Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Oktoba, 2018

SEMINA YA KIMYA KIMYA

Wazo La Leo Hongera sana mwanakarakana ya ubongo kwa siku hii nyingine nzuri sana ya leo. Ni nafasi bora na ya kipekee sana kwetu kwenda kuweka juhudi kubwa ili kuweza kupata matokeo bora sana. Leo nimeonelea vyema nigusie ushiriki wa semina ya kimya kimya ambayo ni muhimu sana kushiriki kwa kila asomaye Makala hii. Somo hili nimejifunza kwa undani kutoka kwa moja wa mentors wangu Mr. Jim Rohn ambaye kwa sasa ni marehemu japo anaishi. Waweza niuliza kivipi anaishi? Kazi zake zinaendelea kubadilisha maisha ya watu siku hadi siku. Sasa turudi kwenye mada yetu ya semina ya kimya kimya itakayokusaidia kubadili kabisa maisha yako kama unataka. Maana bado uchaguzi ni wako, name kamwe siwezi kukulazimisha zaidi ya kukueleza. Semina ya kimya kimya ni hii: UFUNGUO MKUBWA JUU YA MAISHA YAKO BORA YAJAYO NI WEWE (The MAJOR key to your better future is YOU). Ninakuomba kama una gari, basi chapisha haya maandishi na uyaweke sehemu ambayo utalazimika kuyasoma kila wakati ukiwa kweny...

PATO LAKO KAMWE HALIWEZI KUZIDI UPEO WAKO

Wazo La Leo Hongera sana mwanakarakana ya ubongo kwa siku hii nyingine nzuri sana ya leo. Ni nafasi bora na ya kipekee sana kwetu kwenda kuweka juhudi kubwa ili kuweza kupata matokeo bora sana. Watu wengi hujidanganya kwa kujituma sana ili wafikie mafanikio pasipo kuelewa mafanikio yana namna yake na usipoielewa hiyo namna yake itakuwa sawa na kujenga nyumba hewani (Building a castle in the air) au kutwanga maji kwenye kinu. Ukweli wa mafanikio ni upeo (Personal Development). Una upeo kiasi gani? Au una maarifa kiasi gani kwenye Nyanja zote ambazo unataka kuyaona hayo mafanikio. Mfano Nyanja ya pesa. Una upeo kiasi gani juu ya pesa. Kiwango ulichonacho kinatueleza upeo ulio nao juu ya pesa. Kamwe huweza kuwa na pesa kuzidi upeo wako na huo ndio ukweli. Hakuna njia ya mkato, ongeza upeo juu ya pesa na pesa zitaongezeka. Usipoongezeka upeo, sahau kuongeza pato. Kifupi mafanikio hayatafutwi bali yanavutwa. Ni kama sumaku. Upeo wako utavuta kwa uwiano. Upeo mdogo kila kitu ki...

MAISHA YAKO NI MATOKEO YA UCHAGUZI WAKO

Wazo La Leo Hongera sana mwanakarakana ya ubongo kwa siku hii nyingine nzuri sana ya leo. Ni nafasi bora na ya kipekee sana kwetu kwenda kuweka juhudi kubwa ili kuweza kupata matokeo bora sana. Maisha tuishio ni matokeo ya maamuzi ya kila siku ndiyo yametufikisha hapa tulipo. Je umekuwa unapendelea nini zaidi kati ya kujishughulisha na jambo la kufurahisha na lililo rahisi au jambo la kukufikirisha na gumu. Nimesikia mara nyingi watu wakiambiana njoo ufanye huku nkwani ni rahisi kuliko huko. Naomba utambue vizuri kanuni ya dunia ifanyavyo kazi. Rahisi huwa havidumu na vigumu ndivyo hudumu. Jambo lolote linalokufanya ufikiri linakukuza na kinyume chake linakudumaza. Wakati tukiendelea na mada yetu ya uchaguzi, najaribiwa kukuambia jambo hili:- Kujua jambo litakalo kuletea matokeo mazuri ni jambo moja na kulitenda ni jambo linguine. Ndio maana kuna tuna makundi ya waliofanikiwa na wasiofanikiwa. Kujua kufanikiwa ni kufanya yale wayafanyayo na waliofanikiwa. Na yampa...

FALSAFA(GUIDING PRINCIPLE FOR BEHAVIOUR(ZINAZOWEZA KUONGOZA MAISHA YAKO.

Wazo La Leo Hongera sana mwanakarakana ya ubongo kwa siku hii nyingine nzuri sana ya leo. Ni nafasi bora na ya kipekee sana kwetu kwenda kuweka juhudi kubwa ili kuweza kupata matokeo bora sana. Ninapoanza kuongelea neno falsafa naona vyema nikatoa tafsiri ya hili neno kama ambavyo nimesoma kwenye kamusi. Neno falsafa limetokana na neno la kigiriki na tafsiri sahihi na ambayo ndiyo tutaitumia katika mada yetu ya leo ni kanuni inayolinda tabia au mwenendo. Yaani mwenendo wako au tabia zako ni kutokana na kanuni ongozi na hivyo maisha yako yana kuwa katika namna fulani ya kuishi maana unaongozwa na falsafa ulizozikubali na kuzitumia katika maisha. Wiki zima hii nimekuwa nikisiliza video ya Jim Rohn na kwa hakika nimejifunza falsafa mbali mbali kutoka kwake ambazo ndizo zilibadilisha kabisa maisha yake. Hii inamaanisha ya kuwa hata wewe na mimi tukitumia falsafa hizi zitatusaidia kuboresha maisha yetu. 1.       Falsafa ya 1: FAIDA AIPATAYO MTU KATIKA KUFANYA BIA...

MAISHA NI VITA

Wazo La Leo Hongera sana mwanakarakana ya ubongo kwa siku hii nyingine nzuri sana ya leo. Ni nafasi bora na ya kipekee sana kwetu kwenda kuweka juhudi kubwa ili kuweza kupata matokeo bora sana. Maisha ni vita na hivyo bila ya kuwa na kiongozi aliye jemedari na mbinu wengine huita mikakati basi tegemea kushindwa vita yako. Jemedari wa vita yako kwa bahati nzuri ni wewe mwenyewe. Hivyo yakupasa kujiimarisha. Hebu pata siku ongea na wanajeshi juu ya mazoezi afanyayo askari kabla ya kutambuliwa kuwa afisa (Commissioned) Kimsingi hakuna mtu aitwaye afisa jeshini aliye goigoi na hasa linapokuja suala la vita. Leo nimestuliwa na mhamasishaji na mwalimu wa kimataifa ambaye niandikapo yeye ni marehemu lakini kazi zake zinaishi. Asubuhi nimekuwa nikisikiliza moja ya video zake na ndipo nikakutana na maneno ambayo yamenigeuza sana katika msimamo wa mapambano na maisha yangu. Jim Rohn anasema tena pasi kupapasa macho ‘USINUNUE GARI KABLA YA KUNUNUA NYUMBA YAKO YA PILI AU KABLA HUJA...

UNAFANYA NINI NA PESA YAKO?

Wazo La leo Hongera sana mwanakarakana ya ubongo kwa siku hii nyingine nzuri sana ya leo. Ni nafasi bora na ya kipekee sana kwetu kwenda kuweka juhudi kubwa ili kuweza kupata matokeo bora sana. Kama ilivyo safari ya umbari wa kilometa 10 huanza na hatua ya kwanza. Hivyo kamwe usiidharau hatua ya kwanza kwani ni mwanzo wa mwendo mrefu. Hivyo safari yako ya mwenendo wa pesa huanzia na shilingi moja unayoikamata. Ninachomaanisha hapa kama unatamani uwe mtu wa kumiliki billions of money basi ni muhimu kujua mambo makuu mawili:- 1.       Namna gani waweza kutumia uwezo mkubwa uliko ndani yako au ni kwa namna gani utaanza kuutumia uweza wa ajabu uliko ndani yako kidogokidogo kwa kuongezeka kila siku hadi kufikia hatua ya juu kabisa ya uwezo wako. 2.       Kwa nini utumie rasilimali zako zote.  Rasilimali ambazo twaweza kuongelea leo ni mbili tu, nazo ni MUDA na PESA. Ila mimi kwa siku ya leo nitajikita sana kwenye pesa na hasa pesa uipatayo kama ...

ONGEZA UFANISI

Wazo La Leo: Hongera sana mwanakarakana ya ubongo kwa siku hii nyingine nzuri sana ya leo. Ni nafasi bora na ya kipekee sana kwetu kwenda kuweka juhudi kubwa ili kuweza kupata matokeo bora sana. Moja ya jambo linalofanya wengi wachelewe kufikia mafanikio ni suala zima la ufanisi. Leo nitagusia maeneo machache yatakayokusaidia kuongeza ufanisi wa kila utendacho. 1.       Jua kupangilia vipaumbele vyako. Waweza kuwa na mambo kumi ya kufanya leo. Unachotakiwa kufanya ni kuanza na kile kilicho muhimu yaani ukifanyapo kinakusogeza kwa sehemu kuelekea lengo lako, kisha kinachofuata kwa umuhimu hadi unafikia cha mwisho. Hivyo utafuata mpangilio uliojiwekea hadi siku yako inakwisha. Ukijizoeza kufanya hivi kila siku, utaona mabadiliko katika maisha yako ya utendaji. 2.       Jiambie mara kwa mara ya kwamba kwako msamiati wa kushindwa haupo. Ni kupambana mpaka kieleweke. Maisha si rahisi kivile. Dunia huzawadia majemedari na si walegevu/wachovu/wakata ta...

CONSCIOUS NA SUB-CONCIOUS MIND

Wazo La Leo Hongera sana mwanakarakana ya ubongo kwa siku hii nyingine nzuri sana ya leo. Ni nafasi bora na ya kipekee sana kwetu kwenda kuweka juhudi kubwa ili kuweza kupata matokeo bora sana. Leo nimeona vyema nizungumzie maana ya maneno ambayo tumekuwa tukiyasikia mara kwa mara. Conscious na Subconscious. Kwanza unatakiwa uelewe "sub" maana yake nn, hii ni prefix...ikiwa na maana ya "below" something, sio negative or opposite that something. Kwa hiyo maana ya "conscious mind" ni kujitambua na subconscious mind means: internal sense of being ambayo consious mind haiwezi decipher, i mean kukupa maono halisi, wakristo wanaita nafsi, mfano mzuri wa activities za subconscious mind ni ndoto Conscious mind-ni kutumia akili wakati tendo fulani linafanyika. Hii inatokea pale mtu anapokuwa hana uzoefu wakati anafanya jambo/tendo fulani, kutokana na kutokuwa na uzoefu inabidi atumie uzingativu wakati wa kutekeleza jambo/tendo husika. kwa mfano mtu anayej...

KUTAHAJUDI/MEDITATION

Wazo La Leo Hongera sana mwanakarakana ya ubongo kwa siku hii nyingine nzuri sana ya leo. Ni nafasi bora na ya kipekee sana kwetu kwenda kuweka juhudi kubwa ili kuweza kupata matokeo bora sana. Leo tunakwenda kujifunza juu ya Tahajudi/Meditation. Tafadhali fuatana name. Meditation au taamuli ni kitendo ambacho wengi ambao wamejifunza mambo mengi ya hekima, nguvu ya akili katika maisha ya mwanadamu, sayansi, na Imani mbalimbali, wamekuwa wakivutiwa na kufanya meditation. Mojawapo ya changamoto ya kwanza ambayo wengi wamekuwa wakikutana nayo ni akili kuhama sana kwenye meditation. Kupitia Makala hii, nitajaribu kuelezea njia mbalimbali ambazo unaweza kuzifanya katika kuhakikisha akili inatulia sehemu moja na kuongeza nguvu ya umakini na utambuzi wa hali ya akili yako. Mwanzo Meditation au kwa jina la kiswahi Taamuli ni kitendo cha kutazama hali (nature) ya akili na kuongeza utambuzi na umakini. Wengi wanaofanya meditation ni kwa lengo la kuituliza akili kutoka katika stress...

NJIA ZA KUKUWEZESHA KUPAKUA MAWAZO

Wazo La Leo Hongera sana mwanakarakana ya ubongo kwa siku hii nyingine nzuri sana ya leo. Ni nafasi bora na ya kipekee sana kwetu kwenda kuweka juhudi kubwa ili kuweza kupata matokeo bora sana. Jana niliiishia kwa kusema:- Utaratibu/njia zitakazo kusaidia kupakua mawazo ni hizi zifuatazo:- 1.            Nunua kinoti buku chenye ukubwa wa kuingia kwenye mfuko wa shati na kwa akina dada/mama iwe na uwezo wa kukaa kwenye pochi. Yaani popote ulipo ni lazima uwe na noti buku na peni. 2.            Moja ya njia rahisi sana ya kupakua mawazo inaitwa kwa lugha ya wenzetu ‘PRIME HOUR’ ambayo nikitafsiri Kiswahili ni ‘SAA MOJA MUHIMU’. Hii inamaanisha nini. Katika ratiba yako ya kutwa nzima ambayo wewe unaijua vizuri ina mchanganyiko wa shughuli. Sasa kanuni hii inasema katika hizo shughuli chagua baadhi ya shughuli utakazo zifanya kwa kutumia kanuni hii ya PRIME HOUR. Mfano ratiba yangu ya leo iko hivi: •    ...

ACHA VISINGIZIO

Wazo La Leo: Acha Visingizio Habari za leo mpendwa msomaji wa wazo la leo. Karibu tena kuweza  kufuatana nami katika mtiririko wa Makala mbalimbali nizitoazo kila siku ili kuweza kusaidiana katika safari yetu ya maisha. Leo ningependa kuongelea kwa sehemu juu ya mada niliyoiita ‘ACHA VISINGIZIO’ Imekuwa jambo la kawaida kwa tulio wengi kuacha kuongea ukweli badala yake twakimbilia kutoa visingizio. Leo tutajadili baadhi ya maeneo ili tuone tunavyojidangaya. Hebu fikiria mtu asemaye siku moja nitafanya hiki na kile. Sentensi hii japo haijasema ni kisingizio bali ni kisingizio tosha. Siku moja hiyo iko wapi? Na kwani nini siku hiyo moja. Usidanganyike siku sahihi ni leo. Hebu boresha maisha yako kwa kuchukua hatua. Leo ni siku njema mno kufanya kitu. Acha uzembe na binafsi nachukuia watu wazembe. Inuka katende ulitakalo. Ni vizuri tukajua jinsi ya kupambana na hofu katika maisha zitupelekazo kutoa visingizio. Ufumbuzi sahihi ni kuhakikisha una kitu cha kufanya mbele yak...