Utaambulia nini kwenye Wazo la Leo? Jifunze kutambua vitu muhimu kwenye maisha yako kwanza. Vingine ni vya ziada. Hiyo yaweza kuwa siri ya maisha bora hapa Duniani. Kupokea na Kutoa ni kama watoto mapacha. Siku zote wanaongozana pamoja haswa wanapokuwa wadogo. Leo hii tunaishi kwenye Dunia yenye fursa mbalimbali. Fursa hizo zinatubariki na pia tunazitumia kubadili wengine. Ni sawa na kusema tunapokea na pia kutoa. Haijalishi ni fursa gani iko mbele yako, kama ni kusoma, kazi, kupata mwenza au hata kitu chochote ukipendacho kinachokupatia maarifa kama vile Karakana ya Ubongo, hizo zote ni fursa. Madhalani tunapenda kuishi. Tufikirie pamoja maswali ya kujiuliza ili tufanye majaribio (Experiments). Tusipende sana kukimbilia majibu maana ni njia rahisi zaidi ya kujiua. Haswa jibu linapokuwa siyo lenyewe . Ni vizuri kutambua ya kuwa, hata unapokuwa umeshapata jibu la kwanza, endelea kufikiri ili upate jibu la pili, tatu, nne na kuendelea ili usiwe Mfu. Ipe akili isiyoonekana kazi ya ...