Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2017

Kukuza akili/ufahamu(mind development)

Habari ya leo mpendwa msomaji wa Makala zangu za kila siku sijulikanazo kwa jina la Wazo La Leo. Ni kawaida kusikia watu wakilalamika ya kuwa wanapenda sana kufanya biashara lakini tatizo hawana mtaji kuwawezesha kuanza biashara. Yawezekana hata wewe usomaye hii makala ni mmojawapo. Hili limewafanya walio wengi washindwe kuona mtaji wa kwanza ambao kila binadamu amezaliwa nao. Ikumbukwe na kuamini ya kuwa mwenyezi Mungu katika uumbaji wake alihakikisha kila binaadamu aliyemuumba alimkabidhi mtaji wa kuendesha maisha yake pasi shida yoyote. Mtaji ninaoongelea hapa ni AKILI. Akili ni kila kila kitu linapokuja suala la mchakato wa kutatua matatizo (changamoto). Shida kubwa kwa tulio wengi huwa hatutengi muda wa kufikiri na mbaya kuliko vyote hatuna tabia ya kukaa eneo tulivu ambalo ni muafaka kwa zoezi la kufikiri. Kuna nyakati akili zetu hutupa mawazo (Ideas) nzuri sana kutekeleza na kufanikisha kile tumekuwa tunakitafuta kwa muda mrefu lakini kwa kujua au kutokujua mawazo haya huja ...

Pata muda wa utulivu(Take time to be quite)

Habari za asubuhi mpendwa msomaji wa Makala za kila siku zijulikanazo kwa jina la Wazo La Leo. Leo nakwenda kuongelea PATA MUDA WA UTULIVU (TAKE TIME TO BE QUITE). Katika dunia hii tuliopo michaka michaka au kwa lugha nyepesi na kueleweka kwa walio wengi namaanisha ubize umetufikisha mahali tunashindwa kuwa na muda wa kutosha kutulia katika hali iliyojaa utulivu, Kinachoendelea katika maisha yetu ni kukimbizana, kukimbizana huku tukiwa tunasikilizishwa makelele yanayotuzunguka, mara siasa, mara ajali, mara raisi kasema lile, mara yanga na simba, mara Mugabe, basi ili mradi tunasikilizishwa kila kitu pasi kuchuja. Hii ni hatari kwa mstakabali wa maisha yetu. Kitu ninachotaka kukisema leo ni kwamba hatutakiwi kukubaliana na maisha yasiyo na uhalisia kwa mgongo wa kukimbizana kusiko na tija ya aina yoyote. Kila mtu bize na ukifatilia kinachomfanya mtu kuwa bize, utagundua ni ubize wa kumfananisha na mtu anayetengeneza pesa kwa kasi ya ajabu, lakini kumbe ni ubize wa kutengeneza madeni...

uwezo/nguvu ya mawazo (Ideas)

Leo ningependa kuongelea uwezo/nguvu ya mawazo (Ideas) ambayo kamwe huwezi kuyaweka kwenye mizania na ukasema hakika wazo au mawazo ya leo yana thamani sana au hata kumshukuru Mungu kwa namna uwazavyo na kupata mawazo/wazo murua kwa kuchukua hatua na kwa walio wengi maisha yamebadilika kwa kufanyia kazi mawazo (Ideas) ambazo kimsingi zimetoka ndani yao. Kitu ambacho ninaweza kukiwekea mkazo ni uwezo wa kutambua uwepo wa mawazo (Ideas) na ukawa katika nafasi ya kuelezea wazo/mawazo yako na ukaeleweka na anayekusikiliza. Yawezekana naongea na mtu ambaye hata namna ya kupakua hayo mawazo hajui. Naomba niongelee kidogo eneo hili. Kimsingi kila mtu anatakiwa awe na note book (Brain damping note book) angalau ya kutosha kuingia mfuko wa shati kwa ajili ya urahisi wa kubeba. Najua unamaswali ya kuniuliza: Je hichi kijinotibook kinatumikaje? Kimsingi upatapo wazo mara moja liandike kwenye hicho kijitabu kwani usipofanya hivyo mawazo hupotea na huwa ngumu kukumbuka. Yaani mwacheni Mungu ait...

Ukibadilika Kila Kitu Kina badilika

Namnukuu Jim Rohn ‘ Mafanikio ni pale unapokua umebadilika kiasi cha kuwa sumaku ya kuvuta mafanikio na wala usijidanganye kwa kufanya kazi sana kwa bidi ili kupata mafanikio. Mafanikio huvutwa na mtu aliyebadilika kiasi cha kuwa sumaku ya kuvuta mafanikio. Kubadilika ni shughuli pevu kushughulikia. Kazi kubwa ni kubadilika kifikra na hakuna njia nyingine Zaidi ya:- 1. Kujisomea vitabu kila siku na kupata maarifa mapya na unapochukua hatua ya kuyafanyia kazi mawazo mapya ndipo badiliko kamili kwako hutokea. Kwanini nasisitiza vitabu. Unaposoma kitabu kimoja unajifunza mambo ambayo yu mkini aliyekiandika imemchukua miaka 30 kuweza kuwa na hayo aliyoamua kuandika ili watu wengine waweze kujifunza. Hivyo kama utasoma kitabu kimoja kwa mwezi tafsiri yake ni kuwa umeweza kujifunza udhoefu wa mtu wa miaka 30 kwa mwezi mmoja. Sasa niambie utakapokuwa umesoma vitabu hamsini utakuwaje? Badiliko ni lazima na linanzia na fikra kwa kujaza mambo yenye tija na fikra taka kuondoka. 2. Kusikiliza/vi...

Tabia tatu muhimu zinazotenganisha matajiri na masikini

Naomba nisaidie kuendelea kumshukuru Mungu kwa wingi wa rehema katika maisha yetu. Naamini umeamka ukiwa mwenye afya njema na tayari kuianza siku kwa shauku kubwa ya kufanya makuu. Karibu katika wazo la leo ambapo tunakwenda kujifunza tabia tatu muhimu zinazotenganisha matajiri na masikini ambazo natamani wewe rafiki yangu uweze zijua na hatimae unajua nini faida yake katika maisha yako kwani wahenga walisema kumjua adui ni nusu ya ushindi. Kwanza kabisa natanguliza wazo lenye kukufanya uchangamke unapolitafakari – Hivi ni kwa nini wale walio ajiriwa (wafanyakazi) na kumtumikia mwajiri wao, wengi wao hawana shughuli za ziada kuwasaidia kufupisha safari ya mafanikio? Wengi wamebweteka na uhakika wa msharahara. Naomba nitoe angalizo kwa walioajiriwa wote. 1. Uhusiano wako na mwajiri wako ni kwa vile una siha nzuri kuweza kumzalishia na hivyo anahakikisha anakurubuni na vitu mbalimbali ili ujione umefika kama vile posho, pesa ya ziada kwa kazi za ziada, mikopo, pesa ya likizo, bima ya...

Hakuna Eneo Salama

Ashukuriwe Mungu kwa pumzi aliyotupa siku ya leo. Ombi langu kwako ni moja tu asubuhi ya leo – TUKAITENDEE KAZI HII PUMZI KWA MAAMUZI YETU NA ZAIDI SANA MATENDO YETU YA SIKU YA LEO. Yawezekana wewe ni mmoja wa watu wasio wepesi kujaribu vitu kufanya ukihofia labda kupata hasara au kuumizwa na mengine mengi ambayo ni vikwazo kwako kuchukua hatua. Kifupi ni mtu unayejipenda sana kiasi cha kuona kwamba hutaki kitu kiwayo chochote kibaya kikutokee na hivyo umebeba tabia ya kuwa mwangalifu kupitiliza (Overcautious behaviour). Naomba nikuonye – HUTOFIKA MBALI. Ukweli wa maisha ni huu – Tangu tunazaliwa hadi tunakufa hakuna sehemu yoyote iliyo salama. Mimi nakushangaa wewe unayetafuta sana kujilinda usipatwe na hasara/mabaya. Mifano michache upate kunielewa:- 1. Tendo la wewe kuzaliwa tu lilijawa na hatari/hasara kibao, mojawapo ungeweza kuyatoa maisha ya mama akafa na ukaishi pasipo kumwona mama yako. Lakini hilo halitoshi, hata wewe mwenyewe ungeweza kupoteza maisha wakati wa kuzaliwa au hu...

Makundi manne ya watu

Ninamshukuru sana Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa siku nyingine nzuri yenye baraka ambayo tunakwenda kuitumia vizuri ili kuboresha maisha yetu. Leo tunakwenda kujifunza kwa pamoja juu ya makala inayokujia kila siku ijulikanayo kwa jina la “Wazo La Leo”. Hivyo kwa leo nitajikita zaidi kuelezea makundi makubwa manne ya watu linapokuja suala la muda na fedha/kipato/shekeli. Nini maana ya haya makundi? Na je we uko kundi lipi. Sipendi na wala sihitaji unitajie kundi lako acha ibaki kuwa siri yako. Lakini upande wa pili wa shillingi nakuuliza iwapo kila kitu kingekuwa sawia kiasi cha kujichagulia kundi mubashara, je wewe ungejichagulia kundi lipi kati ya hayo manne? Majibu yote juu ya maswali hayo manne yanabaki ndani ya nafsi yako usije nizulia kesi ati nimekwambia uko kundi flani acha ibaki kuwa msala wako. Kikubwa ufanye nini kutoka kundi ulilopo ambalo pasipo kumung’unya maneno uko kundi la hasara au kwa lugha nyepesi hujatambua ulikuja duniani kufanya nini? Wengi hudhani lengo la...

Ushauri wa bure

Naamini kwa rehema za Bwana sote tu wazima. Leo ninakuja na ujumbe juu ya ushauri wa bure: 1. Katika maisha hakikisha unajiwekea msimamo ya kuwa unapofanya shughuli yoyote Ile hulegezi mikono lakini pia unaifanya kwa kiwango cha juu/ubora (make commitment to your excellence). 2. Ishi maisha yenye ujasiri kwani tunakabiliwa na maadui wakuu wawili ambao wamekuwa wakitushika na kutuvuta. Maadui Hawa ni hofu ya kushindwa na hofu ya kukataliwa. Jenga tabia ya kujisemesha ya kuwa unaweza kufanya.... Kamwe usiruhusu hofu kukushida. 3.Kujitoa (commitment) - Naona vyema nikatoa mfano ili kuweza mjua mtu mwenye tabia ya kujitoa. Tumchukulie mtu anayefanya kazi ya kuuza vyombo vya nyumbani ain't mauzo ya chochote like. Mtu WA Hindi hii ana kazi kubwa ya kufanya kazi yake akiwa na hamasa na tabasam mubashara. Hapo ni lazima auze kwani ameonyesha kujitoa kweli kweli na cha ajabu ni kwamba kwa kila mtu afanye biashara ya kuuza kuna siri nzito imejificha kwenye hamasa na tabasam mubashara kwan...

Uzalishaji

Karibu mfuatiliaji wa Makala sijulikanazo kama wazo la leo. Leo nimeonelea vyema niongelee juu ya nafasi yako katika uzalishaji, iwe umeajiliwa au unajishughulisha na shughuli binafsi – huna budi kujiweka katika nafasi itakayokufanya uwe mtu wa thamani katika uzalishaji na kwa uhakika utashangaa uzalishaji wako ukipanda kwa kasi maana utasaidika iwapo utafuata ushauri ambao ninakwenda kuuachilia kwako. Kimsingi hakuna mwanadamu anayehitaji kuishi maisha yasiyokuwa na maana. Wengi wetu tunaishi pasipo kuwa na mwalimu/mentor/coach katika maisha. Naomba nikutangazie kuishi kwa namna hiyo kutakucheleweshea mafanikio yako. Ushauri wangu kwako chukua hatua haraka za kumtafuta mtu atakaye kuwa anakuongoza katika maisha. Amini usiamini ukichukua hatua utajionea mwenyewe maisha yako yanavyoanza kuboreka. Sijui naongea na mtu wa jinsi gani, lakini kwangu umri ni namba tu, vinginevyo hauna maana yoyote kimaisha kwani waweza badilisha maisha yako katika kipindi chochote. Jambo ninalotaka kusisit...

Uzalishaji

Karibu mfuatiliaji wa Makala sijulikanazo kama wazo la leo. Leo nimeonelea vyema niongelee juu ya nafasi yako katika uzalishaji, iwe umeajiliwa au unajishughulisha na shughuli binafsi – huna budi kujiweka katika nafasi itakayokufanya uwe mtu wa thamani katika uzalishaji na kwa uhakika utashangaa uzalishaji wako ukipanda kwa kasi maana utasaidika iwapo utafuata ushauri ambao ninakwenda kuuachilia kwako. Kimsingi hakuna mwanadamu anayehitaji kuishi maisha yasiyokuwa na maana. Wengi wetu tunaishi pasipo kuwa na mwalimu/mentor/coach katika maisha. Naomba nikutangazie kuishi kwa namna hiyo kutakucheleweshea mafanikio yako. Ushauri wangu kwako chukua hatua haraka za kumtafuta mtu atakaye kuwa anakuongoza katika maisha. Amini usiamini ukichukua hatua utajionea mwenyewe maisha yako yanavyoanza kuboreka. Sijui naongea na mtu wa jinsi gani, lakini kwangu umri ni namba tu, vinginevyo hauna maana yoyote kimaisha kwani waweza badilisha maisha yako katika kipindi chochote. Jambo ninalotaka kusisit...

Kujenga mfumo wa maisha wenye tija.

Habari za asubuhi mfuatiliaji wa masomo ya kila siku kwa jina maarufu la wazo la leo.Leo nimeonelea vyema nigusie juu ya kujenga mfumo wa maisha wenye tija. Ninapokwenda kuelezea hili napenda kila mmoja atambue jambo moja ya kuwa mwanadamu kwa asili ni mvivu au kwa lugha nyingine miili yetu kwa asili inapenda kustarehe au kwa msisitizo kubweteka. Wahenga walisema, kumjua adui ni nusu ya ushindi kwani inakuwia rahisi kupanga mikakati ya maangamizi. Shida kubwa kwa mwanadamu ni kwamba vita hii ni ya kila siku na mbaya Zaidi adui huyu unaye kila uendako na achelei kukusemesha. Mwili unaongea sana na ukiuendekeza utakuletea madhara maishani. Lugha kama nimechoka, siwezi, acha nipumzike, raha jipe mwenyewe na mengine mengi yanadhihirisha asili ya mwili na hapo mwili unakusemesha mpaka uutimizie. Wapo watu wametengeneza tiba kuhakikisha mwili unatia adabu. Mfano – Kimsingi mwanadamu anayejitambua ni lazima awe nje ya kitanda kabla au saa 11 asubuhi. Nachelea kusema hiyo ni kama kanuni, uw...

Matumizi ya whatApp na simu.

Habari za leo rafiki na mfuatiliaji wa Makala zangu zijulikanazo kwa jina la wazo la leo. Leo nimeona vyema nizungumzie juu ya matumizi ya na whatApp na simu. Maendeleo ya technologia yametuletea ulimbukeni uliokithiri. Utakuta mtu kutwa nzima yuko kwenye watsApp utafikiri ni mfanyakazi wa mgodi wa Buswagi amepangiwa shift na haruhusiwi kutoka inamlazimu akazane kuchimba madini. Ukifuatilia kwa makini unagundua tayari mtu amekwisha kuwa teja wa watsApp maana haipiti dk mara kujiselfie na kutuma mara kapokea picha ya mwenzake anakula, mara katumiwa picha za watu waliokufa kwa ajali mara Diaomond mara nini yaani taja uwezayo. Akilala usiku ni mang’amung’amu maana mapicha mchanganyiko kichwani yanaanza kumsumbua. Utakuta kakurupuka kitandani ati anaota wanataka kumua na vituko vya kila aina. Huo ni ulimbukeni na uteja wa hali ya juu. Ukifuatilia hali ya uchumi utakuta hoi bin taabani. Unakuta mtu ni rafiki tu wa facebook hata hamjawahi onana anakuomba pesa ya bando. Tunakwenda wapi? N...

Maswala muhimu ya kujiuliza

Ninamshukuru Mungu kuiona siku nyingine tena. Leo nataka niongelee maswali muhimu maishani yampasayo kila mtu kujiuliza. Ikumbukwe kwamba tunakaribia kuanza Mwaka mpya kwani tumebakiwa na mwezi mmoja tu. Hivyo nimeonelea vyema niongelee maswali manne muhimu mwanadamu anayejitambua hana budi kujiuliza katika maisha haya tuliyo nayo:- 1. Ni nini 2. Lini 3. Kwa nini 4. Kwa namna gani Kimsingi kila mmoja wetu hana mudi kujua kusudio la yeye kuruhusiwa kuwepo hapa duniani. Kumbuka hatukuja kupumua tu tukapita. Liko kusudio maalum ambalo Mungu ameweka ndani yako ambalo anataka ulitimize. Mimi na wewe yawezekana kabisa hatujawahi kukutana ana kwa ana ila uhakika nilio nao ni kwamba wewe ni mtu wa thamani sana kwani una uwezo mkubwa ajabu wa kuweza badilisha kabisa maisha yako na ukabaki kuwa simulizi. Hivyo kujua kwa hakika kusudio lako la kuwepo hapa duniani ni jambo kuu na la maana kwa kila mmoja wetu. Kujua ni nini unahitaji si mwisho na kiuhakika hupoteza maana hadi pale utakapoju...

Mwonekano Wako ‘Unaongea’

Siku zote hakikisha mwonekano wako unakuongelea chanya. Kamwe usiondoke nyumbani kwako bila kuwa na hisia ya kwamba mwonekano wako ndio unaokuelezea unavyo hitaji kujitambulisha ya kuwa wewe ni mtu wa namna gani. Tangazo pekee lililo la ukweli duniani kupata kutokea kubandikwa linasomeka ‘VAA SAHIHI’. Ni rahisi kuonyesha dosari ya aina fulani kwa mtu kwa jinsi anavyonekana tu. Kiukweli si haki, lakini ndio ukweli wenyewe. Upende usipende ndio mambo yanayoendelea kila siku kwenye maisha yetu. Kuwa sharp kwani faida yake ni kukusaidia kufikiri kwa usharp (Look sharp because it will help you think sharp). Unajua hata tembea ya kizembe inaathiri ufikiri. Tembea ukijiamini. Watu wengine wanatembea utadhani muda wowote ule anaanguka. Mwonekano wako kwa nje una athari ya jinsi unavyofikiri na kujisikia kwa ndani. Mwonekano wako unaongea kwako; lakini pia unaongea kwa wengine. Heshimu mwonekano wako. Ili kujihakikishia unajiheshimu jiulize swali moja tu – Je nauzika. Wewe ni bidhaa. J...

Wazo La Leo

Ninamshukuru sana Mungu kuiona siku ya leo. Leo napenda kuzungumzia juu ya nguvu ya hamasa. Naliongelea hili ili kila mtu aone jinsi anavyoweza kujiwezesha kuwa katika hisia chanya. Kimsingi napenda kila mmoja ajue ukweli kwamba katika kila hali kuna chaguzi tunafanya. Kitendo hichi cha kufanya uchaguzi ni takribani cha kila siku au kwa lugha nyingine ndio maisha yetu ya kila siku lazima ufanye chaguzi. Ili kuweza kupata uelewa vizuri wa kujiwezesha kuwa na hisia chanya naomba nikupitishe katika vipengele vifuatavyo:- Hofu - wakati wowote tunapokuwa watu wa kushughulikia hali iliyotufanya tupoteze amani au furaha tuliyokuwa nayo matokeo yake tunajawa na hofu ya kupata maumivu zaidi. Maumivu haya kamwe sio halisia bali ni onyo ya kuwa kama mambo hayatobadilika, basi hali iliyo mbele yetu itakuwa mbaya zaidi. Hili lawezea kukutokea katika maisha. Mfano unapofukuzwa kazi ghafla, huingiwa na hofu ya maisha kuwa chini ya kiwango ulichokuwa ukiishi kwa sababu ya uhakika wa mshahara na...

Wazo La Leo:

Tunaishi nyakati ambazo Ninaziita ni nyakati za habari (Information age). Taarifa vidoleni. Ukweli ni kwamba upande mmoja wa shilingi ni jambo Jema sana lakini upande wa pili ni jambo baya sana. Kwa nini tuseme hayo. 1. Ni nyakati nzuri kwa sababu sasa hutumii nguvu na gharama nyingi kupata taarifa kwani ziko kiganjani. 2. Kipindi hichi ni kibaya kwa sababu taarifa nyingi ni mbaya kusikiliza na hata kuangalia, hivyo sehemu ya pili ya ubongo wako inayoitwa subconscious mind inaathirika sana. Na kumbuka sehemu hii ya akili kwanza huna udhibiti nayo lakini ndiyo eneo unalolitegemea kwa 90%. Kazi ya eneo hili ni kurekodi kila kitu unachosikia na unachoona na pili inaamsha matendo ambayo wewe huna udhibiti nayo. Nitakupa mfano mdogo na kwa kuwa site ni watu wazima tutaelewana. Chukulia mtu anayependa kuangalia Picha za ngono sana. Kinachozalishwa ni kwamba tabia za mtu huyu zitaanza kujifunua kwa kufanya ngono sana mpaka jamii ikamtambua hivyo lakini mwenyewe akifanya anajutia kwa kuwa ...