Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SOMO JUU YA FEDHA /SHEKELI (SEHEMU YA 33)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 33


Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku.


Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli

Leo tunakwenda kujifunza umuhimu wa mizania katika mafanikio.


Tumejifunza mengi kuhusiana na masuala ya fedha na sasa ni muhimu tukajua umuhimu wa mizania katika mafanikio.


Kikubwa ninachotaka kukufahamisha leo ni kuwa mafanikio sahihi ni lazima yawe yametokana na uwekezaji wa kiroho na uwekezaji halisia unaoweza onekana kwa macho ya nyama.


Ni ujinga kujikita kwenye mambo ya kiroho 100% ikiwa ni pamoja na utoaji wa fungu la kumi kwa uaminifu ati kwa kuwa imeandikwa utabarikiwa kwa kuwa mwaminifu na kubaki umekaa na kusubiria baraka zimwagike. UTASUBIRI SANA na ndipo utaanza kujiuliza na kuona kama Mungu amekuacha.


Hivi unawezaje mfano kuwa mwaminifu wa fungu la kumi na kushindwa kuwa mwaminifu wa kuwekeza 10% kwa uaminifu kama ilivyo kwa fungu la kumi na ukafuata kanuni zote za kufanikisha, na uone kama Mungu hatakufanikisha.


Shida kubwa ni kwamba wakristo wengi wamefikiria mafanikio ni aoutomatic yaani yatajijia tu maadamu uaminifu kwa Mungu atauzingatia. Mbona ingekuwa hivyo watu wangekimbilia wokovu maana wokovu ungelikuwa ni kichaka cha kuficha wavivu na wazembe wasiozingatia kanuni za kufuata na kusababisha mambo kutokea.


Lakini pia ni mbaya zaidi ukifanikiwa pasipo kuwa na uaminifu kwa Mungu au kwa lugha nyingine wewe ukajibidisha kufuata kanuni zote za kiuchumi kukufikisha kwenye mafanikio na huku ukiwa huna mahusiano mazuri na Mungu. Utaishi na ‘mafanikio’ lakini utakuwa huna furaha, si ajabu kama umeoa hata ndoa yumkini itakuwa kwenye matatizo na mambo kadha wa kadha maana shetani itakuwa rahisi kufanya makao kwako na kukuletea kadhia mbalimbali kama ilivyo kawaida yake. Mungu atusaidie.


Utaona kwa hakika ya kuwa, kuegemea sehemu moja na kuacha nyingine ni shida. Lazima mambo yabalance yaani kuwa mwaminifu kwa Mungu na vivyo hivyo mwaminifu kwa utekelezaji wa yale yakupasayo kuyafanya na ndipo utaona uzuri wa kumjua Mungu.



.

Acha kwa leo niishie hapa tutaendeleza somo hili katika Makala ijayo. Usikose kunifuatilia katika Makala zinazofuata.

Karakana ya ubongo tunatengeneza ubongo wako

Kwa wasioijua karakana ya ubongo ni watu waliojikusanya pamoja katika kundi la watsapp kwa lengo la kuondoa takataka kwenye ufahamu na kuanza kujifunza pamoja na kukutana angalau mara moja kwa mwezi ili kuwa chachu ndani na nje ya nchi.

Ili kujiunga yakupasa kuwasiliana nami ili kuweza kukufanyia udahili kama unavigezo vya kuwa mmoja wa wanakarakana ya ubongo.

Na kwa sasa tuna kitabu maarufu kiitwacho ‘KOPE ZAKO BAHARI YAKO’ na kama wewe ni mmoja ya wanaojipenda hiki kitabu si cha kukosa. Tuwasiliane na kuona jinsi ya kukipata.


Seth Simon Mwakitalu

Senior Auditor, Entrepreneurship Consultant, Coach and Lifestyle Trainer.

Tel:- +255 754 441325; +255 788 493836

Email: ssmwakitalu2013@gmail.com

Websites:www.karakanayaubongo.blogspot.com;

Instagram: karakana_ya_ubongo

Facebook: https://www.facebook.com/karakana-YA-Ubongo-109000130642880/?referr=whatsapp

You tube: karakanayaubongo

                

We empower people:-

1. Achieve life and Career goals through part-time business venture.

2. Acquire life changing business skills.

3. Prepare for retirement.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Akili Hisia (emotional intelligence).

Lea mtizamo wa kisayansi, akili hisia ni ule uwezo wa mtu kuweza kutawala anachokiona kwenye mazingira aliyomo. Hii inaamanisha kwamba aweze kutawala mazingira kwa kutumia akili ya hisia zake na wale waliomzunguka. Mtu atawezaje kuelewa kwa kutumia hisia, ishara zinazoonekana kwenye mahusiano mbalimbali bila kuambiwa sentensi au hata neno moja? Utawezaje kutawala hisia zako na za watu wengine katika mazingira uliyomo? Kuna hatua sita za kuchukua ili akili hisia zako zikupe mafanikio unayoyatafuta. #1. Hatua ya kwanza ni wewe mwenyewe kujitambua. Kujitambua ni kitu muhimu kabisa linapokuja suala la akili hisia au emotional intelligence (EQ). Hebu tujiulize ni kwanini? Bila akili hisia hatuna namna yeyote ya kujitathmini kwa vile vipaji ama tulivyo navyo, tusivyo navyo au tunavyohitaji kujifunza ili tuweze kufanikiwa katika mambo yetu mbalimbali. Utaishia kuwa kama kipofu, maana hutaona chochote katika mazingira yaliyokuzunguka. Utapata shida kubwa kutumia mikono isiyoonekana. Aki...

Timiza Malengo Yako na Joel Nanauka.

Ninamshukuru Mungu sana kuweza kuwa na waandishi mashuhuri wa kitanzania ambao wanaweza andika vitabu kwa lugha ya Kiswahili na kusaidia watanzania wengi zaidi. Kitabu cha Timiza Malengo ni kitabu cha aina yake na kamwe si cha kukosekana kwenye maktaba yako. Kama kuna kitu familia yako inabidi ikushukuru basi ni hichi kitabu. Mimi ni msomaji sana wa vitabu na niseme tu ukweli kitabu hichi ni hazina tosha na hakikisha unapata nakala yako. Wahenga walisema tusiandikie wino wakati mate yapo. Nilichokifanya ni kukupatia sehemu ya hichi kitabu kutoka ukurasa wa 29 hadi 40 neno kwa neon ujisomee na useme mwenyewe je uko tayari kukikosa hichi kitabu? Tafadhali fuatana name nikinukuu kitabu cha Joel Nanauka kwa idhini yake kama ifuatavyo:- NJIA MBILI ZA KUTAMBUA KUSUDI LA MAISHA YAKO: Siku moja wakati Tiger Woods anahojiwa na mtangazaji akamwabia ‘’It seems like you like golf so much’’ (Inaonekana kuwa unaipenda gofu sana).Tiger Woods akamjibu, ‘’Not only I like golf but I am golf,’’ a...

CONSCIOUS NA SUB-CONCIOUS MIND

Wazo La Leo Hongera sana mwanakarakana ya ubongo kwa siku hii nyingine nzuri sana ya leo. Ni nafasi bora na ya kipekee sana kwetu kwenda kuweka juhudi kubwa ili kuweza kupata matokeo bora sana. Leo nimeona vyema nizungumzie maana ya maneno ambayo tumekuwa tukiyasikia mara kwa mara. Conscious na Subconscious. Kwanza unatakiwa uelewe "sub" maana yake nn, hii ni prefix...ikiwa na maana ya "below" something, sio negative or opposite that something. Kwa hiyo maana ya "conscious mind" ni kujitambua na subconscious mind means: internal sense of being ambayo consious mind haiwezi decipher, i mean kukupa maono halisi, wakristo wanaita nafsi, mfano mzuri wa activities za subconscious mind ni ndoto Conscious mind-ni kutumia akili wakati tendo fulani linafanyika. Hii inatokea pale mtu anapokuwa hana uzoefu wakati anafanya jambo/tendo fulani, kutokana na kutokuwa na uzoefu inabidi atumie uzingativu wakati wa kutekeleza jambo/tendo husika. kwa mfano mtu anayej...