Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 26
Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku.
Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli
Leo tunakwenda kujifunza juu ya kwa nini uko jinsi ulivyo.
Kwa nini uko njinsi ulivyo – Kuna mambo unatakiwa kuyajua ambayo yanachangia sana kukutengeneza na kuonekana jinsi ulivyo. Leo tunakwenda kuangalia jambo la tatu linalomtengeneza mtu:-
UMEZUNGUKA NCHI YAKO/DUNIA KWA KIWANGO GANI? – Kitendo cha kuzalia, kukulia, kusoma na kisha maisha katika nchi yako bila kuona sehemu nyingine ya dunia ikoje kumembupaza wengi na mbaya zaidi wengine wamezaliwa kijiji X wamesoma kijiji X wameoa kiji X na maisha yote hadi kuzeeka na kufa wangali kijiji X. Niambie mtu wa jinsi hiyo atakuwaje kuchukulia mambo maana ayajuayo ni ndani ya mipaka yake na wala hajui upande mwinge wa dunia mambo yakoje. Watu wa jinsi hii wameishia na maisha yasiyoridhisha na kuwa na mtazamo usiozidi mipaka yao.
Mithali 4:7
Bora hekima, basi jipatie hekima; Naam, kwa mapato yako yote jipatie ufahamu.
Ashukuriwe Mungu kuzunguka dunia haikuhitaji tena mpaka usafiri, waweza kutembea na kujifunza vitu vingi na kukubadili na kuwa mtu wa manufaa sana kupitia kusoma vitabu, kusikiliza vitabu, tapes,magazeti, videos, maandiko mbalimbali, wasifU wa watu mashuhuri, kufahamiana na watu mbalimbali nk. Vitu vyote hivi vinatusaidia kupata udhoefu wa maeneo mbalimbali kana kwamba tumekuwa tukisafiri sana kumbe la hasha.
Kile unachokichukua ili kikusaidie kukuza ufahamu wako kinahitaji uchaguzi maana vingine si vizuri. Hivyo yakupasa kuwa mwangalifu na kama huelewi bora uulize usaidiwe.
Chukua tahadhali kutojihusisha na vitu vitakavyoharibu hatima ya maisha yako.
Mithali 23:23
Inunue kweli, wala usiiuze; Naam, hekima, na mafundisho, na ufahamu.
Lini ilikuwa mara ya mwisho kujisomea kitabu?
Lini ilikuwa mara ya mwisho kwenda kutembelea nchi au mkoa tofauti na uishipo ili kupumzika na kujifunza?
Lini mara ya mwisho uliweza kujifunza kitu kipya kupitia kitabu, au video au magazeti au tapes au mafunzo nk?
USIKUBALI KURUHUSU KUTO JIFUNZA IWE KWA KUTOKA NJE YA MIPAKA YAKO AU AKUJISOMEA NK KUKUNYIME KUPANUKA KIMAWAZO. MUNGU ATUSAIDIE.
Acha kwa leo niishie hapa tutaendeleza somo hili katika Makala ijayo. Usikose kunifuatilia katika Makala zinazofuata.
Karakana ya ubongo tunatengeneza ubongo wako
Kwa wasioijua karakana ya ubongo ni watu waliojikusanya pamoja katika kundi la watsapp kwa lengo la kuondoa takataka kwenye ufahamu na kuanza kujifunza pamoja na kukutana angalau mara moja kwa mwezi ili kuwa chachu ndani na nje ya nchi.
Ili kujiunga yakupasa kuwasiliana nami ili kuweza kukufanyia udahili kama unavigezo vya kuwa mmoja wa wanakarakana ya ubongo.
Na kwa sasa tuna kitabu maarufu kiitwacho ‘KOPE ZAKO BAHARI YAKO’ na kama wewe ni mmoja ya wanaojipenda hiki kitabu si cha kukosa. Tuwasiliane na kuona jinsi ya kukipata.
Seth Simon Mwakitalu
Senior Auditor, Entrepreneurship Consultant, Coach and Lifestyle Trainer.
Tel:- +255 754 441325; +255 788 493836
Email: ssmwakitalu2013@gmail.com
Websites:www.karakanayaubongo.blogspot.com;
Instagram: karakana_ya_ubongo
Facebook: https://www.facebook.com/karakana-YA-Ubongo-109000130642880/?referr=whatsapp
You tube: karakanayaubongo
We empower people:-
1. Achieve life and Career goals through part-time business venture.
2. Acquire life changing business skills.
3. Prepare for retirement.
Maoni
Chapisha Maoni