Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SOMO JUU YA FEDHA/SHEKELI (SEHEMU YA 27)


Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 27

Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku.

Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli
Leo tunakwenda kujifunza juu ya kwa nini uko jinsi ulivyo.

Kwa nini uko njinsi ulivyo – Kuna mambo unatakiwa kuyajua ambayo yanachangia sana kukutengeneza na kuonekana jinsi ulivyo. Leo tunakwenda kuangalia jambo la nne linalomtengeneza mtu:-

NANI RAFIKI YAKO/MAHUSIANO – Siku moja mkulima alikuwa mlimani na akabahatika kuyaona mayai ya tai na kubahatika kuchukua yai moja. Lengo alitaka kuona akichanganya na mayai ya kuku yakaatamiwa pamoja, je mwisho wa siku itakuwaje.
Ukweli ni kwamba mwisho wa siku kuku alitotoa mayai yote ikiwa ni pamoja na yai la tai. Hivyo vifaranga vya kuku na tai vikawa vikilelewa pamoja. Tai huyo mdogo
1. Aliishi sehemu ile ile vifaranga vingine vilpoishi
2. Naye alifanya kama vifaranga vya kuku vifanyavyo
3. Naye aliogopa kama vifaranga vya kuku vilivyoogopa
4. Alikula vile vifaranga vya kuku vilivyokula
5. Alifanya au alikuwa na tabia kama za vifaranga vya kuku
6. Alipata mateso yale yale yaliyowasibu vifaranga wa kuku
Kadri kimo kilivyoongezeka alianza kuona tofauti kati yake na vifaranga vya kuku.Siku moja alisikia kilio cha tai jike na ghafla kuna kitu toka ndani kikainuka kwa lugha nyingine niseme machale yalimcheza kayatanua mabawa yake, akaanza kupaa na akashangaa akienda mbali zaidi kuliko uwezo wa ‘wenzake’.
Nataka tujifunze kitu kimoja hapa. Huyu tai toka siku ya kwanza uwezo  wa kupaa kuliko kuku ulikuwa ndani yake, lakini kule kuendelea kuhusiana na vifaranga vya kuku vilimfanya asione huo uwezekano ambao alikuwa nao ni mpaka siku ya siku ilipotokea na mengine yakabaki kuwa historia.
Mahusiano yako yamekuweka sehemu usiyostahili na kupotosha hatima yako katika maisha. Ni kujidanganya ya kuwa waweza kuwa na mahusiano maovu na kutegemea mwisho mwema. Nioneshe rafiki yako, nami nitakuelezea ulivyo, kama msemo usemavyo ndege watembeao pamoja huruka pamoja.
‘Kamwe huwezi kulala kwenye mapaja ya Delila na uamkie kwenye mabega ya Abraham.’
1 Wakorintho 15:33

Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema.

Huwezi kubishana na ukweli mahusiano yako huaribu akili na hatimaye hatima ya maisha yako. Kuwa na busara na jichagulie marafiki kwa uangalifu si kila mtu wa kuhusiana naye.

USIRUHUSU MAHUSIANO YAKO YAKUHARIBIE HATIMA YAKO YA MAISHA.


Acha kwa leo niishie hapa tutaendeleza somo hili katika Makala ijayo. Usikose kunifuatilia katika Makala zinazofuata.
Karakana ya ubongo tunatengeneza ubongo wako
Kwa wasioijua karakana ya ubongo ni watu waliojikusanya pamoja katika kundi la watsapp kwa lengo la kuondoa takataka kwenye ufahamu na kuanza kujifunza pamoja na kukutana angalau mara moja kwa mwezi ili kuwa chachu ndani na nje ya nchi.
Ili kujiunga yakupasa kuwasiliana nami ili kuweza kukufanyia udahili kama unavigezo vya kuwa mmoja wa wanakarakana ya ubongo.
Na kwa sasa tuna kitabu maarufu kiitwacho ‘KOPE ZAKO BAHARI YAKO’ na kama wewe ni mmoja ya wanaojipenda hiki kitabu si cha kukosa. Tuwasiliane na kuona jinsi ya kukipata.

Seth Simon Mwakitalu
Senior Auditor, Entrepreneurship Consultant, Coach and Lifestyle Trainer.
Tel:- +255 754 441325; +255 788 493836
Email: ssmwakitalu2013@gmail.com
Websites:www.karakanayaubongo.blogspot.com;
Instagram: karakana_ya_ubongo
Facebook: https://www.facebook.com/karakana-YA-Ubongo-109000130642880/?referr=whatsapp
You tube: karakanayaubongo
               
We empower people:-
1. Achieve life and Career goals through part-time business venture.
2. Acquire life changing business skills.
3. Prepare for retirement.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Akili Hisia (emotional intelligence).

Lea mtizamo wa kisayansi, akili hisia ni ule uwezo wa mtu kuweza kutawala anachokiona kwenye mazingira aliyomo. Hii inaamanisha kwamba aweze kutawala mazingira kwa kutumia akili ya hisia zake na wale waliomzunguka. Mtu atawezaje kuelewa kwa kutumia hisia, ishara zinazoonekana kwenye mahusiano mbalimbali bila kuambiwa sentensi au hata neno moja? Utawezaje kutawala hisia zako na za watu wengine katika mazingira uliyomo? Kuna hatua sita za kuchukua ili akili hisia zako zikupe mafanikio unayoyatafuta. #1. Hatua ya kwanza ni wewe mwenyewe kujitambua. Kujitambua ni kitu muhimu kabisa linapokuja suala la akili hisia au emotional intelligence (EQ). Hebu tujiulize ni kwanini? Bila akili hisia hatuna namna yeyote ya kujitathmini kwa vile vipaji ama tulivyo navyo, tusivyo navyo au tunavyohitaji kujifunza ili tuweze kufanikiwa katika mambo yetu mbalimbali. Utaishia kuwa kama kipofu, maana hutaona chochote katika mazingira yaliyokuzunguka. Utapata shida kubwa kutumia mikono isiyoonekana. Aki...

Timiza Malengo Yako na Joel Nanauka.

Ninamshukuru Mungu sana kuweza kuwa na waandishi mashuhuri wa kitanzania ambao wanaweza andika vitabu kwa lugha ya Kiswahili na kusaidia watanzania wengi zaidi. Kitabu cha Timiza Malengo ni kitabu cha aina yake na kamwe si cha kukosekana kwenye maktaba yako. Kama kuna kitu familia yako inabidi ikushukuru basi ni hichi kitabu. Mimi ni msomaji sana wa vitabu na niseme tu ukweli kitabu hichi ni hazina tosha na hakikisha unapata nakala yako. Wahenga walisema tusiandikie wino wakati mate yapo. Nilichokifanya ni kukupatia sehemu ya hichi kitabu kutoka ukurasa wa 29 hadi 40 neno kwa neon ujisomee na useme mwenyewe je uko tayari kukikosa hichi kitabu? Tafadhali fuatana name nikinukuu kitabu cha Joel Nanauka kwa idhini yake kama ifuatavyo:- NJIA MBILI ZA KUTAMBUA KUSUDI LA MAISHA YAKO: Siku moja wakati Tiger Woods anahojiwa na mtangazaji akamwabia ‘’It seems like you like golf so much’’ (Inaonekana kuwa unaipenda gofu sana).Tiger Woods akamjibu, ‘’Not only I like golf but I am golf,’’ a...

CONSCIOUS NA SUB-CONCIOUS MIND

Wazo La Leo Hongera sana mwanakarakana ya ubongo kwa siku hii nyingine nzuri sana ya leo. Ni nafasi bora na ya kipekee sana kwetu kwenda kuweka juhudi kubwa ili kuweza kupata matokeo bora sana. Leo nimeona vyema nizungumzie maana ya maneno ambayo tumekuwa tukiyasikia mara kwa mara. Conscious na Subconscious. Kwanza unatakiwa uelewe "sub" maana yake nn, hii ni prefix...ikiwa na maana ya "below" something, sio negative or opposite that something. Kwa hiyo maana ya "conscious mind" ni kujitambua na subconscious mind means: internal sense of being ambayo consious mind haiwezi decipher, i mean kukupa maono halisi, wakristo wanaita nafsi, mfano mzuri wa activities za subconscious mind ni ndoto Conscious mind-ni kutumia akili wakati tendo fulani linafanyika. Hii inatokea pale mtu anapokuwa hana uzoefu wakati anafanya jambo/tendo fulani, kutokana na kutokuwa na uzoefu inabidi atumie uzingativu wakati wa kutekeleza jambo/tendo husika. kwa mfano mtu anayej...