Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Februari, 2018

Siri ya Maisha ni nini?

Siri ya mafanikio inaishi wapi? Wewe unajitambua? Muda wako wa kujiweka huru umefika. Ninakuweka huru kuanzia sasa. Je, uko tayari? Anza na maswali haya: 1) Huwa unalisha tumbo lako kila siku? 2) Huwa unalisha ubongo wako kila siku? 3) Huwa unalisha moyo wako kila siku? Ninakuweka huru kwa kukulipa sarafu yenye pande tatu kwa majina yake ni: #1. Jana yako #2. Kesho yako #3. Sasa yako Mwendo wa jaribio (experiment) Kwanza. Leo ni leo. Anza kutembea kuelekea kwenye mafanikio yako. Unaijua njia? Anza kutembea kwa miguu yako miwili. Kama huna miguu na uanze kufanya kile unachoweza utoke hapo ulipo hadi sehemu nyingine. Tembea kama vile maisha yako yote yanategemeana na kutembea huko. Kiuhalisia kutembea kwako ndo muujiza wa kujiweka huru. Unashangaa? Ni hivi: Miili yetu inashibishwa sumu kibao kwa hewa tunayopumua na vyakula tunavyokula. Hewa ina Carbon dioxide kutoka kwenye moshi wa magari (pollution) na viwanda. Vyakula vina dawa za mimea(pesticides). Itapendeza k...

Unaulisha nini mwili wako?

Unakula chipsi na soda kila siku? Umeacha kula mboga za majani? Tabia zako zikoje linapokuja suala la lishe? Acha kula Msosi usio na virutubisho. Unaulisha nini ubongo wako? Hili ndo suala nyeti kuliko lishe. Acha kusoma magazeti ya udaku! Acha kutumia Dopamine zako vibaya. Unaweza kusema wajinga wapumbavu huliwa na wajinga werevu. Ukiangalia magazeti ya udaku yakishapambwa na picha na vichwa vya habari vya mambo ya udaku, basi kila mtu atakimbilia kulinunua. Cha kufurahisha zaidi mara nyingi tunachoambulia ni kuangalia picha na umbeya usio na maana yoyote. Hata msomaji haongezeki thamani hata kidogo. Tunatumia muda mwingi kusoma magazeti kwa sababu tunataka kujuzwa mambo. Je, ni lazima tujizwe kila aina ya uchafu kama dodoki? Ni lazima tuwe zoa zoa kama dodoki? Tunapojuzwa vitu visivyo na maana ni kwa faida ya nani? Huo muda tunaopoteza nani anatulipa? Vitu vingi vinavyoandikwa kwenye magazeti ya udaku havidumu. Ukizingatia jinsi ambavyo teknologia imerahisisha mawasil...

Akili Hisia (emotional intelligence).

Lea mtizamo wa kisayansi, akili hisia ni ule uwezo wa mtu kuweza kutawala anachokiona kwenye mazingira aliyomo. Hii inaamanisha kwamba aweze kutawala mazingira kwa kutumia akili ya hisia zake na wale waliomzunguka. Mtu atawezaje kuelewa kwa kutumia hisia, ishara zinazoonekana kwenye mahusiano mbalimbali bila kuambiwa sentensi au hata neno moja? Utawezaje kutawala hisia zako na za watu wengine katika mazingira uliyomo? Kuna hatua sita za kuchukua ili akili hisia zako zikupe mafanikio unayoyatafuta. #1. Hatua ya kwanza ni wewe mwenyewe kujitambua. Kujitambua ni kitu muhimu kabisa linapokuja suala la akili hisia au emotional intelligence (EQ). Hebu tujiulize ni kwanini? Bila akili hisia hatuna namna yeyote ya kujitathmini kwa vile vipaji ama tulivyo navyo, tusivyo navyo au tunavyohitaji kujifunza ili tuweze kufanikiwa katika mambo yetu mbalimbali. Utaishia kuwa kama kipofu, maana hutaona chochote katika mazingira yaliyokuzunguka. Utapata shida kubwa kutumia mikono isiyoonekana. Aki...

Utaambulia Nini? Kwa Lugha Ya Wenzetu Ni "What's In It For Me?" Inaendelea...

Akili Hisia (emotional intelligence). Lea mtizamo wa kisayansi, akili hisia ni ule uwezo wa mtu kuweza kutawala anachokiona kwenye mazingira aliyomo. Hi inaamanisha kwamba aweze kutawala mazingira kwa kutumia akili ya hisia zake na wale waliomzunguka. Mtu atawezaje kuelewa kwa kutumia hisia, ishara zinazoonekana kwenye mahusiano mbalimbali bila kuambiwa sentensi au hata neno moja? Utawezaje kutawala hisia zako na za watu wengine katika mazingira uliyomo? Hii ni sehemu ya pili kuhusu akili hisia jinsi ya kutawala mazingira ya nje kwa kutumia akili hisia kupitia watu wengine. #4. Hatua ya nne ni Uelewa. Kushawishi watu wengine waweze kutupatia tunachohitaji au watufanyie kile tunachotaka ni kazi kubwa sana. Ni lazima tuwe na uelewa mpana ambao ni sehemu ya akili hisia. Kile kitendo cha kuwa na uwezo wa kumwelewa mtu mwingine katika mazingira ya Dunia ya hisia na kuwachukulia walivyo bila mfarakano ni kazi ya kipekee. Kwa nini iwe ni kazi ya kipekee? Kwa sababu lazima utumie miza...

Utaambulia Nini? Kwa Lugha Ya Wenzetu Ni "What's In It For Me?

Unaishi karne ipi? Uko karne ya 19 au karne ya 21? Muda wa kujitambua ni sasa? Hebu tuambatane kwa pamoja Leo. Sitaki nikuache nyuma. Leo ninakuwa mkali kidogo. Ninataka tuamke. Ninataka tuingie kwenye Bongo zetu tufikirie kwa makini. Hiyo ndiyo kazi yetu hapa Karakana ya Ubongo na Be Ready To Learn. Ubongo ulio nao ndo kifaa au zana pekee yenye nguvu kuliko computer nyingine yoyote ile unayoijua. Ubongo wako ndo unaokuwezesha kufanya mambo yote muhimu katika maisha yako. Mifano iko mingi kama vile: 1) Inawezesha mawasiliano, uumbaji wa vitu kama fikra, kufanya tathmini na kupanga. 2) Pia kuna watu ambao wameweza kujifunza na kugeuza Bongo zao kwa kubadilisha jinsi ambavyo ubongo ulikuwa ukifanya kazi karne ya 19 hadi unavyotakiwa kufanya kazi karne ya 21. Ili uweze kuishi vizuri karne ya 21 ni lazima kutafuta mbinu mpya za kukabiliana na mazingira yanayotuzunguka. Ni lazima uweze kutafuta mtu sahihi ambaye kwa pamoja mtaweza kutengeneza siyo tu familia bali mazingira mapy...

Utaambulia Nini? Kwa Lugha Ya Wenzetu Ni "What's In It For Me?"

Utaambulia Nini? Kwa Lugha Ya Wenzetu Ni "What's In It For Me?" Jinsi ya Kukabiliana na Mihemko ya Hisia za Aina Mbalimbali Mhemko wa hisia ni mabadiliko yanayoweza kumtokea mtu yeyote yule awaye. Kila mtu anayo mihemko ya aina mbalimbali kulingana na mazingira aliyomo na pia watu waliokuzunguka. Kuna muda wa furaha, huzuni na hata kuwa kawaida. Saa nyingine tunajisikia kama vile tuko juu ya kila kitu, baada ya muda tunajikuta tunasononeka au hata kujisikia kila kitu kiko hovyo. Mabadiliko ya mihemko ya hisia ni jambo la kawaida katika maisha yetu ya kila siku. Ila inapotokea mihemko ya hisia inapopitiliza (extreme cases) inaweza kusababisha usumbufu na kusababisha ufanisi wa mtu husika kuwa mbovu. Tafadhali, jisajili kwa ajili ya kupata huduma zetu kwa ufanisi zaidi. 1) Be Ready To Learn - www.bereadytolearn.org 2) Karakana ya Ubongo - www.karakanayaubongo.blogspot.com Kuna ugonjwa unaoitwa marashi ya hisia (bipolar disorder) ambao unasababishwa na mihemko ya hi...