Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi, 2020

SOMO JUU YA FEDHA /SHEKELI (SEHEMU YA 22)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 22 Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza juu ya AINA 5 ZA UFAHAMU ULIOTIWA SUMU JUU YA UWEKEZAJI. Makala iliyopita tuliongelea na kumalizia aina ya nne ya sumu juu ya uwekezaji. Leo naanza kuongelea aina ya tano na nikuombe endelea kunifuatilia:- . 5.   Utajiri/Dhana ya  mali/vitu kuwa ndio utajiri Kama unadhani ukijilimbikizia mali ndio utajiri naomba nikupe pole kwani hiyo pekee ni ubinafsi na utakutesa sana. Ninapoongelea mafanikio namaanisha kuacha alama, kugusa maisha ya watu wengine. Huwezi kujiita umefanikiwa kama huna mawazo ya kugusa jamii kwa mahitaji mbalimbali. Huu ndio utajiri wa kweli kufanyika baraka kwa watu wengine. Siri kubwa ya kufanikiwa ni kuelewa kwa kina dhana ya uwekezaji – Hapa msisitizo ni kwamba unawaza chochote upatacho utawezaje kukizidisha na wala si kupanga matumizi. Napenda hapa twende p...

SOMO JUU YA FEDHA /SHEKELI (SEHEMU YA 21)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 21 Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza juu ya AINA 5 ZA UFAHAMU ULIOTIWA SUMU JUU YA UWEKEZAJI. Makala iliyopita tuliongelea na kumalizia aina ya tatu ya sumu juu ya uwekezaji. Leo naanza kuongelea aina ya nne na nikuombe endelea kunifuatilia:- . 4.   Utumishi wa Umma/Dhana ya mshahara Aina ya nne ya sumu ya uwekezaji ni dhana ya utumishi wa uma/mshahara. Wengi wamejikuta katika dimbwi la umasikini kwa sababu maisha yao yote wamekuwa wakiishi kwa kumtegemea boss, mwajiri, au serikali ili kupewa mshahara kwa lengo la kutajirika siku za usoni. Amka acha kulala! • Boss wako si asili ya mafanikio yako bali ni chanzo cha kuhakikisha unatumika kumfanikishia. • Ajira yako vivyo hivyo kamwe haiwezi kukufanikisha labda kama utakuwa kwenye ngazi maalum (executives) bali ajira yako inakuimarisha kuwa mtumwa mstaarabu. Wewe ni kutumi...

SOMO JUU YA FEDHA /SHEKELI (SEHEMU YA 20)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 20 Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza juu ya AINA 5 ZA UFAHAMU ULIOTIWA SUMU JUU YA UWEKEZAJI. Makala iliyopita tuliongelea aina mbili za sumu juu ya uwekezaji. Leo tunaendelea na nikuombe endelea kunifuatilia:- . 3. KUJIHALALISHIA/DHANA YA UMILIKI – Katika kuongelea aina hii ya tatu, Makala iliyopita nilimalizia kwa kusema:- ‘Swali linasema unataka kuwa mzima? Hebu angalia jibu la mgonjwa kwa swali la Bwana Yesu - Yule mgonjwa akamjibu, Bwana, mimi sina mtu wa kunitia birikani, maji yanapotibuliwa; ila wakati ninapokuja mimi, mtu mwingine hushuka mbele yangu. Je swali na jibu vina uhusiano? Kinachoonekana kwa huyu mgonjwa ni kwamba alikwisha jihalalishia ya kuwa kupona kwake asahau kwa hiyo akawa mmiliki wa ugonjwa wake na kwamba haiwezekani yeye kupona. Unaiona hatari ya kujimilikisha inavyotesa watu. Kwa Jina la Yesu naomba usiwe...

SOMO JUU YA FEDHA /SHEKELI (SEHEMU YA 19)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 19 Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza juu ya AINA 5 ZA UFAHAMU ULIOTIWA SUMU JUU YA UWEKEZAJI. Makala iliyopita tuliongelea aina mbili za sumu juu ya uwekezaji. Leo tunaendelea na nikuombe endelea kunifuatilia:- . 3. KUJIHALALISHIA/DHANA YA UMILIKI – Aina hii ya tatu inapaswa kushughulikiwa na kuondokana nayo kabisa. Kujihalalishia au kujiona wewe ndiye mmiliki wa jambo fulani baya imeathiri wengi. Akili ya kujidhania/kujisikia kila wakati ya kuwa wewe ndiye mwenye kustahili kuwa na hali mbaya, kuishi maisha magumu na kujidhania ya kuwa yuko mtu anayekusababishia kuwa na hali uliyonayo na kuomba atoweke duniani ndipo utapata unafuu. Ukweli ni kwamba hakuna mtu awazaye kukufanya ushindwe pasipo wewe mwenyewe kuruhusu, hivyo chochote unachoruhusu kwenye maisha yako ndicho unachopokea. Dalili ya watu wa aina hii ni wale wote wenye kila wa...

SOMO JUU YA FEDHA /SHEKELI (SEHEMU YA 18)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 18 Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza juu ya AINA 5 ZA UFAHAMU ULIOTIWA SUMU JUU YA UWEKEZAJI. . 1. AKILI YA KUHAMAHAMA – Kama kuna kitu cha kushughulikia kuondokana nacho basi ni hii hali ya mtu kutotulia kubaki kutangatanga yaani kutokuwa na jambo au kitu maalum kukifanya bali ni kushika hiki na kukiacha kisha kukimbilia kingine. Watu wenye tabia hii ni vigumu hata kujua wanasali wapi maana hawaachi kuhama hama mara leo huku kesho kule  na inaathiri hata kutulia kituo kimoja cha kazi ni kila wakati kubadili sehemu ya kazi na hata ukifuatilia sababu za kuacha kazi hapa na kwenda pale utakuta hazina mashiko. Kifupi hii ni roho inayomwendesha mtu kumuongoza kutotulia au kuwa na maisha yasiyo mipaka, maisha yasio na mwelekeo au kusuduo. Tabia za watu wa aina hii ni mbili kuu:- i. Hawana mahali maalum – Ni watu wa kutangatanga kut...

SOMO JUU YA FEDHA/SHEKELI (SEHEMU YA 17)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 17 Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza juu ya UKOSEFU WA UFAHAMU JUU YA UWEKEZAJI. Ninaandika hii Makala nikiwa na shukrani nyingi kwa mwenyezi Mungu kwani kwa miaka 59 (Leo niandikapo Makala ni tarehe 02.03.2020)  iliyopita hii siri sikuijua kabisa na nimekuja kuijua nikiwa nimebakiza miezi michache nifikie miaka 60. Ninashukuru kwa sababu nayaona maisha yangu yakiwa na pande mbili, moja ni onyo juu ya yapi  usiyafanye au kuyafuata maana mimi nimeshuhudia madhara hasi ambayo nimeyaishi kwa kuyafanya hayo ambayo leo nasimama kwa ujasiri nikiwaonya wote wanaosoma hii makala wasiyafanye/wasiyafuate. Lakini upande wa pili wa maisha yangu nimebeba mambo mazuri ya wewe kuyafuata  au kuyafanya maana nimeona namna yalivyofanyika baraka si tu kwangu bali kwa familia nzima. Haya nitazidi kusisitiza kuyafuata. Hivyo kwa ujumla ...

SOMO JUU YA FEDHA/SHEKELI (SEHEMU YA 16)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 16 Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza juu ya PESA HAITAFUTWI BALI INATENGENEZEWA NJIA. Maisha ya utafutaji/usakaji pesa umewaacha wengi katika maumivu na wengine kupoteza maisha. Dhana ya fedha ni vyema kuijua kwa undani. Fedha kwa lugha nyepesi ni mtumishi. Najua ninaposema mtumishi tayari umeanza kupata picha ya nini hufanywa na mtumishi. Kwa kawaida mtumishi ni mtu wa kutumwa huko na huku ili kusaidia kufanya mambo yaende inavyotakiwa. Na mtumaji hawezi kumtuma mtu mahali ambapo hakuna uhitaji wa mtu kutumwa. Hivyo kwangu pesa inatambulika kwa jina la mtumishi. Jirani yangu akiwa mgonjwa na hana namna ya kufika hospitali sijiulizi mara mbili kama mtumishi yupo naitisha uber na mtumishi mara moja anachukua nafasi yake na kuhakikisha mgonjwa amefika hospitali na kumfikisha kwa daktari na hatimaye kupewa dawa na kumrudisha nyumba...