Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

SOMO JUU YA FEDHA /SHEKELI (SEHEMU YA 15)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 15 Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza juu ya Laana. Kama ambavyo tumejifunza katika Makala zilizotangulia, umasikini ni roho na pia laana. Hakuna jinsi ya kukwepa kuuelezea umasikini pasipo kuhusisha nyanja ya roho. Ninachotaka ukijue pasi shaka ni kwamba baadhi ya umasikini ni kutokana na laana. ‘Lakini itakuwa usipotaka kuisikiza sauti ya Bwana, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata. Utalaaniwa mjini, utalaaniwa na mashambani. Litalaaniwa kapu lako na chombo chako cha kukandia. Utalaaniwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, maongeo ya ng'ombe wako, na wadogo wa kondoo zako. Utalaaniwa uingiapo, utalaaniwa na utokapo, Bwana atakuletea laana na mashaka, na kukemewa, katika yote utakayotia mkono wako kuyafanya, hata uangam...

SOMO JUU YA FEDHA /SHEKELI (SEHEMU YA 14)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 14 Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza juu ya KUTOTII. Ni nani awezaye kuwa na mtu aliye mwajiri asiye pokea maagizo yote ampayo, asiye tii taratibu zote mahali pa kazi, anayeishi na kufanya apendavyo yeye, na bado ukaendelea ukampandisha cheo katika kampuni yako? Ni nani awezaye kufanya hivyo? Tafakari. Nina mashaka hata wewe unayesoma hii makala kama unaweza fanya hivyo kwa mwajiriwa wako. Kama mfanyakazi asiye tii hawezi kamwe pata kupandishwa cheo; Vipi sasa umtegemee Mungu kukubariki ukiwa humtii? Kutokutii kumewatenga wengi kufikia eneo la mafanikio. Kuna Nyanja mbili za kutotii ambazo zimewagharimu wengi kutofikia mafanikio:- 1. Kutotii amri na maagizo ya Mungu. 2. Kutofuata kanuni na sharia za kukufikisha kwenye mafanikio ‘Kama mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi; bali kama mkikataa na kuasi mtaangamizwa kwa upanga; ...

SOMO JUU YA FEDHA / SHEKELI (SEHEMU YA 13)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 13 https ://www.instagram.com/p/B825rFVplbT/?igshid=2e3wb6kv1jq1 Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza juu ya kujisikia utoshelevu kutokana na mafanikio au kujisikia kutokanako na ujuzi maalum unaokufanya ujione si wa kawaida, kifupi hali hii inajulikana kama kiburi yaani kujivunia ulivyonavyo iwe ni mafanikio au ujuzi wa kipekee miongoni wa jamii inayokuzunguka. Kwa walio wengi huambatana na mabadiliko hata ya jinsi ya kutembea na hata ongea yao huwa ya tofauti. Mungu tusaidie. Nimeshuhudia watu wengi wakiwa hawana kazi za kufanya. Kiburi ni mojawapo ya sababu ya umasikini kwa maisha ya walio wengi. • Watu wenye kiburi hawafundishiki na hukataa kufuata maelekezo ambayo yangeweza kuwaepusha na uharibifu. • Watu wenye kujisikia hufanya kosa moja la msingi hasa pale wanapojiona wao ni bora kuliko na kusababisha hata koti wazivaazo ku...

SOMO JUU YA FEDHA /SHEKELI (SEHEMU YA 12)

karakanayaubongo@gmail.com Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 12 Habari za Leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza vyanzo 7 vya umasikini. Uko msemo usemao ‘Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa’ na sababu ni kutokana na kuyakataa maarifa. Naaamini umewahi sikia ya kuwa maarifa ni nguvu. Kama ilivyo maarifa ni nguvu vivyo hivyo ujinga ni ufu. Watu wengi wangali katika shule ya ujinga na ni sehemu kubwa ya watu wamo kwenye umasikini sababu ya ukosefu wa maarifa.Kimsingi kuna aina 7 za ujinga zenye kusababisha umasikini:- a. Ujinga wa kutojitabua (Wewe ni nani) – Swali hili wengi hadi niandikapo hawajitambui. Wengi wameendelea kuwa masikini kisa tu hawajajua wao ni akina nani. Najua kuna watu wanajiuliza nina maana gani. Chukulia mfano kama samaki asingejitambua ya kuwa yeye ni samaki na kuamua kuishi nchi kavu unadhani nini ingalikuwa matokeo yake kama si kifo tena cha haraka....

SOMO JUU YA FEDHA /SHEKELI (SEHEMU YA 11)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 11 Habari za Leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza ‘UMASIKINI HAUHESHIMU MTU, UMRI, RANGI, CHEO, SEHEMU AISHIYO AU DINI YAKE.’ Nikuombe sasa tusafiri pamoja kwa njia ya kuwazua. Hebu fikiria mtu aliyenunua pasi ya umeme na kuanza kuhangaika kupasia nguo kwa pasi ya umeme pasipo kuiunganisha kwenye switch ili pasi ipate moto na kuweza kupasia nguo; Lakini cha ajabu kuishika tu pasi kazi ya kupasia ikaanza mara moja na huku akiendelea kustaajabu ni kwa nini nguo hazisikii pasi ambayo kwa uhakika ni nzuri kwa muonekano. Jitihada ziliendelea hata kutumia vitufe vya kubadili kiwango cha joto kwenye pasi lakini pasi mafanikio. Baada ya mahangaiko ya kutosha ndipo aliamua kukisoma kijitabu kilichoambatana na hiyo pasi na kugundua ya kuwa kuna hatua muhimu na ndio ya kwanza ilipuuzwa ambayo nikuunganisha plug ya pasi kwenye socket ili kupata moto na ku...

SOMO JUU YA FEDHA /SHEKELI (SEHEMU YA 10)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 10 Habari za Leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza Nyanja za umasikini au kwa lugha nyingine ningeweza kusema vipimo vya umasikini. Umasikini una Nyanja mbalimbali, lakini kuu ni hizi zifuatazo. 1. Umasikini wa kifedha – Hii ni tafsiri ya jumla kwa walio wengi pale mtu anapokuwa na ukame wa fedha. Wengine hupenda kuielezea nyanja hii wakiwaweka watu wote wanaoishi chini ya TZA 2,300 (Dola moja) basi hutafsiriwa ya kuwa ni masikini. 2. Umasikini wa kifikra – Huu ni umasikini wa kimawazo. Hii hutokea pale mtu anakuwa na fedha lakini hana mawazo ya kuzifanya fedha hizo ziendelee kuwa mikononi mwake na hatimaye kujiongezea, kwa kawaida watu wa jinsi hii huishia kupoteza fedha zote wazipatazo. Hakuna umasikini wa kutisha kama utasa wa mawazo na ufahamu juu ya fedha. Mungu atusaidie. 3. Umasikini wa kimahusiano – Kuwa na fedha na wakati huo huo ku...

SOMO JUU YA FEDHA /SHEKELI (SEHEMU YA 09)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 9 Leo tena imekuwa siku ya kutiwa moyo sana kutoka kwa mmoja wa wafuatiliaji wa makala zangu za fedha/shekeli kwani ameweza kuniandikia ushuhuda ambao nimeona vyema nawe uweze kuusoma huenda ukaongeza kitu katika safari hii ya kujifunza. Ushuhuda huu umenifanya niuchukue kama Makala na hapo ndipo namalizia. Endela kunifuatilia katika Makala zangu nitakuwa nikitiririka juu ya elimu ya fedha na lengo nikukufikisha mahala uweze kuzitawala na zisikutawale, na ujue jinsi ya kuzitunza na kuzifanya zijiongeze kila iitwapo leo. NA HUU NDIO USHUHUDA WANGU KATIKA MAKALA ZAKO Habari baba ,na nahisi neno habari haitoshi kuonesha heshima ya salamu kwako ,naomba niwe mwafrika  kabisa ,Kama sio mswahiili , SHIKAMOO BABA ,, Na utaelewa mwishoni maana ya SHIKAMOO yangu kwako. naam nakuandikia ujumbe huu nikiwa mwenye tabasamu kubwa na furaha ,na kadri utakavyosoma ujumbe huu utaelewa chanzo Cha furaha yangu . Nimekuwa  nikikufuatilia Sana mak...