Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba, 2018

MAWAZO HUBADILI MAISHA

Wazo La Leo Hongera sana mwanakarakana ya ubongo kwa siku hii nyingine nzuri sana ya leo. Ni nafasi bora na ya kipekee sana kwetu kwenda kuweka juhudi kubwa ili kuweza kupata matokeo bora sana. Majengo, biashara kubwa, viwanja vizuri vya mpira na mengine mengi ambayo wengine huita maajabu ya dunia ni matokeo ya mawazo. Ninachotaka kusema ni kwamba kila mtu ana mafazo ambayo akiyafanyia kazi maisha hayatakuwa kama yalivyo sasa. Mtihani mkubwa ni jinsi ya kuyapata mawazo yako ambayo yako ndani yako mithili ya madini. Wote tunatambua madini si rahisi kuyapata ni mpaka nguvu ya ziada itumike maana hukaa chini sana na mengi ya madidini kama sio yote yako chini ya miamba. Watu hulazimika kununua mitambo ili tu waweze kufikia madini. Kifupi si lelemama. Vivyo hivyo kwa mwanadamu ili kukutana na mawazo kuntu yaliyomo ndani yake, ni lazima afanye kazi ya ziada. Yawezekana umejaribu mawazo mengi kufanyia kazi lakini mambo bado hayajabadilika. Hii haimaanishi ya kuwa wewe huna m...

UMEFANYA NINI KATIKA MAISHA YAKO?

Wazo La Leo: Habari ya   leo rafiki na msomaji wa mtiririko wa Makala za kila siku zijulikanazo kama wazo la leo. Leo nataka niongelee kidogo juu ya: Umefanya nini katika maisha yako? Swali laweza mfikirisha sana mtu, lakini kifupi toka uzaliwe umefanya nini ili hata uweze sema angalau nimefanya jambo/kitu ambacho ninaweza sema hakika sijutii kuzaliwa kwangu. Wengi ni tatizo maana hadi muda huu ujumbe huu unawafanya wajishangae maana wakiangalia nyuma hawaoni kabisa kitu/jambo lenye tija ambalo limefanyika. Leo hebu nianze kukuambia rafiki yangu, Sehemu ya kwanza ambayo imesababisha tushindwe kufanya mambo yenye maana ni kule kusjishughulisha na shughuli tusizo zipenda. Umewahi sikia watu wakishangilia siku ya Ijumaa inapofika. Wengi utasikia asante Mungu ni Ijumaa leo. Usemi huu hubeba ujumbe mkubwa sana ya kwamba sasa nakwenda kuisahau hii shughuli na kupumzika. Watu wa jinsi hii wako lukuki. Ukisikia maneno yatokayo vinywani mwao ni kulaani viongozi, kulaani utaratib...

UPINZANI ULIOPO KATI YA UBONGO NA MOYO

Wazo La Leo Habari ya   leo rafiki na msomaji wa mtiririko wa Makala za kila siku zijulikanazo kama wazo la leo. Leo nataka niongelee kidogo juu ya upinzani uliopo kati ya ubongo  na moyo. Ninapoanza kuelezea naomba nikuulize kitu kitogo: Je unajua kwa uhakika wewe una kitu kisicho cha kawaida ndani yako kiwezacho kubadili kabisa maisha yako na mengine yakawa stori? Kama hujui naomba nikuambie ya kwamba maisha unayoishi sasa mfanano wake ni tone ndani ya bahari.  Huna haja ya kuwa tone kwani wewe ni bahari. Sababu moja kubwa inayokufanya ushindwe kuishi kwa viwango vya juu ambapo ni haki yako ni ukinzani uliopo kati ya moyo na ubongo. Unaweza kuona jambo linafanywa na mtu na ukajisemea  moyoni ya kuwa nami naweza kufanya lile afanyalo yule (MOYO). Ghafla unaanza kujiongelesha hivi nitawezaje (UBONGO)? Yaani unaanza angalia uwezakano wa wewe kufanya na ukiendelea kutafakari unajiambia siwezi. Sasa ubongo       umesema huwezi lakini na unakuu...

NGUVU NA MUDA WAKO UNAUWEKEZA WAPI?

Wazo La Leo Karibu tena msomaji wa Makala Naamini umewahi kujiuliza na kama bado basi endelea kufuatana nami juu ya  mada yetu ya leo isemayo Nguvu na muda unauwekeza wapi? Kimsingi kila mmoja wetu kwa namna moja au nyingine kuna mahali anawekeza muda na nguvu zake. Nini namaanisha nini nisemapo kuwekeza muda na nguvu? Kimsingi chochote ufanyacho lazima utumie muda na nguvu pia. Hii ndio naita kuwekeza. Hebu niachane na sehemu ambayo wewe huwekeza muda na nguvu zako, nami nijikite kwenye uwekezaji wenye tija. Kujiendeleza Kama kuna kitu ambacho mwanadamu amefumbwa basi ni eneo la kujiendeleza (Pesornal Development). Hivi umewahi kujiuliza ni kwa nini umekuwa hupigi hatua? Au kwa nini umekuwa mtu wa uhitaji kila mara na kuzungukwa na madeni mpaka umegeuka kituko utazani unafanya maagizo barabarani maana  kwa jinsi ugeukavyo mara umuonapo mdeni wako Joti atasubiri sana. Wewe tunayekuona siye wewe. Wewe mwenyewe yuko ndani yako. Maana yake mko wawili wewe wan ...