Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Udhoefu Wa Wengine Waweza Kukuokoa Na Majanga

Tunaishi katika dunia ambayo kila mtu na mapito yake na kwa viwango tofauti. Ukweli wa mambo ni huu – Wako watu ambao maisha yao yamebeba maonyo juu ya maisha. Ukipata nafasi kuwasikiliza juu ya yale waliyoyapitia na yaliyowasibu kama matokeo au zawadi ya kufanya waliyofanya; Utakuwa umeonyeka kutothubutu kuyafanya hayo uliyo yasikia na ndio maana wahenga walisema ‘Asiyesikia la mkuu huvunjika guu’. Lakini upande wa pili wa shilingi tunapata mafundisho ya kuzingatia kupitia maisha ya watu. Kitu kimoja cha kushangaza ni kwamba hakuna binadamu asiye na stori ya kukueleza. Kikubwa tu stori yake yaweza kuwa onyo au fundisho, na yote unayahitaji ili uwe na maisha yenye mizania. Udhoefu wa watu waweza okoa maisha yako ya ndoa ambayo inakaribia kuvunjika (divorce). Udhoefu wa watu waweza kukuokoa na kiharusi. Udhoefu wa watu waweza kukuokoa na maisha duni ambayo umeyaishi miaka nenda miaka rudi. Udhoefu wa watu ni madini ya ajabu katika kuboresha maisha na ndio maana mafunzo yako ya pan...

Acha Kuchota Maji Baharini Kwa Kutumia Kijiko.

HERI YA MWAKA MPYA. Jambo moja unalotakiwa kulijua ni kwamba hakuna uhaba wa mafanikio. Hivyo unapopanga kufanikiwa usiwe na mawazo ya uchache. Kanuni nzuri ya kupangilia malengo yako ni kuorodhesha uvitakavyo pasipo kuwazia kwamba pesa ni kikwazo. Jiulize kama pesa isingalikuwa tatizo, je nini unatamani uwe navyo. Hakikisha unaorodhesha matamanio yako yote bila kujali vipaumbele. Kazi yako ni kutiririka tu. Nitafurahi orodha ikifikia angalau 100 au kuzidi lakini isiwe chini ya 100. Ukiona unapata orodha chini ya 100 tafsiri yake wewe ni mvivu wa kufikiri. Yaani ainisha maisha yako uyatakavyo na acha kabisa kuwaza kwamba pesa ni kikwazo. Hii ni hatua muhimu sana na ningefurahi kama kila mmoja wetu angalifanya. Hatua ya pili, anza kupitia kimoja baada ya kingine kwa kuandika tarakimu mbele yake. Yaani mfano umeandika nyumba (3) maana yake unataka uwe na nyumba baada ya miaka mitatu, labda Gari (1) ndani ya mwaka mmoja ( Hapa ni chochote kuanzia mwezi mmoja hadi 12 unaandika 1) na f...

Umuhimu Wa Saa Moja Baada Ya Kuamka Na Saa Moja Kabla Ya Kulala

Duniani tunajifunza kila siku. Na ukikata shauri kujifunza kila siku na kufanyia kazi yale yote unayojifunza maisha yako yatakuwa yakibadilika siku baada ya siku. Unahitaji maamuzi magumu ili kubadilika. Kama kuna jambo mojawapo muhimu unatakiwa kulijua kwa kina basi ni ile saa yako ya kwanza unapokua umeachia kitanda namaanisha asubuhi uamkapo na pia saa yako moja kabla ya kulala. Ukiamka unakimbilia kufanya nini? Utafiti umeonesha ya kwamba wengi tumeathirika na jambo moja kukimbilia simu na kuanza kuangalia watsapp, face book, twitter, Instagram. Tunahitaji kubadili kwani si tabia njema. Saa moja ya kwanza baada ya kuamka kitandani ni ya muhimu sana kujua unaanza na kitu gani cha kwanza ila isiwe simu. Hapa ningefurahi kama kila mmoja angeliniambia akiamka tu anakimbilia kufanya nini? Najua itanichukua muda kupata mawazo mbalimbali lakini naamini kila mmoja anajua anachokimbilia mara aamkapo. Hakuna kanuni ya kipi uanze nacho lakini kutokana na umuhimu wa saa moja ya kwanza ku...

Mambo Ya Kuzingatia Ili Kuwa Na Siku Yenye Tija.

Maisha tunayoishi yanahitaji nidhamu ili kuelekea kwenye mafanikio tunayotarajia. Leo naomba nikushirikishe yafuatayo:- Kila siku unahitajika kupanga malengo unayotarajia kuyakamilisha siku inayofuata. Tendo hili ni vyema likafanyika usiku kabla ya kulala. Nakushauri uwe na noti buku maalum kwa ajili ya kuandika malengo yako ya kila siku. Kuwa mtu wa matokeo na sio maneno – Utakumbuka nimewahi kukusisitiza kabla hujalala orodhesha mambo angalau sita unayotarajia kufanya siku inayofuata. Ninasisitiza tena kuhakikisha unafanya hivyo. Ukisha orodhesha, jiulize swali moja kuu – Kama utalazimika kufanya jambo moja tu kati ya hayo sita, je ni lipi utalipa kipaumbele na mengine ukayaacha. Tafadhali zungushia hilo jambo mara moja. Kitakachofuata ikiwezekana zima simu yako na mara moja anza kukifanya kwa kanuni ya kuwa ukianza hakuna mapumziko mpaka umemaliza ndipo waweza kujipa dk kumi au kumi na tano za kuanza kuandika mawazo (ideas) yatakayoanza kukujia kwenye kinotibuku chako ch...

Unaamini nini?

Mtu akisikia maongezi juu ya Imani haraka kinachokuja akilini ni masuala ya kiimani. Lakini mimi natataka kutabainisha mambo makubwa mawili yaani Imani juu ya Mungu na Imani juu yako wewe mwenyewe. Imani hizi mbili zina umuhimu mkubwa sana katika maisha. Ukweli ni kwamba usipomtanguliza Mungu katika shughuli zako au kama huamini kwamba Mungu yupo basi nisikufiche uko mahali pabaya. Mungu ni nambari moja katika kila shughuli tufanyazo. Mimi naamini hivyo. Nisingependa sana kujikita juu ya Imani juu ya Mungu kwani tu watu wa dini mbalimbali lakii yatosha kusema twawajibika kumtanguliza Mungu katika shughuli zetu. Sasa kikubwa ambacho nitaongelea kwa kina ni Imani iliyojengeka ndani yako tangu kuzaliwa hadi kufikia hapo ulipo. Imani huanza kwa kusikizishwa na kisha kuanza kujijengea mfumo ninaouita mfumo wa kiimani katika maeneo yafuatayo:- Philosofia – mfumo ukuongozao kutenda mambo. Ni vyema ukajua mambo yanayokuongoza katika maisha. Maono – Kimsingi mtu huona kwa kutumia mac...

Jifunze Kanuni/Sheria za Maisha Yalivyo

Tupo duniani tunaishi lakini sijui kama unajua ya kuwa tunaongozwa na kanuni au sheria ambazo kamwe huwezi zibadili. Hivyo ni vyema ukazijua kidogokidogo ili uweze jua jinsi ya kuendana nazo. Utakapotenga muda wako kujifunza sheria za dunia hii utasaidika na mambo makubwa mawili:- Utajilinda na kuumizwa – Kikubwa hapa si kutozipenda sheria za dunia bali muhimu sana ni kupata taarifa za kutosha kuzijua hizo kanuni. Kwa kufanya hivyo utalijilinda na kuumizwa maana ikitokea hivi wajua hii ni kanuni lazima iwe hivi. Lakini ungalikuwa hujui ungeumizwa. Hakuna kitu kibaya kama mtu kuwa mjinga. Lakini upande mwingine ujinga huo ukikupelekea kuwa kapuku inakuwa mbaya Zaidi. Ila utapoteza kabisa maana ya wewe kuishi maisha haya pale itakapotokea ujinga wako umezalisha ukapuku na kupelekea kuwa kitandani ukiwa mgonjwa. Yaani u mjinga, tena kapuku na kama haitoshi u mgonjwa wa kushindwa kuamka kitandani. Unadhani unasubiri nini. Pambana kuondoa ujinga usikufikishe mahali pa kuwa mahututi. ...

Njia Rahisi ya Kuvunja/Kuacha Tabia mbaya

Kuvunja au kuacha tabia mbaya si jambo rahisi. Wanasaikologia na mtaalamu wa kushugurikia watu walioathirika kiasi cha kuwa mateja wa mambo Fulani ndugu Judson Brewer  anasema tabia ni matokeo ya mafuzo yenye kuendana na kuzawadiwa. Tukio kimsingi huleta mafunzo kwenye ubongo kiasi cha kusababisha kuwa na wakati wa ‘kujisikia vizuri’, kama vile ulaji wa vipisi vya keki ya  chokoleti. Kuachana na tabia kama hii ya ulaji wa vipande vya keki vya chokoleti huchukua muda – sanasana hii hutokana  na sababu ambazo kwa kila tabia ambayo hujitokeza kwa mtu huwa kimsingi imepitia mchakato wa hatua tatu kuanzisha, tabia na zawadi. Inatakiwa kuijua tabia kwa kina, uelewa wa kujua nini kinachoendelea kwenye ubongo, ili kuweza kubailika kuwa bora Zaidi. Lakini leo nitaelezea njia rahisi ya namna ya kushughulika na tabia mbaya. Kihistoria, mfumo wa kuzawadiwa kuhusiana na ulaji chakula ni suala la kuweza kuishi yaani kula uendelee kuishi.Brewer yeye anasema kawaida taarifa hupelekw...