Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

SOMO JUU YA FEDHA /SHEKELI (SEHEMU YA 26)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 26 Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza juu ya kwa nini uko jinsi ulivyo. Kwa nini uko njinsi ulivyo – Kuna mambo unatakiwa kuyajua ambayo yanachangia sana kukutengeneza na kuonekana jinsi ulivyo. Leo tunakwenda kuangalia jambo la tatu linalomtengeneza mtu:- UMEZUNGUKA NCHI YAKO/DUNIA KWA KIWANGO GANI? – Kitendo cha kuzalia, kukulia, kusoma na kisha maisha katika nchi yako bila kuona sehemu nyingine ya dunia ikoje kumembupaza wengi na mbaya zaidi wengine wamezaliwa kijiji X wamesoma kijiji X wameoa kiji X na maisha yote hadi kuzeeka na kufa wangali kijiji X. Niambie mtu wa jinsi hiyo atakuwaje kuchukulia mambo maana ayajuayo ni ndani ya mipaka yake na wala hajui upande mwinge wa dunia mambo yakoje. Watu wa jinsi hii wameishia na maisha yasiyoridhisha na kuwa na mtazamo usiozidi mipaka yao. Mithali 4:7 Bora hekima, basi jipatie heki...

SOMO JUU YA FEDHA/SHEKELI (SEHEMU YA 25)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 25 Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza juu ya kwa nini uko jinsi ulivyo. Kwa nini uko njinsi ulivyo – Kuna mambo unatakiwa kuyajua ambayo yanachangia sana kukutengeneza na kuonekana jinsi ulivyo. Ukiyajua itakurahisishia ujiweke wapi ili uwe kivipi. Napenda kuita vitu vinavyokutengeneza au kukupa sura au mtazamo tunaouona tukuangaliapo na kuweza kukuelezea tukikutofautisha na wengine. Leo tunakwenda kuangalia jambo la pili linalomtengeneza mtu:- MAZINGIRA – Mazingira aishiyo mtu yanamchango mkubwa wa ufahamu wa mtu na maendeleo yake. Mazingira hutengeneza akili ya muhusika. Ukiwa kwenye mazingira yaliyodorora pasi shaka akili nazo zitadorora. Chukulia mfano wa mtoto wa miaka mitano aishie kariakoo na mtoto wa umri huo huo aishie bunyangomale huko Tukuyu. Pamoja na kwamba watoto hawa wana umri ulio sawia lakini ukiwaweka pamoja aishi...

SOMO JUU YA FEDHA /SHEKELI (SEHEMU YA 24)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 24 Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza juu ya kwa nini uko jinsi ulivyo. Kwa nini uko njinsi ulivyo – Kuna mambo unatakiwa kuyajua ambayo yanachangia sana kukutengeneza na kuonekana jinsi ulivyo. Ukiyajua itakurahisishia ujiweke wapi ili uwe kivipi. Napenda kuita vitu vinavyokutengeneza au kukupa sura au mtazamo tunaouona tukuangaliapo na kuweza kukuelezea tukikutofautisha na wengine. Mambo yanayomtengeneza mtu na haya yafuatayo: MALEZI/HISTORIA YA FAMILIA ULIYOKULIA – Wengi wetu tumejikuta matatani kifedha kutokana na mambo tuliyo yachukua kwenye familia na mazingira tuliyokulia  wakati wa malezi yetu au ukuwaji wetu na kuyaishi na kama matokeo tuko jinsi tulivyo na mbaya zaidi tumeendelea kuyakumbatia badala ya kuachana nayo. Mambo mengi hasi na ya kutudhorotesha kifedha tumeyabeba na kuyaamini na kuyaishi. Mifano ni ni mingi,...

SOMO JUU YA FEDHA /SHEKELI (SEHEMU YA 23)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 23 Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza juu ya ufikiri sahihi linapokuja suala la kuitawala fedha/shekel na udhibiti juu ya matumizi na nikuombe endelea kunifuatilia:- . Ufikiri sahihi juu ya fedha:- Ninapoongelea juu ya ufikiri sahihi juu ya fedha ninamaanisha ile hali itakayokupelekea kupata badiliko zuri kimaisha ikiwa ni pamoja na kuidhibiti pesa uipatayo isikupokonyoke na izidi kujiongeza. Hapa natamani upate kunielewa vizuri maana ni ukombozi si kwako tu bali familia na jamii inayokuzunguka. Nitakuwa sikutendei haki nisipokueleza ukweli ya kuwa msingi wa kufanijiwa/kutajirika katika maisha haya tuliyo nayo ni katika KUMJUA YESU KRISTO KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA. KINACHOTAKIWA NI KUYAKABIDHI MAISHA YAKO KWA YESU KRISTO AWE BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YAKO. HILI NI LA MUHIMU NA LA KWANZA NA USIPOLIZINGATIA, MAFUNDISHO YANGU ...

SOMO JUU YA FEDHA /SHEKELI (SEHEMU YA 22)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 22 Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza juu ya AINA 5 ZA UFAHAMU ULIOTIWA SUMU JUU YA UWEKEZAJI. Makala iliyopita tuliongelea na kumalizia aina ya nne ya sumu juu ya uwekezaji. Leo naanza kuongelea aina ya tano na nikuombe endelea kunifuatilia:- . 5.   Utajiri/Dhana ya  mali/vitu kuwa ndio utajiri Kama unadhani ukijilimbikizia mali ndio utajiri naomba nikupe pole kwani hiyo pekee ni ubinafsi na utakutesa sana. Ninapoongelea mafanikio namaanisha kuacha alama, kugusa maisha ya watu wengine. Huwezi kujiita umefanikiwa kama huna mawazo ya kugusa jamii kwa mahitaji mbalimbali. Huu ndio utajiri wa kweli kufanyika baraka kwa watu wengine. Siri kubwa ya kufanikiwa ni kuelewa kwa kina dhana ya uwekezaji – Hapa msisitizo ni kwamba unawaza chochote upatacho utawezaje kukizidisha na wala si kupanga matumizi. Napenda hapa twende p...

SOMO JUU YA FEDHA /SHEKELI (SEHEMU YA 21)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 21 Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza juu ya AINA 5 ZA UFAHAMU ULIOTIWA SUMU JUU YA UWEKEZAJI. Makala iliyopita tuliongelea na kumalizia aina ya tatu ya sumu juu ya uwekezaji. Leo naanza kuongelea aina ya nne na nikuombe endelea kunifuatilia:- . 4.   Utumishi wa Umma/Dhana ya mshahara Aina ya nne ya sumu ya uwekezaji ni dhana ya utumishi wa uma/mshahara. Wengi wamejikuta katika dimbwi la umasikini kwa sababu maisha yao yote wamekuwa wakiishi kwa kumtegemea boss, mwajiri, au serikali ili kupewa mshahara kwa lengo la kutajirika siku za usoni. Amka acha kulala! • Boss wako si asili ya mafanikio yako bali ni chanzo cha kuhakikisha unatumika kumfanikishia. • Ajira yako vivyo hivyo kamwe haiwezi kukufanikisha labda kama utakuwa kwenye ngazi maalum (executives) bali ajira yako inakuimarisha kuwa mtumwa mstaarabu. Wewe ni kutumi...

SOMO JUU YA FEDHA /SHEKELI (SEHEMU YA 20)

Somo Juu Ya Fedha/Shekeli Sehemu Ya 20 Habari za leo mfuatiliaji wangu wa makala zangu za kila siku. Bado tunaendelea na somo letu pendwa juu ya fedha/shekeli Leo tunakwenda kujifunza juu ya AINA 5 ZA UFAHAMU ULIOTIWA SUMU JUU YA UWEKEZAJI. Makala iliyopita tuliongelea aina mbili za sumu juu ya uwekezaji. Leo tunaendelea na nikuombe endelea kunifuatilia:- . 3. KUJIHALALISHIA/DHANA YA UMILIKI – Katika kuongelea aina hii ya tatu, Makala iliyopita nilimalizia kwa kusema:- ‘Swali linasema unataka kuwa mzima? Hebu angalia jibu la mgonjwa kwa swali la Bwana Yesu - Yule mgonjwa akamjibu, Bwana, mimi sina mtu wa kunitia birikani, maji yanapotibuliwa; ila wakati ninapokuja mimi, mtu mwingine hushuka mbele yangu. Je swali na jibu vina uhusiano? Kinachoonekana kwa huyu mgonjwa ni kwamba alikwisha jihalalishia ya kuwa kupona kwake asahau kwa hiyo akawa mmiliki wa ugonjwa wake na kwamba haiwezekani yeye kupona. Unaiona hatari ya kujimilikisha inavyotesa watu. Kwa Jina la Yesu naomba usiwe...