Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

SOMO JUU YA FEDHA /SHEKELI (SEHEMU YA 33)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 33 Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza umuhimu wa mizania katika mafanikio. Tumejifunza mengi kuhusiana na masuala ya fedha na sasa ni muhimu tukajua umuhimu wa mizania katika mafanikio. Kikubwa ninachotaka kukufahamisha leo ni kuwa mafanikio sahihi ni lazima yawe yametokana na uwekezaji wa kiroho na uwekezaji halisia unaoweza onekana kwa macho ya nyama. Ni ujinga kujikita kwenye mambo ya kiroho 100% ikiwa ni pamoja na utoaji wa fungu la kumi kwa uaminifu ati kwa kuwa imeandikwa utabarikiwa kwa kuwa mwaminifu na kubaki umekaa na kusubiria baraka zimwagike. UTASUBIRI SANA na ndipo utaanza kujiuliza na kuona kama Mungu amekuacha. Hivi unawezaje mfano kuwa mwaminifu wa fungu la kumi na kushindwa kuwa mwaminifu wa kuwekeza 10% kwa uaminifu kama ilivyo kwa fungu la kumi na ukafuata kanuni zote za kufanikisha, na uone kama...
Machapisho ya hivi karibuni

SOMO JUU YA FEDHA /SHEKELI (SEHEMU YA 32)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 32 Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza MAMBO MAKUU MATATU UNAYOTAKIWA KUZINGATIA JUU YA FEDHA. Tumejifunza mengi kuhusiana na masuala ya fedha na sasa ni muhimu tukajua mambo matatu yakayotusaidia kutuweka sawa linapokuja suala la fedha. 1. Elimu juu ya fedha – Itafurahisha kama utaweka kipaumbele kujikumbusha mara kwa mara juu ya hii elimu kwani kurudia rudia imethibitika kuwa ni njia bora kufanya jambo unalorudia kushikamana na ubongo wako wa ndani  (sub-conscious mind) na kusababisha utekelezaji wa jambo husika kuwa rahisi zaidi  kuliko kutorudiarudia. Sote tunahitaji hii elimu na ingewezekana mashuleni pia ifundishwe. 2. Kuipangilia fedha – Tabia ya kupata pesa na kuanza kuitumia ndio imetufikisha hapa tulipo. Mtu yeyote makini akipata tu pesa huipangilia katika mpangilio uliothibitika kuwa bora zaidi 30/70 na waweza ...

SOMO JUU YA FEDHA /SHEKELI (SEHEMU YA 31)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 31 Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza MUNGU HATUPI UTAJIRI BALI HUTUPA NGUVU ZA KUTENGENEZA/KUPATA UTAJIRI. Kumbukumbu la Torati 8:18 Bali utamkumbuka Bwana, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako, kama hivi leo. Acha maombi ya kumuomba Mungu akupe utajiri kwani Yeye hukupa uweza wa kupata utajiri. Sasa suala la kuutumia uwezo ulipewa ni suala lingine. Kinachotokea ni kwamba una uweza ndani yako tayari ambao hautumiki na hiyo ndio maana u masikini. Tatizo hujautumia uweza uliopewa ndani yako. Msingi au sehemu ya kuanzia kuanza kuutumia uweza uliopewa na Mungu ni pale unapofanya agano la kushikamana na Mungu katika maisha yako kwa kuyakabidhi maisha yako kwake ili awe Bwana na Mwokozi wa maisha yako, ndio kitu cha kwanza na muhimu sana na si vinginevyo. Nikijua...

SOMO JUU YA FEDHA/SHEKELI (SEHEMU YA 30)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 30 Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza juu ya kwa nini uko jinsi ulivyo. Kwa nini uko njinsi ulivyo – Kuna mambo unatakiwa kuyajua ambayo yanachangia sana kukutengeneza na kuonekana jinsi ulivyo. Leo tunakwenda kuangalia jambo la saba linalomtengeneza mtu:- ROHO MTAKATIFU – Mkristo katika makuzi yake ya kiroho kuna hatua anapitia zilizo muhimu, hatua ya kwanza ni hatua anayoifikia kuujua ukweli ya kwamba hawezi kumpendeza Mungu pasipo kuukubali mpango wa Mungu wa ukombozi kupitia Yesu Kristo aliye Bwana na Mwokozi wa Maisha yetu. Kila mwanadamu chini ya jua hana budi kutubu dhambi zake na kumpokea Yesu  Kristo kama Bwana na Mwokozi wa maisha binafsi. Baada ya hapo ubatizo wa maji hufuata japo si utaratibu rasmi kwa kuwa mtu aweza kumpokea Yesu Kristo na kubatizwa kwa Roho Mtakatifu kabla ya ubatizo wa maji. Hivyo hatua hii ya ...

SOMO JUU YA FEDHA/SHEKELI (SEHEMU YA 29)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 29 Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza juu ya kwa nini uko jinsi ulivyo. Kwa nini uko njinsi ulivyo – Kuna mambo unatakiwa kuyajua ambayo yanachangia sana kukutengeneza na kuonekana jinsi ulivyo. Leo tunakwenda kuangalia jambo la tano linalomtengeneza mtu:- NENO LA MUNGU – Kama kuna jambo hutengeneza ufahamu basi ni neno la Mungu, Ukilipa nafasi neno la Mungu katika maisha yako basi nalo neno hukupa nafasi stahiki katika nchi uishiyo. 2 Timotheo 2:15 Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari, ukitumia kwa halali neno la kweli. Ushauri kwako msomaji, nakushauri fanya mojawapo au yote yafuatayo ila moja au mbili lazima viwemo kwenye uchaguzi wako:- 1. Hakikisha unaisoma biblia yote ndani ya waka mmoja 2. Soma sura moja ya kitabu cha mithali kila siku 3. Fikia kasi ya kujisome...

SOMO JUU YA FEDHA/SHEKELI (SEHEMU YA 28)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 28 Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza juu ya kwa nini uko jinsi ulivyo. Kwa nini uko njinsi ulivyo – Kuna mambo unatakiwa kuyajua ambayo yanachangia sana kukutengeneza na kuonekana jinsi ulivyo. Leo tunakwenda kuangalia jambo la tano linalomtengeneza mtu:- MAONO – Naona vyema nianze na maana ya maono, neno ambalo ni wingi likitokana na neon kuona. Wengi wanatizama bali hawaoni. Waweza kutana na watu wa jinsi mbili yaani kipofu na asiye kipofu na chakushangaza ni kwamba kipofu aweza kuona akashindwa kutizama kwa ajili ya upofu lakini asiye na upofu akaweza kutizama na kushindwa kuona. Na kama ungaliambiwa chagua moja kati ya kuona na kutizama, basi kuona ni jambo la maana zaidi kuliko kutizama. Ukifumba macho taswira utakazoanza kuziona ndani yako itamaanisha uko kwenye hatua ya kuona na si kutizama. Kifupi kuona ni taswira zipatik...

SOMO JUU YA FEDHA/SHEKELI (SEHEMU YA 27)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 27 Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza juu ya kwa nini uko jinsi ulivyo. Kwa nini uko njinsi ulivyo – Kuna mambo unatakiwa kuyajua ambayo yanachangia sana kukutengeneza na kuonekana jinsi ulivyo. Leo tunakwenda kuangalia jambo la nne linalomtengeneza mtu:- NANI RAFIKI YAKO/MAHUSIANO – Siku moja mkulima alikuwa mlimani na akabahatika kuyaona mayai ya tai na kubahatika kuchukua yai moja. Lengo alitaka kuona akichanganya na mayai ya kuku yakaatamiwa pamoja, je mwisho wa siku itakuwaje. Ukweli ni kwamba mwisho wa siku kuku alitotoa mayai yote ikiwa ni pamoja na yai la tai. Hivyo vifaranga vya kuku na tai vikawa vikilelewa pamoja. Tai huyo mdogo 1. Aliishi sehemu ile ile vifaranga vingine vilpoishi 2. Naye alifanya kama vifaranga vya kuku vifanyavyo 3. Naye aliogopa kama vifaranga vya kuku vilivyoogopa 4. Alikula vile vifaranga ...