Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Siku Moja Utatoweka Katika Uso Wa Dunia

Leo nimeonelea vyema tukumbushane ya kuwa hatupo hapa duniani milele. Sote tu wapitaji na sijui kama umewahi kujiuliza hili swali ya kwamba siku moja utatoweka. Ukilijua hili vizuri hutakuwa na muda wa kupoteza maana kifo hakina taarifa wala kanuni. Hivyo kila siku akupayo Mungu hakikisha unajipangia kufanya vitu kana kwamba kesho hutakuwepo. Hili litakufanya uwaguse watu wengi Zaidi katika uwepo wako duniani. Utalazimika kuishi maisha yenye maana na kuwa mwangalifu kwa mengi ili uache alama utakapokuwa haupo. Napenda msemo anaoutumia Joel Nanauka ya kwamba ulikuja duniani binafsi lakini yakupasa kuondoka ukiwa taasisi akimaanisha taasisi si ya mtu mmoja bali ya wengi. Hivyo kuondoka kwako kuache mazungumzo kwa wengi kwa jinsi ulivoyagusa maisha yao na hapo ndipo unakuwa taasisi na sio tena mtu binafsi. Maisha ni mafupi. Ishi kila siku kwa utimilifu wake (Live full today). Kuwa bora kuliko katika kila jambo ulifanyalo. Kujua utakufa itakujengea kukumbushwa utakapoondoka watak...

Muda na Pesa

MTU ANAYECHEZEA MUDA = MTU ANACHEZEA PESA MTU ANAYECHEZEA PESA = MTU ANACHEZEA HATIMA YAKE KAA MBALI NA MTU HUYU NI SUMU KULIKO KANSA. Jambo la kwanza nitaongelea kuhusiana na utafiti uliofanyika na kuonesha ya kuwa angalau kila familia kuna mtu mmoja ambaye akikujia na kukusomesha lazima utatoa pesa, sijui niwaite matapeli bado nazidi kutafuta lugha nzuri nataabika lakini nisaidie kuwapatia jina sahihi. Ninachojaribu kuelezea hapa ni kwamba kuna watu hapa duniani ni wabunifu wa kutunga stori ili kujipatia pesa. Watu wa jinsi hii usiombe kukutana nao maana ukimpa tu nafasi akajieleza lazima utatoa pesa. Inawezekana kabisa ukajisemea ya kwamba fulani akija kwangu simpi hata senti tano. Kinachoshangaza kwa ubunifu maridhawa walionao utajikuta si tu nunampatia pesa bali pia unamsaidia kumtafutia na kwa wengine wamuongezee. Sijui kama ninachongea umekutana nacho  maishani au unawafahamu watu wa jinsi hiyo katika jamii zetu kama sio kwenye familia zetu. Yawezekana kabis...

Njia Rahisi ya Kuvunja/Kuacha Tabia mbaya Kuvunja au kuacha tabia mbaya si jambo rahisi.

Wanasaikologia na mtaalamu wa kushugurikia watu walioathirika kiasi cha kuwa mateja wa mambo Fulani ndugu Judson Brewer anasema tabia ni matokeo ya mafuzo yenye kuendana na kuzawadiwa. Tukio kimsingi huleta mafunzo kwenye ubongo kiasi cha kusababisha kuwa na wakati wa ‘kujisikia vizuri’, kama vile ulaji wa vipisi vya keki ya chokoleti. Kuachana na tabia kama hii ya ulaji wa vipande vya keki vya chokoleti huchukua muda – sanasana hii hutokana na sababu ambazo kwa kila tabia ambayo hujitokeza kwa mtu huwa kimsingi imepitia mchakato wa hatua tatu kuanzisha, tabia na zawadi. Inatakiwa kuijua tabia kwa kina, uelewa wa kujua nini kinachoendelea kwenye ubongo, ili kuweza kubailika kuwa bora Zaidi. Lakini leo nitaelezea njia rahisi ya namna ya kushughulika na tabia mbaya. Kihistoria, mfumo wa kuzawadiwa kuhusiana na ulaji chakula ni suala la kuweza kuishi yaani kula uendelee kuishi.Brewer yeye anasema kawaida taarifa hupelekwa kwenye ubongo ili kukumbuka sehemu chakula kilipotikana, na mara ...

Umasikini Ni Dhana Iliyojengeka Kwenye Ubongo

Umasikini ni dhana iliyojengeka kwenye ubongo na kamwe usije ukatafsiri ati umasikini ni ukosefu wa vitu vionekanavyo kwa macho kama kutokuwa na gari, nyumba, chakula na kadahalika. Mtu hufikia hatua ya kuwa masikini ni pale yeye mwenyewe anapoamini ya kuwa yeye  ni masikini (Kifupi amepofuka macho na haoni chochote anachoweza kukifanya nikimaanisha japo anaishi tayari ni maiti anangojea kuzikwa tu). Imani hujenga mtiririko wa mawazo na mtiririko wa mawazo husababisha matendo mfanano (paralysed no more actions) na hatimaye hayo matendo humfikisha mtu kituoni anapostahili (kujihalalishia ya kuwa yeye ni masikini) ambapo sasa Imani hukomaa kama zilivyo dini tuziitazo siasa kali yaani mtu haambiliki, aminicho ndicho hupenda kumsikia kila mtu akubaliane nacho vinginevyo wewe unakuwa adui. Zingatia kanuni hii: Imani>Mawazo>Matendo>Kituo>Imani kali>Mawazo>Matendo>Kituo…huenda ikijirudia (Repeat circle). Wewe hauko vile ujifikirivyo, uko hivyo ulivyo kutokana...

Jinsi Gani Mtu Afanikiwe Katika Maisha

Wengi wetu huyatazama mafanikio kana kwamba ni kitu kisichowezekana kukifikia. Tunajifananisha na watu ambao jamii inawatambua ya kuwa wamefanikiwa na kamwe tunashindwa kujipima kujua kipi tufanye kuwafikia. Tunaishia kudhamiria vitu vichache kuliko uwezo tulio nao ambao wengi hawajui kwamba wana huo uwezo ambao kimsingi ni mkubwa mno kiliko tujuavyo. Lakini ukweli ni kwamba mafanikio ni rahisi sana. Na si uchawi. Ili kuweza kufanikiwa katika maisha, unahitaji vitu vikuu viwili: kufanya kitu unachokipenda bila kujali unapata hela au hupati bali furaha yako ni kuendelea kufanya na ajabu itakayo fuata ni pesa kuanza kukufuata na jambo la pili ni unyenyekevu (Kuwa tayari kumwona mtu yeyote ni bora kuliko wewe). Sasa hebu tuongelee maeneo haya mawili ya kihisia. Jinsi gani ufanikiwe katika maisha: Fanya unachopenda Yawezekana kabisa unajishughulisha na kitu ambacho hukipendi ila unajilazimisha kufanya. Sijui umeajiriwa, au una fanya biashara ambayo huipendi ila unajisemea moyoni nikiach...

Si Kasi Ya Saa Bali Kasi Ya Ubongo

Ukijisahau muda unasonga mbele na ukijitathimini unajutia ya kwamba umepoteza muda. Ukweli unabaki pale pale ya kwamba kamwe hutoweza kurudisha muda uliopotea. Upande wa pili wa shilingi ni ubongo wako. Napenda leo utambue ya kwamba si suala la saa tu kwenda kasi na wewe kutofanya kitu bali zaidi sana ubongo wako una kasi ya kuelekea wapi. Kumbuka uwazacho ndicho kinakuelezea wewe. Ubongo wetu unafanya kazi zaidi ya komputa. Ninachojaribu kukielezea hapa ni kwamba tunahitajika kuzitumia bongo zetu zaidi ya kuangalia saa inavyo zidi songa mbele. Ubongo wetu una macho na uchaguzi unao wewe kuangalia kwa kutumia macho ya kawaida au kuangalia kwa kutumia ubongo. Kuna faida nyingi sana utakapojiruhusu kutumia macho ya ubongo kwani utaanza kuchukulia vitu kwa utofauti na wanaokuzunguka. Mfano – Yawezekana unapitia maisha ya kukatishwa tamaa, unajishughulisha sana wala huoni kusonga mbele, unaumizwa na watu wako wa karibu kiasi cha kuzalisha maumivu/uchungu moyoni. Inafika mah...

Umuhimu Wa Saa Moja Baada Ya Kuamka Na Saa Moja Kabla Ya Kulala

Duniani tunajifunza kila siku. Na ukikata shauri kujifunza kila siku na kufanyia kazi yale yote unayojifunza maisha yako yatakuwa yakibadilika siku baada ya siku. Unahitaji maamuzi magumu ili kubadilika. Kama kuna jambo mojawapo muhimu unatakiwa kulijua kwa kina basi ni ile saa yako ya kwanza unapokua umeachia kitanda namaanisha asubuhi uamkapo na pia saa yako moja kabla ya kulala. Ukiamka unakimbilia kufanya nini? Utafiti umeonesha ya kwamba wengi tumeathirika na jambo moja kukimbilia simu na kuanza kuangalia watsapp, face book, twitter, Instagram. Tunahitaji kubadili kwani si tabia njema. Saa moja ya kwanza baada ya kuamka kitandani ni ya muhimu sana kujua unaanza na kitu gani cha kwanza ila isiwe simu. Hapa ningefurahi kama kila mmoja angeliniambia akiamka tu anakimbilia kufanya nini? Najua itanichukua muda kupata mawazo mbalimbali lakini naamini kila mmoja anajua anachokimbilia mara aamkapo. Hakuna kanuni ya kipi uanze nacho lakini kutokana na umuhimu wa saa moja ya kwanza ku...