Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 32
Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku.
Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli
Leo tunakwenda kujifunza MAMBO MAKUU MATATU UNAYOTAKIWA KUZINGATIA JUU YA FEDHA.
Tumejifunza mengi kuhusiana na masuala ya fedha na sasa ni muhimu tukajua mambo matatu yakayotusaidia kutuweka sawa linapokuja suala la fedha.
1. Elimu juu ya fedha – Itafurahisha kama utaweka kipaumbele kujikumbusha mara kwa mara juu ya hii elimu kwani kurudia rudia imethibitika kuwa ni njia bora kufanya jambo unalorudia kushikamana na ubongo wako wa ndani (sub-conscious mind) na kusababisha utekelezaji wa jambo husika kuwa rahisi zaidi kuliko kutorudiarudia. Sote tunahitaji hii elimu na ingewezekana mashuleni pia ifundishwe.
2. Kuipangilia fedha – Tabia ya kupata pesa na kuanza kuitumia ndio imetufikisha hapa tulipo. Mtu yeyote makini akipata tu pesa huipangilia katika mpangilio uliothibitika kuwa bora zaidi 30/70 na waweza ongeza kadri vyanzo vya pesa viongezekapo. Yawezekana ndio kwanza unasoma makala zangu kwa mara ya kwanza ila kwa wafuatiliaji wa Makala zangu wakisikia tu 30/70 tayari wanajua mpangilio wa fedha:-
10% - Ni Dhaka kama u muumini na kama si muumini saidia makundi yenye uhitaji
10% - Tunza na ikifikia kiwango cha kuweza kuanzisha mradi itoe ulipoitunza na anzisha mradi. Hivyo hatutunzi fedha kwa lengo la kutunza bali twataka ifikie kiwango cha kuanzisha mradi ulio katika mpango. Inashauriwa kutunza sehemu ambayo si rahisi kuichukua kirahisi. Sehemu sahihi uanzapo utaratibu wa kutunza fedha (kusave) ni mfuko wa umoja (UTT) waulizie bank ya CRDB watakuelimisha au njoo inbox nikutumia elimu ya mfuko wa umoja. Hii itakusaidia kukujengea tabia ya kutunza bila kutoa toa mpaka ifikie kiwango utakacho.
10% - Hii ni maalum kwa kununua shares, tresurry bonds, tresurry bills nk ila bado nashauri kama ndio unaanza tabia hii adimu ni vyema ujiunge na mfuko wa Umoja (UTT) . Kimsingi ukiweza kutunza 20% kwenye mfuko wa umoja basi 10% itabaki kwenye mfuko na 10% utaichukua kuanzisha mradi.
3. NIDHAMU YA PESA – Kuna msemo mitaani unasema tumia pesa mpaka ikutambue pia wengine husema tumia pesa utapata akili ya kuitafuta na mengine mengi yenye kuonesha utovu wa nidhamu juu ya fedha.
Fedha inahitaji nidhamu. Nidhamu ni kufanya kile ulichojipangia ya kuwa utafanya bila kujali hali. Ni msimamo thabiti wa utekelezaji mipango. Waweza jua elimu ya pesa na mipango ya fedha na bado ukashindwa kutekeleza na wakati mwingine ukawa mwalimu wa elimu ya fedha lakini kwako ikawa mtihani kutekeleza. Hili ni tatizo kwa kila mwanadamu atakapo kuachana na tabia ya zamani na kuanzisha tabia mpya huwa ni ligi lakini penye nia pana njia. Hili ndilo la msingi sana katika maisha na hasa kama unataka mabadiliko ni lazima kufanyia kazi ulivyojifunza. Hata maandiko husema yeye ajuaye vingi kwake vingi vitahitajika. Pia biblia inasema yeye ajuaye kutenda mema na asitende atakuwa anatenda dhambi. Mungu atusaidie.
Acha kwa leo niishie hapa tutaendeleza somo hili katika Makala ijayo. Usikose kunifuatilia katika Makala zinazofuata.
Karakana ya ubongo tunatengeneza ubongo wako
Kwa wasioijua karakana ya ubongo ni watu waliojikusanya pamoja katika kundi la watsapp kwa lengo la kuondoa takataka kwenye ufahamu na kuanza kujifunza pamoja na kukutana angalau mara moja kwa mwezi ili kuwa chachu ndani na nje ya nchi.
Ili kujiunga yakupasa kuwasiliana nami ili kuweza kukufanyia udahili kama unavigezo vya kuwa mmoja wa wanakarakana ya ubongo.
Na kwa sasa tuna kitabu maarufu kiitwacho ‘KOPE ZAKO BAHARI YAKO’ na kama wewe ni mmoja ya wanaojipenda hiki kitabu si cha kukosa. Tuwasiliane na kuona jinsi ya kukipata.
Seth Simon Mwakitalu
Senior Auditor, Entrepreneurship Consultant, Coach and Lifestyle Trainer.
Tel:- +255 754 441325; +255 788 493836
Email: ssmwakitalu2013@gmail.com
Websites:www.karakanayaubongo.blogspot.com;
Instagram: karakana_ya_ubongo
Facebook: https://www.facebook.com/karakana-YA-Ubongo-109000130642880/?referr=whatsapp
You tube: karakanayaubongo
We empower people:-
1. Achieve life and Career goals through part-time business venture.
2. Acquire life changing business skills.
3. Prepare for retirement.
Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku.
Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli
Leo tunakwenda kujifunza MAMBO MAKUU MATATU UNAYOTAKIWA KUZINGATIA JUU YA FEDHA.
Tumejifunza mengi kuhusiana na masuala ya fedha na sasa ni muhimu tukajua mambo matatu yakayotusaidia kutuweka sawa linapokuja suala la fedha.
1. Elimu juu ya fedha – Itafurahisha kama utaweka kipaumbele kujikumbusha mara kwa mara juu ya hii elimu kwani kurudia rudia imethibitika kuwa ni njia bora kufanya jambo unalorudia kushikamana na ubongo wako wa ndani (sub-conscious mind) na kusababisha utekelezaji wa jambo husika kuwa rahisi zaidi kuliko kutorudiarudia. Sote tunahitaji hii elimu na ingewezekana mashuleni pia ifundishwe.
2. Kuipangilia fedha – Tabia ya kupata pesa na kuanza kuitumia ndio imetufikisha hapa tulipo. Mtu yeyote makini akipata tu pesa huipangilia katika mpangilio uliothibitika kuwa bora zaidi 30/70 na waweza ongeza kadri vyanzo vya pesa viongezekapo. Yawezekana ndio kwanza unasoma makala zangu kwa mara ya kwanza ila kwa wafuatiliaji wa Makala zangu wakisikia tu 30/70 tayari wanajua mpangilio wa fedha:-
10% - Ni Dhaka kama u muumini na kama si muumini saidia makundi yenye uhitaji
10% - Tunza na ikifikia kiwango cha kuweza kuanzisha mradi itoe ulipoitunza na anzisha mradi. Hivyo hatutunzi fedha kwa lengo la kutunza bali twataka ifikie kiwango cha kuanzisha mradi ulio katika mpango. Inashauriwa kutunza sehemu ambayo si rahisi kuichukua kirahisi. Sehemu sahihi uanzapo utaratibu wa kutunza fedha (kusave) ni mfuko wa umoja (UTT) waulizie bank ya CRDB watakuelimisha au njoo inbox nikutumia elimu ya mfuko wa umoja. Hii itakusaidia kukujengea tabia ya kutunza bila kutoa toa mpaka ifikie kiwango utakacho.
10% - Hii ni maalum kwa kununua shares, tresurry bonds, tresurry bills nk ila bado nashauri kama ndio unaanza tabia hii adimu ni vyema ujiunge na mfuko wa Umoja (UTT) . Kimsingi ukiweza kutunza 20% kwenye mfuko wa umoja basi 10% itabaki kwenye mfuko na 10% utaichukua kuanzisha mradi.
3. NIDHAMU YA PESA – Kuna msemo mitaani unasema tumia pesa mpaka ikutambue pia wengine husema tumia pesa utapata akili ya kuitafuta na mengine mengi yenye kuonesha utovu wa nidhamu juu ya fedha.
Fedha inahitaji nidhamu. Nidhamu ni kufanya kile ulichojipangia ya kuwa utafanya bila kujali hali. Ni msimamo thabiti wa utekelezaji mipango. Waweza jua elimu ya pesa na mipango ya fedha na bado ukashindwa kutekeleza na wakati mwingine ukawa mwalimu wa elimu ya fedha lakini kwako ikawa mtihani kutekeleza. Hili ni tatizo kwa kila mwanadamu atakapo kuachana na tabia ya zamani na kuanzisha tabia mpya huwa ni ligi lakini penye nia pana njia. Hili ndilo la msingi sana katika maisha na hasa kama unataka mabadiliko ni lazima kufanyia kazi ulivyojifunza. Hata maandiko husema yeye ajuaye vingi kwake vingi vitahitajika. Pia biblia inasema yeye ajuaye kutenda mema na asitende atakuwa anatenda dhambi. Mungu atusaidie.
Acha kwa leo niishie hapa tutaendeleza somo hili katika Makala ijayo. Usikose kunifuatilia katika Makala zinazofuata.
Karakana ya ubongo tunatengeneza ubongo wako
Kwa wasioijua karakana ya ubongo ni watu waliojikusanya pamoja katika kundi la watsapp kwa lengo la kuondoa takataka kwenye ufahamu na kuanza kujifunza pamoja na kukutana angalau mara moja kwa mwezi ili kuwa chachu ndani na nje ya nchi.
Ili kujiunga yakupasa kuwasiliana nami ili kuweza kukufanyia udahili kama unavigezo vya kuwa mmoja wa wanakarakana ya ubongo.
Na kwa sasa tuna kitabu maarufu kiitwacho ‘KOPE ZAKO BAHARI YAKO’ na kama wewe ni mmoja ya wanaojipenda hiki kitabu si cha kukosa. Tuwasiliane na kuona jinsi ya kukipata.
Seth Simon Mwakitalu
Senior Auditor, Entrepreneurship Consultant, Coach and Lifestyle Trainer.
Tel:- +255 754 441325; +255 788 493836
Email: ssmwakitalu2013@gmail.com
Websites:www.karakanayaubongo.blogspot.com;
Instagram: karakana_ya_ubongo
Facebook: https://www.facebook.com/karakana-YA-Ubongo-109000130642880/?referr=whatsapp
You tube: karakanayaubongo
We empower people:-
1. Achieve life and Career goals through part-time business venture.
2. Acquire life changing business skills.
3. Prepare for retirement.
Maoni
Chapisha Maoni