Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Desemba, 2017

Umuhimu Wa Saa Moja Baada Ya Kuamka Na Saa Moja Kabla Ya Kulala

Duniani tunajifunza kila siku. Na ukikata shauri kujifunza kila siku na kufanyia kazi yale yote unayojifunza maisha yako yatakuwa yakibadilika siku baada ya siku. Unahitaji maamuzi magumu ili kubadilika. Kama kuna jambo mojawapo muhimu unatakiwa kulijua kwa kina basi ni ile saa yako ya kwanza unapokua umeachia kitanda namaanisha asubuhi uamkapo na pia saa yako moja kabla ya kulala. Ukiamka unakimbilia kufanya nini? Utafiti umeonesha ya kwamba wengi tumeathirika na jambo moja kukimbilia simu na kuanza kuangalia watsapp, face book, twitter, Instagram. Tunahitaji kubadili kwani si tabia njema. Saa moja ya kwanza baada ya kuamka kitandani ni ya muhimu sana kujua unaanza na kitu gani cha kwanza ila isiwe simu. Hapa ningefurahi kama kila mmoja angeliniambia akiamka tu anakimbilia kufanya nini? Najua itanichukua muda kupata mawazo mbalimbali lakini naamini kila mmoja anajua anachokimbilia mara aamkapo. Hakuna kanuni ya kipi uanze nacho lakini kutokana na umuhimu wa saa moja ya kwanza ku...

Mambo Ya Kuzingatia Ili Kuwa Na Siku Yenye Tija.

Maisha tunayoishi yanahitaji nidhamu ili kuelekea kwenye mafanikio tunayotarajia. Leo naomba nikushirikishe yafuatayo:- Kila siku unahitajika kupanga malengo unayotarajia kuyakamilisha siku inayofuata. Tendo hili ni vyema likafanyika usiku kabla ya kulala. Nakushauri uwe na noti buku maalum kwa ajili ya kuandika malengo yako ya kila siku. Kuwa mtu wa matokeo na sio maneno – Utakumbuka nimewahi kukusisitiza kabla hujalala orodhesha mambo angalau sita unayotarajia kufanya siku inayofuata. Ninasisitiza tena kuhakikisha unafanya hivyo. Ukisha orodhesha, jiulize swali moja kuu – Kama utalazimika kufanya jambo moja tu kati ya hayo sita, je ni lipi utalipa kipaumbele na mengine ukayaacha. Tafadhali zungushia hilo jambo mara moja. Kitakachofuata ikiwezekana zima simu yako na mara moja anza kukifanya kwa kanuni ya kuwa ukianza hakuna mapumziko mpaka umemaliza ndipo waweza kujipa dk kumi au kumi na tano za kuanza kuandika mawazo (ideas) yatakayoanza kukujia kwenye kinotibuku chako ch...

Unaamini nini?

Mtu akisikia maongezi juu ya Imani haraka kinachokuja akilini ni masuala ya kiimani. Lakini mimi natataka kutabainisha mambo makubwa mawili yaani Imani juu ya Mungu na Imani juu yako wewe mwenyewe. Imani hizi mbili zina umuhimu mkubwa sana katika maisha. Ukweli ni kwamba usipomtanguliza Mungu katika shughuli zako au kama huamini kwamba Mungu yupo basi nisikufiche uko mahali pabaya. Mungu ni nambari moja katika kila shughuli tufanyazo. Mimi naamini hivyo. Nisingependa sana kujikita juu ya Imani juu ya Mungu kwani tu watu wa dini mbalimbali lakii yatosha kusema twawajibika kumtanguliza Mungu katika shughuli zetu. Sasa kikubwa ambacho nitaongelea kwa kina ni Imani iliyojengeka ndani yako tangu kuzaliwa hadi kufikia hapo ulipo. Imani huanza kwa kusikizishwa na kisha kuanza kujijengea mfumo ninaouita mfumo wa kiimani katika maeneo yafuatayo:- Philosofia – mfumo ukuongozao kutenda mambo. Ni vyema ukajua mambo yanayokuongoza katika maisha. Maono – Kimsingi mtu huona kwa kutumia mac...

Jifunze Kanuni/Sheria za Maisha Yalivyo

Tupo duniani tunaishi lakini sijui kama unajua ya kuwa tunaongozwa na kanuni au sheria ambazo kamwe huwezi zibadili. Hivyo ni vyema ukazijua kidogokidogo ili uweze jua jinsi ya kuendana nazo. Utakapotenga muda wako kujifunza sheria za dunia hii utasaidika na mambo makubwa mawili:- Utajilinda na kuumizwa – Kikubwa hapa si kutozipenda sheria za dunia bali muhimu sana ni kupata taarifa za kutosha kuzijua hizo kanuni. Kwa kufanya hivyo utalijilinda na kuumizwa maana ikitokea hivi wajua hii ni kanuni lazima iwe hivi. Lakini ungalikuwa hujui ungeumizwa. Hakuna kitu kibaya kama mtu kuwa mjinga. Lakini upande mwingine ujinga huo ukikupelekea kuwa kapuku inakuwa mbaya Zaidi. Ila utapoteza kabisa maana ya wewe kuishi maisha haya pale itakapotokea ujinga wako umezalisha ukapuku na kupelekea kuwa kitandani ukiwa mgonjwa. Yaani u mjinga, tena kapuku na kama haitoshi u mgonjwa wa kushindwa kuamka kitandani. Unadhani unasubiri nini. Pambana kuondoa ujinga usikufikishe mahali pa kuwa mahututi. ...

Njia Rahisi ya Kuvunja/Kuacha Tabia mbaya

Kuvunja au kuacha tabia mbaya si jambo rahisi. Wanasaikologia na mtaalamu wa kushugurikia watu walioathirika kiasi cha kuwa mateja wa mambo Fulani ndugu Judson Brewer  anasema tabia ni matokeo ya mafuzo yenye kuendana na kuzawadiwa. Tukio kimsingi huleta mafunzo kwenye ubongo kiasi cha kusababisha kuwa na wakati wa ‘kujisikia vizuri’, kama vile ulaji wa vipisi vya keki ya  chokoleti. Kuachana na tabia kama hii ya ulaji wa vipande vya keki vya chokoleti huchukua muda – sanasana hii hutokana  na sababu ambazo kwa kila tabia ambayo hujitokeza kwa mtu huwa kimsingi imepitia mchakato wa hatua tatu kuanzisha, tabia na zawadi. Inatakiwa kuijua tabia kwa kina, uelewa wa kujua nini kinachoendelea kwenye ubongo, ili kuweza kubailika kuwa bora Zaidi. Lakini leo nitaelezea njia rahisi ya namna ya kushughulika na tabia mbaya. Kihistoria, mfumo wa kuzawadiwa kuhusiana na ulaji chakula ni suala la kuweza kuishi yaani kula uendelee kuishi.Brewer yeye anasema kawaida taarifa hupelekw...

Jinsi Gani Mtu Afanikiwe Katika Maisha

Wengi wetu huyatazama mafanikio kana kwamba ni kitu kisichowezekana kukifikia. Tunajifananisha na watu ambao jamii inawatambua ya kuwa wamefanikiwa na kamwe tunashindwa kujipima kujua kipi tufanye kuwafikia. Tunaishia kudhamiria vitu vichache kuliko uwezo tulio nao ambao wengi hawajui kwamba wana huo uwezo ambao kimsingi ni mkubwa mno kiliko tujuavyo. Lakini ukweli ni kwamba mafanikio ni rahisi sana. Na si uchawi. Ili kuweza kufanikiwa katika maisha, unahitaji vitu vikuu viwili: kufanya kitu unachokipenda bila kujali unapata hela au hupati bali furaha yako ni kuendelea kufanya na ajabu itakayo fuata ni pesa kuanza kukufuata na jambo la pili ni unyenyekevu (Kuwa tayari kumwona mtu yeyote ni bora kuliko wewe). Sasa hebu tuongelee maeneo haya mawili ya kihisia. Jinsi gani ufanikiwe katika maisha: Fanya unachopenda Yawezekana kabisa unajishughulisha na kitu ambacho hukipendi ila unajilazimisha kufanya. Sijui umeajiriwa, au una fanya biashara ambayo huipendi ila unajisemea moyoni nikiach...

Ukweli kuhusu maisha

Maisha ni neno moja lakini lenye mana nyingi unapoamua kumyambulisha maana yake. Kufikia malengo utakayo kuyafikia nayo ni maisha na hili ni eneo nitakaloliongelea kwa kina siku ya leo. Kutamani uwe vile na hivi ni rahisi sana lakini kuchukua hatua ya kutenda ndilo eneo ambalo wengi hushindwa na kuishia kuona maisha hayana maana yoyote. Wanadamu wanatakiwa kujua ya kwamba kutenda ni muujiza unaojiridhisha kwa watu wenye uthubutu na hili linatuthibitishia kusahau kabisa kutamani kuwa kama fulani bila kuchukua hatua ya utendaji. Kwa kawaida huwa nawashauri watu ya kuwa chochote unachotamani kuwa nacho, tayari wengine wanacho. Kwa hiyo njia rahisi ni kukutana na hao ambao tayari wanavyo ili upate kujua yakupasa kunya nini ili nawe uweze kupata. Hii inamaanisha ya kuwa unakuwa tayari kupitia maumivu yatakayokufikisha unapotamani kufika, au ukaishia hatua ambayo hukuitamani kuifikia kwa kutofanya yale uliyoelekezwa kufanya. Yote kwa yote wewe ndiye mwamuzi. Ni sawa na nadharia ihusishayo...

Pesa - Sehemu ya mwisho

Marafiki waweza kufanya maono yako yapanuke zaidi kwa upande mmoja lakini pia waweza kukuzimisha juu ya maono yako, je wewe uko na lipi kati ya hayo mawili…’ Tim Kyara. Siku ya kwanza:Tulijifunza ni kwa jinsi gani unaweza kuidhalilisha pesa nayo ikakukimbia Siku ya pili: Tulijifunza ni kwa njinsi gani twaweza tibu mahusiano yaliyovunjika Siku ya Tatu: Leo tutajifunza ukaribu wetu na baadhi ya watu unavyoweza athiri mahusiano yetu na pesa. ‘…Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema…’ ‘mwanadamu huzaliwa akiwa huru, lakini kila sehemu yuko na minyororo imemviringisha’ (man is born free, but everywhere he is in chain) Hii ni nukuu kutoka kwa Jacques Rousseau, Mfaranza mwenye philiosofia ya  siasa (1712 – 1778). Ni kwa nini anasema hivi? Kwa nini baadhi ya watu hupata pesa kirahisi sana kuliko wengine wenye kushishughulisha sana lakini huishia kupata kiduchu na kuweka kwenye mifuko yenye matundu, kwa kawaida mifuko hiyo huunganishwa na mabomba yanayozisafirisha pes...

Pesa - mwendelezo wa somo la jana

Jana katika kuongelea mahusiano yetu na pesa, tulijifunza sababu zinazofanya pesa ziwakimbie baadhi ya watu kila wakati na wakati huo huo hukimbilia kwenye mifuko ya watu wengine. Kama tulivyoona, pesa ni kitu chenye uhai chenye uwezo wa kuhusiana na ikitokea umeidhalilisha (umeitumia vibaya) basi mahusiano hayatadumu itabidi pesa ikukimbie. Hivyo leo katika ‘Mahusiano na pesa’ tutaangalia tiba juu ya mahusiano yaliyoharibika- pesa- mwanadamu-mahusiano. Tiba kwa mahusiano yaliyovunjika pesa-mahusiano na mtu Kabla hutujaanza kuangalia tiba juu ya mahusiano yaliyoathirika juu ya pesa, nafikiri ni muhimu tukaongelea baadhi ya Imani walizo nazo watu juu ya pesa ambazo zimekuwa kikwazo kiasi cha kutengeneza ukuta na kukosa kuwa na mahusiano yenye afya na pesa. Iwapo una Imani mbaya juu ya pesa, haijalishi unafanya nini kamwe hautafanikiwa kwa kuwa kimsingi Imani ni compass inayoongoza/kuendesha maisha yetu. Tunavuta na tuko jinsi tulivyo kutokana na tunavyoamini, na si vinginevyo. Ka...

Pesa

Naomba kabla sijaanza kuandika chochote nimshukuru sana Mchungaji Timoth Kyara ambaye ni rafiki na kocha wangu kwa jinsi alivyonifundisha na anaendelea kunifundisha juu ya pesa. Na mengi nitakayokushirikisha hapa ni yale nilijifunza kwake na baada ya kuona ni elimu murua ya kuweza kushirikisha wana karakana ya ubongo nikaamua kufanya hivyo. Karibu tuendelee. Kuna msemo wa kiingereza usemao ‘A fool and his money are soon parted’ pia ‘man is born free, but everywhere he is in chain’ by Jean Jacques Rousseau, French Political Philosopher (1972 – 1978). Kwa nini iko hivyo? Hivi umewahi kujiuliza inakuwaje baadhi ya watu kwao kupata pesa ni kitu raisi sana lakini kwa wengine ni kinyume kwani hujituma sana na kuishia kupata kiduchu ambapo huingiza kwenye mifuko iliyotoboka, kwa kawaida pesa za watu wa jinsi hii zimeungamanishwa na mabomba ambayo kimsingi pesa ikiingia tu mfukoni husafirishwa mara moja kwenda kusikojulikana na kumuacha mtu akiwa kapuku. Kama kuna kitu nataka ujifunze leo b...

Unakwenda wapi?

Mara nyingi unapokuwa umepewa maelezo ya eneo ambalo toka uzaliwe hujawahi kufika hakika utahitaji kupata namna itakayokuwezesha kufika huko utakako kwenda. Ashukuriwe Mungu kwa ubunifu aliompa mwanadamu katika suala la kusaidiana kufika maeneo ya ugenini kwani kuna vitu mbali mbali vimsaidiavyo mwanadamu kuweza kufika aendako. Nakumbuka mimi binafsi kwa mara yangu ya kwanza kwenda Marekani. Haikuwa jambo rahisi. Ninaye rafiki aishie Marekani na familia yake kwa muda sasa. Hivyo tuliandikiana na kunipatia namba zake za simu akiwa marekani na za mke wake na simu za nyumbani ili tu kutengeneza mazingira ya kupokelewa kirahisi na nisipate usumbufu nchi za watu na tena nchi yenyewe marekani. Nilimpatia details za ticket ambazo zilionesha hadi muda wa kuwasili Dallas. Simaanishi daladala maana vijana hamishi kusema mzee kateleza, hayo ni majina ya nchi za wenzetu. Eneo hilo liko TEXAS nchini Marekani. Nakumbuka aliniuliza swali moja unapokuja uwe unaniambia ndege unayokuja nayo maa...

Mambo Ya Kuzingatia Ili Kuwa Na Siku Yenye Tija.

Maisha tunayoishi yanahitaji nidhamu ili kuelekea kwenye mafanikio tunayotarajia. Leo naomba nikushirikishe yafuatayo:- 1. Kila siku unahitajika kupanga malengo unayotarajia kuyakamilisha siku inayofuata. Tendo hili ni vyema likafanyika usiku kabla ya kulala. Nakushauri uwe na noti buku maalum kwa ajili ya kuandika malengo yako ya kila siku. 2. Kuwa mtu wa matokeo na sio maneno – Utakumbuka nimewahi kukusisitiza kabla hujalala orodhesha mambo angalau sita unayotarajia kufanya siku inayofuata. Ninasisitiza tena kuhakikisha unafanya hivyo. Ukisha orodhesha, jiulize swali moja kuu – Kama utalazimika kufanya jambo moja tu kati ya hayo sita, je ni lipi utalipa kipaumbele na mengine ukayaacha. Tafadhali zungushia hilo jambo mara moja. Kitakachofuata ikiwezekana zima simu yako na mara moja anza kukifanya kwa kanuni ya kuwa ukianza hakuna mapumziko mpaka umemaliza ndipo waweza kujipa dk kumi au kumi na tano za kuanza kuandika mawazo (ideas) yatakayoanza kukujia kwenye kinotibuku chako ch...

Fanya Vitu Vingi Kwa muda mchache (Get more done in less time)

Maisha yanahitaji kujipanga. Acha kuishi kihasara. Wengi wetu hujishughulisha sana na vitu vingi visivyo na tija na kutusababishia uchovu na kwa kuwa havina matokeo makubwa shida nyingine huzaliwa  uhitaji wa pesa, msongo wa mawazo, mahusiano kuharibika, hujihisi hufai na kwa wenye Imani ndogo huishia kusema ukoo wetu una nuksi au nyota yangu imeibiwa. Leo napenda kwanza ujue ukweli huu Kanuni ya Pareto inasema asilimia 20 ya vitu tufanyavyo vina uwezo wa kutupa matokeo ya asilimia 80 na kwa upande mwingine asilimia 80 ya mambo tufanyayo hutuletea matokeo ya asilimia 20. Wengi wetu huishia kujishughulisha na vitu ambavyo ni asilimia 80 na tunapata matokeo asilimia 20. Mungu atusaidie tupange kufanya vitu vichache vyenye matokeo makubwa na tufurahie maisha. Tabia hii ya kufanya mambo mengi yasiyo na tija na kutufanya kila siku tuko hoi imesababisha ndoa nyingi ziyumbe maana wengi wameishia kulala mzungu wa nne na wengine wamegawana vyumba. Hii ni hatari. TUBADILIKE> Hapa nd...

Hakuna Eneo Salama

Ashukuriwe Mungu kwa pumzi aliyotupa siku ya leo. Ombi langu kwako ni moja tu asubuhi ya leo TUKAITENDEE KAZI HII PUMZI KWA MAAMUZI YETU NA ZAIDI SANA MATENDO YETU YA SIKU YA LEO. Yawezekana wewe ni mmoja wa watu wasio wepesi kujaribu vitu kufanya ukihofia labda kupata hasara au kuumizwa na mengine mengi ambayo ni vikwazo kwako kuchukua hatua. Kifupi ni mtu unayejipenda sana kiasi cha kuona kwamba hutaki kitu kiwayo chochote kibaya kikutokee na hivyo umebeba tabia ya kuwa mwangalifu kupitiliza (Overcautious behaviour). Naomba nikuonye – HUTOFIKA MBALI. Ukweli wa maisha ni huu – Tangu tunazaliwa hadi tunakufa hakuna sehemu yoyote iliyo salama. Mimi nakushangaa wewe unayetafuta sana kujilinda usipatwe na hasara/mabaya. Mifano michache upate kunielewa:- Tendo la wewe kuzaliwa tu lilijawa na hatari/hasara kibao, mojawapo ungeweza kuyatoa maisha ya mama akafa na ukaishi pasipo kumwona mama yako. Lakini hilo halitoshi, hata wewe mwenyewe ungeweza kupoteza maisha wakati wa kuzaliwa ...

Mwaka unafikia ukingoni, Nini Cha Kufanya?

Tunapokaribia mwisho wa mwaka kuna mambo ya muhimu ya kufanya. Hebu tenga muda ili kutathmini mwaka unaoishia katika maeneo makuu yafuatayo:- Mafanikio yako binafsi na ya kifani yameboreka? Umetoka wapi? Uko wapi? Na unakwenda wapi? Una akiba kiasi gani? Una madeni kiasi gani? Una miradi yenye thamani gani? Je uwekezaji wako umefikia hatua gani? Afya yako ikoje? Mahusiano yako na mwenzi wako yakoje? Je ni nini mafanikio yako 2017? Je waweza orodhesha? Nguo zipi hujawahi kuzivaa kwa mwaka mzima? Hebu zitenge pembeni Group lipi la watsApp hujawahi ingia na kusoma? Wesites zipi umedowload lakini huwajawahi soma Ingia store yako ya jiko - je kuna makolokolo kiasi gani? Je wajua jinsi ya kupunguza kiwango cha kulipa kodi ya mapato? Je una mlundikano wa magazeti yasiyokufaa kwa sasa? Msimamo unabaki pale pale ya kwamba hakuna mwaka mpya pasipo wewe kuwa mpya kwani mambo yatabaki kuwa yaleyale. Hata upate muda wa kupanga malengo ya mwaka bado mwaka utais...

Unaamini nini?

Mtu akisikia maongezi juu ya Imani haraka kinachokuja akilini ni masuala ya kiimani. Lakini mimi natataka kutabainisha mambo makubwa mawili yaani Imani juu ya Mungu na Imani juu yako wewe mwenyewe. Imani hizi mbili zina umuhimu mkubwa sana katika maisha. Ukweli ni kwamba usipomtanguliza Mungu katika shughuli zako au kama huamini kwamba Mungu yupo basi nisikufiche uko mahali pabaya. Mungu ni nambari moja katika kila shughuli tufanyazo. Mimi naamini hivyo. Nisingependa sana kujikita juu ya Imani juu ya Mungu kwani tu watu wa dini mbalimbali lakii yatosha kusema twawajibika kumtanguliza Mungu katika shughuli zetu. Sasa kikubwa ambacho nitaongelea kwa kina ni Imani iliyojengeka ndani yako tangu kuzaliwa hadi kufikia hapo ulipo. Imani huanza kwa kusikizishwa na kisha kuanza kujijengea mfumo ninaouita mfumo wa kiimani katika maeneo yafuatayo:- 1. Philosofia – mfumo ukuongozao kutenda mambo. Ni vyema ukajua mambo yanayokuongoza katika maisha. 2. Maono – Kimsingi mtu huona kwa kutumia ma...

Jifunze Kanuni/Sheria za Maisha Yalivyo

Tupo duniani tunaishi lakini sijui kama unajua ya kuwa tunaongozwa na kanuni au sheria ambazo kamwe huwezi zibadili. Hivyo ni vyema ukazijua kidogokidogo ili uweze jua jinsi ya kuendana nazo. Utakapotenga muda wako kujifunza sheria za dunia hii utasaidika na mambo makubwa mawili:- 1. Utajilinda na kuumizwa – Kikubwa hapa si kutozipenda sheria za dunia bali muhimu sana ni kupata taarifa za kutosha kuzijua hizo kanuni. Kwa kufanya hivyo utalijilinda na kuumizwa maana ikitokea hivi wajua hii ni kanuni lazima iwe hivi. Lakini ungalikuwa hujui ungeumizwa. Hakuna kitu kibaya kama mtu kuwa mjinga. Lakini upande mwingine ujinga huo ukikupelekea kuwa kapuku inakuwa mbaya Zaidi. Ila utapoteza kabisa maana ya wewe kuishi maisha haya pale itakapotokea ujinga wako umezalisha ukapuku na kupelekea kuwa kitandani ukiwa mgonjwa. Yaani u mjinga, tena kapuku na kama haitoshi u mgonjwa wa kushindwa kuamka kitandani. Unadhani unasubiri nini. Pambana kuondoa ujinga usikufikishe mahali pa kuwa mahututi. 2...

Tabia za Kimaendeleo

1. Kitu gani kinakusukuma ufanye. Hivi umewahi hata siku moja kukaa peke yako na ukajisemesha ya kuwa kama pesa sio tatizo hata kidogo ungeweza kufanya nini hapa duniani. Je hiyo orodha unayo? Orodha hii kimsingi inatakiwa kuwa ndefu angalau vitu au idadi ya mambo yasiyo pungua 100. Nakushauri kama zoezi hili hujawahi kufanya lifanye mara moja. Kuwa na fikra huru maana rasilimali pesa si tatizo tena, hebu orodhesha kila kitu ambacho unatamani kufanya iwapo pesa si tatizo. Ukisha pata hii orodha, anza kuipitia kwa kuweka mbele tarakimu yaani 1 ukimaanisha uwe umekipata baada yam waka mmoja, 2 baada ya miaka 2 hivyo hivyo 10 hata 20 itategemea nini umeorodhesha. Ukihitaji msaada nipigie tusaidiane. Hii jambo muhimu sana maana huzalisha msukumo wa kufanya mambo yatokee. 2. Kujiamini – Kinachomfanya mtu kuwa na nidhamu ni pale anapokuwa mtekelezaji wa mambo madogomadogo ya kila siku (Daily routine). Mfano kufanya mazoezi, kujisomea, kupangilia ratiba ya angalau mambo sita ya kufanya sik...