi na pia nimesoma vidato vyote pamoja na chuo lakini hakuna mtu aliyethubutu kunifundisha nikafundishika na kuchukua hatua achali mbali maisha yangu ya kazi kama mwalimu wa fizikia na hisabati pamoja na kuwa meneja wa uhasibu na mwishowe mkaguzi mwandamizi bado suala la ufahamu juu ya uwekezaji lilikuwa mithili ya umbali ulivyo kati ya Tanzania na Marekani.
Kutokujua au kutokuwa na ufahamu juu ya uwekezaji si suala la kufurahia hata kidogo kwani limechelewesha wengi kufikia mafanikiona kubaki kwenye dimbwi la umasikini.
Shida ninayoipata ni pale makanisani elimu hii pia imekuwa adimu. Kutofundishwa kwa elimu hii si kwamba wachungaji na wasaidizi hawapendi kufundisha bali tatizo walio wengi kama si wote hawajui. Hivyo hili linafanya hali kuwa mbaya zaidi na wale wanaofahamu wamejikuta wakijitenga kwa kutofundisha. Mungu atusaidie.
‘Kazi yao wapumbavu huwachosha kila mmoja, Maana hajui hata njia ya kuuendea mji.’ Mhubiri 10:15
Watu wengi hawajui jinsi ya kuipata elimu hii ya uwekezaji ambayo ni ya muhimu kwa mstakabali wa maisha yetu.
Hakuna atakaye kupangia kesho yako iwapo hutaipangilia mwenyewe.
Ukosefu wa ufahamu juu ya uwekezaji umewaacha wengi katika dimbwi la umasikini, kuishiwa (ukata), na ugumu wa maisha.
Mtu yeyote atakaye mafanikio analazimika kufanya juhudi ya makusudi kuhakikisha ufamu wake unaelewa na kuchukua hatua kuhakikisha mambo yanatokea na si hadithi tena.
Wengi wetu tumekuwa vizuizi kwa walio wengi kwa kuwakatisha tamaa juu ya uwekezaji na kama matokeo wengi wameishia kuwa na mawazo hasi juu ya uwekezaji na kujikuta wanaendelea katika umasikini. Njia pekee ni kuhakikisha tunaondokana kabisa na mawazo hasi (mgando).
Tutaendelea kujifunza aina 5 za ufahamu uliotiwa sumu juu ya uwekezaji.
Acha kwa leo niishie hapa. Usikose kunifuatilia katika Makala zinazofuata.
Karakana ya ubongo tunatengeneza ubongo wako
Kwa wasioijua karakana ya ubongo ni watu waliojikusanya pamoja katika kundi la watsapp kwa lengo la kuondoa takataka kwenye ufahamu na kuanza kujifunza pamoja na kukutana angalau mara moja kwa mwezi ili kuwa chachu ndani na nje ya nchi.
Ili kujiunga yakupasa kuwasiliana nami ili kuweza kukufanyia udahili kama unavigezo vya kuwa mmoja wa wanakarakana ya ubongo.
Na kwa sasa tuna kitabu maarufu kiitwacho ‘KOPE ZAKO BAHARI YAKO’ na kama wewe ni mmoja ya wanaojipenda hiki kitabu si cha kukosa. Tuwasiliane na kuona jinsi ya kukipata.
Seth Simon Mwakitalu
Senior Auditor, Entrepreneurship Consultant, Coach and Lifestyle Trainer.
Tel:- +255 754 441325; +255 788 493836
Email: ssmwakitalu2013@gmail.com
Websites:www.karakanayaubongo.blogspot.com;
Instagram: karakana_ya_ubongo
Facebook: https://www.facebook.com/karakana-YA-Ubongo-109000130642880/?referr=whatsapp
You tube: karakanayaubongo
We empower people:-
1. Achieve life and Career goals through part-time business venture.
2. Acquire life changing business skills.
3. Prepare for retirement.
Maoni
Chapisha Maoni